Download PDF
Back to stories list

Nozibele no fuuk tolu Nozibele na nywele tatu

Written by Tessa Welch

Illustrated by Wiehan de Jager

Translated by Aurelio da Costa

Read by Aurelio da Costa, Vitalina dos Santos, Criscencia R. Da Costa Viana

Language Tetum

Level Level 3

Narrate full story

Reading speed

Autoplay story


Tempu uluk liu ba, labarik feto nain tolu ba hili ai.

Hapo zamani za kale, wasichana watatu walienda kukusanya kuni.


Loron ne’e manas ho nune’e sira ba iha mota atu nani. Sira halimar no nani no kari bee ba malu iha bee laran.

Ilikuwa ni siku yenye jua kali na wakaamua kwenda mtoni kuogelea. Wakaogelea huku wakicheza na kurushiana maji.


Derepente, sira realiza katak tarde ona. Sira la’o fila lalais ba suku.

Ghafla waligundua kuwa muda umekwenda. Wakaharakisha kurudi nyumbani.


Bainhira sira besik uma, Nozibele hasa’e ninia liman ba ninia kakorok. Nia haluha tiha ona ninia korrente! “Favor mai fali ho ha’u!” Nia husu ba ninia belun. Maibé ninia belun sira dehan ne’e tarde loos ona.

Walipokuwa wanakaribia kufika nyumbani, Nozibele akajishika shingoni. Alikuwa amesahau shanga zake! “Tafadhali turudini!” aliwasihi rafiki zake. Lakini rafiki zake wakasema tumechelewa.


Ho nune’e Nozibele mesak mak ba fali mota mesak. Nia hetan ninia korrente no halai fila ba uma. Maibé nia lakon iha nakukun laran.

Kwa hiyo Nozibele akarudi mwenyewe mtoni. Akapata shanga zake na akakimbia kurudi nyumbani. Lakini akapotea gizani.


Husi dook nia haree naroman mai husi uma du’ut ida. Nia halai ba ne’eba no dere odamatan.

Kwa mbali akaona mwanga unatoka kwenye nyumba. Akakimbilia kwenye nyumba na kugonga mlango.


Ba ninia surpreza, asu ida mak loke odamatan no dehan “Saida mak o hakarak?” “Ha’u lakon no ha’u presija fatin ida atu toba, “Nozibele hateten. “Tama mai, se lae ha’u sei tata o!” asu ne’e dehan. Entaun Nozibele tama ba laran.

Akastaajabu kumwona mbwa akifungua mlango na akasema, “Unataka nini?” “Nimepotea na ninatafuta sehemu ya kulala,” akasema Nozibele. “Ingia ndani, la sivyo nitakung’ata!” mbwa akamwambia. Nozibele akaingia ndani.


Depois asu ne’e dehan, “Te’in ba ha’u!” “maibé ha’u nunka te’in ba asu ida antes,” nia responde. “Te’in, se lae ha’u sei tata o!” Asu ne’e dehan. Ho nune’e Nozibele te’in hahán balun ba asu ne’e.

Mbwa akamwambia, “Nipikie!” “Sijawahi kumpikia mbwa,” akajibu. “Pika, la sivyo nitakung’ata!” mbwa akasema. Nozibele akampikia mbwa chakula.


Depois asu ne’e dehan, “Prepara ha’u nia toba fatin!” Nozibele hatan, “Ha’u nunka prepara toba fatin ida ba asu ida.” Prepara fatin ne’e, se lae ha’u sei tata o!” Asu ne’e dehan. Ho nune’e Nozibele prepara fatin toba ne’e.

Mbwa akamwambia, “Nitandikie kitanda!” Nozibele akajibu, “Sijawahi kumtandikia mbwa kitanda.” “Tandika kitanda, la sivyo nitakung’ata!” mbwa akasema. Nozibele akatandika kitanda.


Loron loron nia tenke te’in no dasa rai no fó hariis asu ne’e. Hafoin loron ida asu ne’e dehan, “Nozibele, ohin loron ha’u tenke vizita kolega sira balun. Dasa uma laran, te’in hahán no fase ha’u nia sasán molok ha’u fila.”

Akawa kila siku anampikia, anamfulia na kumfagilia mbwa. Siku moja mbwa akasema, “Nozibele, leo naenda kuwatembelea rafiki zangu. Fagia nyumba, pika chakula na osha vitu vyangu kabla sijarudi.”


Iha kedas momentu asu ne’e ba, Nozibele foti fuuk tolu husi ninia ulun. Nia tau fuuk ida iha kama okos, ida seluk iha odamatan kotuk no seluk ida iha Kraal (kraal= uma du’ut tradisional Afrika nian). Hafoin nia halai maka’as fila ba uma.

Mara baada tu ya mbwa kuondoka, Nozibele akanyofoa nywele tatu kutoka kwenye kichwa chake. Akaweka unywele mmoja chini ya kitanda, mmoja nyuma ya mlango, na mwingine akauweka kwenye uzio wa nyumba. Halafu, akakimbia kuelekea nyumbani kwa nguvu zote.


Bainhira asu ne’e fila mai, nia buka Nozibele. “Nozibele, o iha ne’ebé?” Nia hakilar. “Ha’u iha ne’e, iha kama okos,” fuuk primeiru hatan. “Ha’u iha ne’e, iha odamatan kotuk,” fuuk segundu hatan. “Ha’u iha ne’e, iha kraal,” fuuk terseiru hatan.

Mbwa aliporudi akaanza kumtafuta Nozibele. “Nozibele, uko wapi?” akapiga kelele. “Niko hapa, chini ya kitanda,” unywele wa kwanza ukajibu. “Nipo hapa nyuma ya mlango,” unywele wa pili ukajibu. “Niko hapa kwenye uzio,” unywele wa tatu ukajibu.


Depois asu ne’e hatene katak Nozibele lohi tiha ona nia. Entaun nia halai no halai ba iha suku. Maibé Nozibele ninia maun sira hein nia ho ai-sanak tolu. Asu ne’e fila no halai no nunka haree hetan dezde momentu ne’e.

Mbwa akagundua kuwa Nozibele amemkimbia. Kwa hiyo akakimbia kuelekea kijijini. Kaka zake Nozibele walikuwa wakimsubiri na fimbo. Mbwa alipowaona akageuka na kukimbia, na hajawahi kuonekana tena.


Written by: Tessa Welch
Illustrated by: Wiehan de Jager
Translated by: Aurelio da Costa
Read by: Aurelio da Costa, Vitalina dos Santos, Criscencia R. Da Costa Viana
Language: Tetum
Level: Level 3
Source: Nozibele and the three hairs from African Storybook
Creative Commons License
This work is licensed under a Creative Commons Attribution 3.0 International License.
Options
Back to stories list Download PDF