Download PDF
Back to stories list

Nankoko na Pungwa Kuku na Tai

Written by Ann Nduku

Illustrated by Wiehan de Jager

Translated by Sandra Mulesu

Language IciBemba

Level Level 3

Narrate full story The audio for this story is currently not available.


Patile akantu, kaikele ngefi, nankoko na pungwa bali fibusa. Baleikala mumutende nefyuni fimbi. Tapali nefyalepupuka.

Hapo zamani za kale, Kuku na Tai walikuwa marafiki. Waliishi kwa amani na ndege wengine. Hakuna kati yao aliyeweza kupaa.


Bushiku bumo, kwaliponene insala. Pungwa aile alefwaya ifyakulya ukutali sana. Abweleleko ninshi nanaka sana. “Kufwile kwaba inshila yakwendelamo ukwabuka ukucula!”

Kuna siku njaa ilitokea. Ikamlazimu Tai kutembea umbali mrefu kutafuta chakula. Alirudi akiwa amechoka sana. “Lazima kuwe na njia rahisi ya kusafiri!” Tai alisema.


Panuma yakubuka ulucelo, Nankoko epakusanga inshilaimo iisuma. Efyo ayambile uku longanya amasako yaponene kufyuni fimbi. Tiyeni tubililile pamo aya amasako pamulu waaya twakwata. Limbi kuti catwangukilako mumyendele”.

Baada ya usingizi mnono wa usiku, Kuku alijiwa na wazo zuri sana. Akaanza kukusanya manyoya yaliyodondoka kutoka kwa ndege wenzao. “Tuyashonee haya manyoya juu ya manyoya yetu,” Kuku alisema. “Labda itaturahisishia kusafiri.”


Pungwa ewalifye nakela mumushi, ewabalilapo nokubila. Aipangila amapindo ayasuma sana nokupupukila mumulu umutali. Inkoko epakwashima akela, nomba yalifilwa ukubila kumulandu wakunaka. Epakusha akela pa kabati, nokuya mukupekanya ifyakulya fyabana.

Tai pekee ndiye aliyekuwa na sindano kijijini, kwa hiyo akaanza kushona wa kwanza. Akajitengenezea mabawa mawili mazuri na akapaa juu ya kuku. Kuku aliazima sindano lakini akachoka kushona baada ya muda mfupi. Akaacha sindano kabatini na akaenda jikoni kuandaa chakula kwa ajili ya watoto wake.


Nomba ifyuni fimbi fyalimwene uko pungwa apupwike. Epakulomba nankoko ukubashimako akele pakuti nabo babilileko amasako. Mukashitafye akanono, ifyuni ifing fyayamba ukulapupuka mumulu.

Lakini ndege wengine walimwona Tai akipaa. Wakamwomba Kuku awaazime sindano ili nao wajishonee mabawa pia. Muda si mrefu ndege wakawa wamepaa na kuzagaa anga zima.


Elyo icuni cakulekelesha caishile mukulomba akela, nankoko talipo. Efyo abana bakwe basendele akela nokwamba ukwangasha. Elyo banakile ukwangala, basile akela mumuchanga.

Ndege wa mwisho aliporudisha sindano aliyoazima, Kuku hakuwepo. Kwa hiyo watoto wake wakachukua sindano na wakaanza kuichezea. Walipochoka na mchezo wao, wakaiacha sindano kwenye mchanga.


Mukasuba, pungwa efyo abwelele. Epakwipusha pakela pakuti alundeko amasako nayambi nokubililila ayanenwike elyo aile pabulendo bwakwe. Nankoko epakwamba ukufwaya. Afwaya mu cikini. Afwaya mulubansa, aleka tekakumoneka.

Baadaye jioni Tai akarudi. Akaomba sindano ili aweze kushona baadhi ya manyoya yaliyokuwa yameanza kulegea alipokuwa safarini. Akaangalia kwenye kabati. Akaangalia jikoni. Akaangalia uani. Ila sindano haikupatikana.


” Mpelakofye ubushiku bumo,” Nankoko apapata. “kuti wiasa bikako amasako kumapindo yobe nokupupuka ukuya mukufwaya ifyakulya nakabili”. Pungwa epakuti “nakupelafye ubushiku bumo, ngatawasange akela, ukampeka ukampela umwana obe umo ngamalipilo”.

“Nipatie siku moja,” Kuku alimwomba Tai. “Halafu utaweza kushona bawa lako na kuruka tena kwenda kutafuta chakula.” “Siku moja tu,” alisema Tai. “Kama hutaipata sindano, itabidi unipe kimoja cha vifaranga vyako kama malipo.”


Ubushiku bwakonkelepo, elyo pungwa aishile, asangile nankoko alefwaya akela mumuchanga. Pungwa epakupupuka bwangu panshi nukwikatapo akameana kankoko. Nokuka senda. Ukufuma apopene lyonse pungwa naisa asanga nankoko alefwaya akela mumuchanga.

Tai aliporudi siku iliyofuata, alimkuta Kuku akichakura mchangani, ila hakukuwa na sindano. Kwa hiyo Tai alishuka kwa kasi na kukwapua kifaranga kimoja. Akaondoka nacho. Tangu hapo, kila Tai anapojitokeza humkuta Kuku akichakura kwenye mchanga akitafuta sindano.


Ngakwaisa icinshigwa cakwa pungwa, nankoko alacenjesha abana bakwe. “Fumeni palwalala”. Elyo tumwasuka ati, “tatuli fipuba, tulebutuka”.

Kila kivuli cha mabawa ya Tai kinapoonekana ardhini, Kuku huwatahadharisha vifaranga vyake. “Tokeni kwenye eneo la wazi.” Na wanajibu: “Sisi si wajinga. Tutakimbia.”


Written by: Ann Nduku
Illustrated by: Wiehan de Jager
Translated by: Sandra Mulesu
Language: IciBemba
Level: Level 3
Source: Hen and Eagle from African Storybook
Creative Commons License
This work is licensed under a Creative Commons Attribution 3.0 International License.
Options
Back to stories list Download PDF