Download PDF
Back to stories list

Nozibele na Umushishi utatu Nozibele na nywele tatu

Written by Tessa Welch

Illustrated by Wiehan de Jager

Translated by Sandra Mulesu

Language IciBemba

Level Level 3

Narrate full story The audio for this story is currently not available.


Munshita yakale, abakashana batatu baile mukuteba inkuni.

Hapo zamani za kale, wasichana watatu walienda kukusanya kuni.


Kwali ukwakaba sana, eyo baile mumumana mukowa. Bayangele nokowa mumenshi.

Ilikuwa ni siku yenye jua kali na wakaamua kwenda mtoni kuogelea. Wakaogelea huku wakicheza na kurushiana maji.


Elyo baimwene ati bwaila. Babutukile ukubwelela kumushi.

Ghafla waligundua kuwa muda umekwenda. Wakaharakisha kurudi nyumbani.


Cilya bapalamina kumushi, Nozibele aikete mumukoshi. Alilaba akakufwala mumukoshi, “Napapata nshindikeniko!” Nomba abanankwe bamukanina.

Walipokuwa wanakaribia kufika nyumbani, Nozibele akajishika shingoni. Alikuwa amesahau shanga zake! “Tafadhali turudini!” aliwasihi rafiki zake. Lakini rafiki zake wakasema tumechelewa.


Nozibele epakubwekelamo kumumana eka. Asendel akakufwala mumukoshi nokubweluluka bwangu bwangu ku mushi. Nomba aliluba munfifi.

Kwa hiyo Nozibele akarudi mwenyewe mtoni. Akapata shanga zake na akakimbia kurudi nyumbani. Lakini akapotea gizani.


Akatalamukila, amona ulubuto mukasaka. Eko aya bwangubwangu mukukonkosha pacibi.

Kwa mbali akaona mwanga unatoka kwenye nyumba. Akakimbilia kwenye nyumba na kugonga mlango.


Camupapwishe ukuti imbwa eyaiswile kucibi nokumwipusha, “Finshi ulefwaya?” Nozibele ati “Ninduba eico ndefwaya aponingasendama”, embwa aiti “Ingila pantu nalakusuma!” Nozibele epakwingila.

Akastaajabu kumwona mbwa akifungua mlango na akasema, “Unataka nini?” “Nimepotea na ninatafuta sehemu ya kulala,” akasema Nozibele. “Ingia ndani, la sivyo nitakung’ata!” mbwa akamwambia. Nozibele akaingia ndani.


Imbwa epakumweba ati, “njipikilako!” Nozibele ati “nomba nshatala ipikilapo imbwa.” Imbwa aiti “Ipika pantu nalakusuma”. Efyo Nozibele aipikile imbwa ifyakulya.

Mbwa akamwambia, “Nipikie!” “Sijawahi kumpikia mbwa,” akajibu. “Pika, la sivyo nitakung’ata!” mbwa akasema. Nozibele akampikia mbwa chakula.


Imbwa aiti, “Njanshikila ubusanshi!” Nozibele ati “nshatala anshikapo ubusanshi bwambwa.” Imbwa aiti, “njashikila ubusanshi pantu nalakusuma”! Efyo Nozibele ayanshike ubusanshi.

Mbwa akamwambia, “Nitandikie kitanda!” Nozibele akajibu, “Sijawahi kumtandikia mbwa kitanda.” “Tandika kitanda, la sivyo nitakung’ata!” mbwa akasema. Nozibele akatandika kitanda.


Cilabushiku aleipikila imbwa nokuicapila. Bushiku bumo imbwa aiti, “Nozibela, lelo nalaya mukutandalila abanandi. Upyange ing’anda, wipike ifyakulya, uwashe nokuwasha eponshila bwela.

Akawa kila siku anampikia, anamfulia na kumfagilia mbwa. Siku moja mbwa akasema, “Nozibele, leo naenda kuwatembelea rafiki zangu. Fagia nyumba, pika chakula na osha vitu vyangu kabla sijarudi.”


Cilyafye imbwa yaya, Nozibele asenda umushishi utatu mumutwe. Abika umushishi umo pabusnahi, umbi kunuma yacibi elyo umbi mwicinka. Efyo abutwike ukuya.

Mara baada tu ya mbwa kuondoka, Nozibele akanyofoa nywele tatu kutoka kwenye kichwa chake. Akaweka unywele mmoja chini ya kitanda, mmoja nyuma ya mlango, na mwingine akauweka kwenye uzio wa nyumba. Halafu, akakimbia kuelekea nyumbani kwa nguvu zote.


Elyi imbwa yabwelele, yaambile ukufwaya Nozibele. yapunda aiti “Nozibele ulikwisa?” Umushishi wali mwisamba lyabusanshi lyabalilapo aliti “ndimuno!” Iyakonkelepo aliti “Indikunuma yacibi”. ishiwi Ilyabutatu aliti, “ndimwicinka”.

Mbwa aliporudi akaanza kumtafuta Nozibele. “Nozibele, uko wapi?” akapiga kelele. “Niko hapa, chini ya kitanda,” unywele wa kwanza ukajibu. “Nipo hapa nyuma ya mlango,” unywele wa pili ukajibu. “Niko hapa kwenye uzio,” unywele wa tatu ukajibu.


Eyo imbwa yaimwene ukuti Nozibele naicenjesha. Epakubutuka ukukonamo ukuya kumushi. Nomba bandume yakwa Nozibele baleilolela nefimiti. Imbwa epakupilibuka nokubwekelamo ukufumapo tayatalile aimoneka nakabili.

Mbwa akagundua kuwa Nozibele amemkimbia. Kwa hiyo akakimbia kuelekea kijijini. Kaka zake Nozibele walikuwa wakimsubiri na fimbo. Mbwa alipowaona akageuka na kukimbia, na hajawahi kuonekana tena.


Written by: Tessa Welch
Illustrated by: Wiehan de Jager
Translated by: Sandra Mulesu
Language: IciBemba
Level: Level 3
Source: Nozibele and the three hairs from African Storybook
Creative Commons License
This work is licensed under a Creative Commons Attribution 3.0 International License.
Options
Back to stories list Download PDF