Tom anabeba tenga la ndizi zilizoiva.
Tom bærer en kasse med modne bananer.
Tom anaenda sokoni kuuza ndizi.
Tom går til markedet for at sælge bananerne.
Sokoni watu wananunua matunda.
Folk på markedet køber frugt.
Lakini hakuna anayenunua ndizi za Tom. Wanapenda kununua matunda kutoka kwa akina mama.
Men ingen køber Toms bananer. De vil hellere købe frugt fra kvinder.
“Kwenye jamii yetu, ni wanawake pekee ndio wanaouza matunda,” watu wanasema. “Ni mwanamume wa aina gani huyu?” watu wanahoji.
“Her i området er det kun kvinder, der sælger frugt,” siger folk. “Hvad er det her for en mand?” spørger folk.
Lakini Tom hakati tamaa. Anaita, “Nunua ndizi zangu! Nunueni ndizi zangu tamu zilizoiva!”
Men Tom giver ikke op. Han råber: “Køb mine bananer! Køb mine søde, modne bananer!”
Mwanamke mmoja anachukua kichane cha ndizi kutoka kwenye tenga. Anaziangalia ndizi kwa umakini.
En kvinde tager en klase bananer fra kassen. Hun ser omhyggeligt på bananerne.
Watu wengine wanakuja kwenye kichanja. Wananunua ndizi za Tom na kuzila.
Flere mennesker kommer til boden. De køber Toms bananer og spiser dem.
Mara, tenga linakuwa tupu. Tom anahesabu pesa alizopata.
Snart er kassen tom. Tom tæller de penge, han har tjent.
Tom ananunua sabuni, sukari, na mkate. Anaweka vitu kwenye tenga lake.
Så køber Tom sæbe, sukker og brød. Han lægger tingene i sin kasse.
Tom anajitwisha tenga kichwani na kwenda nyumbani.
Tom balancerer kassen på hovedet og går hjem.