Download PDF
Back to stories list

Tom der Bananenverkäufer Tom muuza ndizi

Written by Humphreys Odunga

Illustrated by Zablon Alex Nguku

Translated by Anna Westpfahl

Read by Jula Eberth

Language German

Level Level 2

Narrate full story

Reading speed

Autoplay story


Tom trägt einen Korb mit reifen Bananen.

Tom anabeba tenga la ndizi zilizoiva.


Tom geht zum Markt, um Bananen zu verkaufen.

Tom anaenda sokoni kuuza ndizi.


Die Leute auf dem Markt kaufen Obst.

Sokoni watu wananunua matunda.


Aber niemand kauft Toms Bananen. Sie kaufen lieber Obst von Frauen.

Lakini hakuna anayenunua ndizi za Tom. Wanapenda kununua matunda kutoka kwa akina mama.


„In unserer Gemeinschaft verkaufen nur Frauen Obst“, sagen die Leute. „Was ist denn das für ein Mann?“, fragen die Leute.

“Kwenye jamii yetu, ni wanawake pekee ndio wanaouza matunda,” watu wanasema. “Ni mwanamume wa aina gani huyu?” watu wanahoji.


Aber Tom gibt nicht auf. Er ruft: „Kauft meine Bananen! Kauft meine süßen, reifen Bananen!“

Lakini Tom hakati tamaa. Anaita, “Nunua ndizi zangu! Nunueni ndizi zangu tamu zilizoiva!”


Eine Frau nimmt ein Bündel Bananen aus dem Korb. Sie schaut sich die Bananen genau an.

Mwanamke mmoja anachukua kichane cha ndizi kutoka kwenye tenga. Anaziangalia ndizi kwa umakini.


Die Frau kauft die Bananen.

Mwanamke ananunua ndizi.


Mehr Leute kommen an den Stand. Sie kaufen Toms Bananen und essen sie.

Watu wengine wanakuja kwenye kichanja. Wananunua ndizi za Tom na kuzila.


Bald ist der Korb leer. Tom zählt das Geld, das er verdient hat.

Mara, tenga linakuwa tupu. Tom anahesabu pesa alizopata.


Dann kauft Tom Seife, Zucker und Brot. Er legt die Sachen in seinen Korb.

Tom ananunua sabuni, sukari, na mkate. Anaweka vitu kwenye tenga lake.


Tom balanciert den Korb auf seinem Kopf und geht nach Hause.

Tom anajitwisha tenga kichwani na kwenda nyumbani.


Written by: Humphreys Odunga
Illustrated by: Zablon Alex Nguku
Translated by: Anna Westpfahl
Read by: Jula Eberth
Language: German
Level: Level 2
Source: Tom the banana seller from African Storybook
Creative Commons License
This work is licensed under a Creative Commons Attribution 4.0 International License.
Options
Back to stories list Download PDF