Download PDF
Back to stories list

Umwana wakwa Punda Mtoto Punda

Written by Lindiwe Matshikiza

Illustrated by Meghan Judge

Translated by AGNES CHIBAMBA

Language IciBemba

Level Level 3

Narrate full story The audio for this story is currently not available.


Umukashana umunono ewabalilepo ukumona icinjelengwe akatalamukila.

Ilikuwa ni msichana mdogo aliyekuwa wa kwanza kuona umbo la ajabu kwa mbali.


Ilyo icinjelengwe cafikile mupepi, amwene ukuti ni namayo uwali sana pabukulu.

Kadiri umbo lilipokaribia, aliona kwamba lilikuwa ni mwanamke mwenye ujauzito mkubwa.


Nensoni shakwe, umukashana umunono alikosela na ukupalama mupepi na namayo. “Tufwile twamusunga pamo naifwe, “umukashana umunono uwatemenwe ukwikala na bantu ali ipeleshe. “Tulemusunga bwino na umwana wakwe.”

Kwa upole na ujasiri, msichana alimsogelea mwanamke yule. “Lazima tumhifadhi,” watu wa msichana yule walisema. “Tutawaweka yeye na mtoto wake salama.”


Panonofye umwana ali munshila. “Sunka!” “Leta amalangeti!” “Amenshi!” “Suunkaa!!!”

Mtoto alikuwa njiani kuzaliwa si muda mrefu. “Sukuma!” “Leteni mablanketi!” “Maji!” “Suuukuuumaaaa!!!”


Nomba ilyo bamwene umwana, bonse balitolokela kunuma mu kusunguka. “Punda?”

Lakini walipomwona mtoto, wote waliruka kwa mshtuko. “Punda?!”


Bonse batampile ukusushanya. “twacitila tulesunga umwana naba nyina mutende, efyo twalacita, “efyo bamobamo basosele. “Nomba bakatuletela ishamo!” efyo bambi basosele.

Wakaanza kubishana. “Tulisema tutawaweka mama na mtoto salama, na hivyo ndivyo tutakavyofanya,” baadhi wakasema. “Lakini watatuletea mkosi!” wengine wakadai.


Efyo nomba namayo aisangile eka nakabili. Taishibe ifyakucita na icinjelengwe ca mwana. Taishibe ifyakucita umwine.

Kwa hiyo mwanamke yule alijikuta yuko peke yake kwa mara nyingine tena. Akajiuliza atafanya nini na mtoto huyo wa ajabu. Akajiuliza atafanya nini na yeye mwenyewe.


Panuma alisuminafye ukuti ali mwana wakwe elyo nao ali ninyina.

Lakini hatimaye alikubali kwamba huyo ni mwanaye na yeye ni mama yake.


Nomba, ngacakuti umwana talekula, alifye umunono, fyonse nga fyalipusana. Lelo umwana wa punda alikulile sana icakuti aleka ukukumana mu numa yaba nyina. Elyo nangu eshe shani, ificitwa fyakwe tafyali fya buntu. Inshita yonse ba nyina balifye abanaka na icifukushi. Limo limo balemupela incito sha nama.

Endapo mtoto huyo angebaki kuwa vilevile, na umbo dogo, labda kila kitu kingekuwa tofauti. Lakini mtoto Punda aliendelea kukua na kukua mpaka hakuweza kutoshea tena mgongoni mwa mama yake. Pamoja na kujaribu kwa bidii, hakuweza kuwa na tabia za kibinadamu. Mara nyingi mama yake alichoka na kuvunjika moyo. Wakati mwingine alimlazimisha kufanya kazi walizostahili wanyama.


Punda alifye awa lubana elyo atampile ukumfwa na icifukushi. Teti acite icili conse. Teti abe ifili fyonse. Ali fulilwe sana icakuti, ubushiku bumo, alipantile ba nyina bapona na panshi.

Kuchanganyikiwa na hasira vilianza kujengeka ndani mwa Punda. Alishindwa kufanya hivi wala vile. Alishindwa kuwa hivi wala vile. Alipatwa na hasira sana kiasi kwamba, siku moja, alimpiga teke mama yake mpaka akaanguka chini.


Punda alyumfwile insoni. Atampile ukubutuka ukuya ukutali sana.

Punda alijawa na aibu. Akaanza kukimbilia mbali kwa haraka kadiri awezavyo.


Ilyo Punda alekele ukubutuka, palifita, aluba na ukuluba. “Hee haw?” atotosha munfifi panono panono. “Hee Haw?” Iciunda caumfwika. Ali eka. Aipeteka sana, apona namutulo utwine twine utwamalangulushi.

Wakati aliposimama, ilikuwa ni usiku, na alikuwa amepotea. “Hii hoo?” alinong’ona gizani. “Hii hoo?” giza likatoa mwangwi. Alikuwa mwenyewe. Alijikunyata katika umbo dogo, akalala fofofo usingizi wa mang’amung’amu.


Punda ukubuka asanga shikulu bantu uwo taishibe alemulolesha. Alolesha mu menso yakwa shikulu bantu atendeka ukumfwa icicetekelo.

Punda aliamka na kumkuta mzee mmoja wa ajabu akimtazama. Akamwangalia mzee yule machoni na akaanza kuhisi ishara ya matumaini.


Punda aile mu kwikala na shikulu bantu, uwa mufundile inshila sha kwikalilamo ishingi. Punda alyumfwile na ukusambilila, cimo cine na shikulu bantu. Baleyafwana na ukusekela pamo.

Punda alienda kuishi na mzee yule, na mzee alimfundisha mbinu nyingi za kuishi. Punda alisikiliza na kujifunza, na mzee vivyo hivyo pia. Walisaidiana na kucheka pamoja.


Ubushiku bumo, shikulu bantu aipwishe punda ukumusenda pamulu wa lupili.

Asubuhi moja, mzee alimwomba Punda ambebe hadi kwenye kilele cha mlima.


Pamulu mu makumbi basendama. Punda alotele banyina abalwele balemwita. Ilyo abukile…

Walipofika juu kwenye mawingu, walipatwa na usingizi. Punda akaota kuwa mama yake alikuwa mgonjwa na alimhitaji. Na alipoamka…


…amakumbi yaliya pamo na umunankwe, shikulu bantu.

…mawingu yalikuwa yametoweka pamoja na rafiki yake, yule mzee.


Panuma punda alishibe ifyakucita.

Hatimaye, Punda alijua alichotakiwa kufanya.


Punda alisangile ba nyina, beka balelosha umwana uwalubile. Baliloleshanya akashita akatali. Elyo bakumbatana sana.

Punda alimkuta mama yake akiwa peke yake huku akimwomboleza mwanaye aliyepotea. Wakaangaliana kwa muda mrefu. Na kisha wakakumbatiana kwa hisia.


Umwana wa donkey na banyina bali kulila pamo elyo balisanga inshila ishingi ishakwikala pamo. Panono panono, bonse ababashinguluka, balupwa bambi balitampa ukwikala bwino.

Mtoto Punda na mama yake wamekuwa kitu kimoja na kuishi kwa ushirikiano. Taratibu, familia nyingine zimeanza kuhamia na kuishi miongoni mwao.


Written by: Lindiwe Matshikiza
Illustrated by: Meghan Judge
Translated by: AGNES CHIBAMBA
Language: IciBemba
Level: Level 3
Source: Donkey Child from African Storybook
Creative Commons License
This work is licensed under a Creative Commons Attribution 4.0 International License.
Options
Back to stories list Download PDF