Download PDF
Back to stories list

ውሳኔ Uamuzi

Written by Ursula Nafula

Illustrated by Vusi Malindi

Translated by Mezemir Girma

Read by Abenezer Chane

Language Amharic

Level Level 2

Narrate full story

Reading speed

Autoplay story


መንደሬ ብዙ ችግር ነበረባት። ውሃ ከቦኖ ለመቅዳት ረጅም ሰልፍ እንሰለፍ ነበር።

Kijiji changu kilikuwa na matatizo mengi. Tulipanga foleni ndefu tukisubiri kuchota maji kutoka mfereji mmoja.


በሌሎች ሰዎች የሚሰጠንን ምግብ እንጠብቅ ነበር።

Tulisubiri kupokea msaada wa chakula.


ሌባ ፍራቻ ቤቶቻችንን በጊዜ እንዘጋ ነበር።

Tulifunga nyumba zetu mapema kwasababu ya wizi.


ብዙ ልጆች ትምህርታቸውን ያቋርጡ ነበር።

Watoto wengi waliacha shule.


ወጣት ሴቶች በሌሎች መንደሮች ውስጥ በሰራተኝነት ያገለግሉ ነበር።

Wasichana wadogo walifanya kazi za nyumbani kwenye vijiji vingine.


ግማሾቹ ወንዶች ልጆች በየሰፈሩ እየዞሩ ሲውሉ፤ ሌሎቹ ደግሞ በሰው ማሳ ላይ ያገለግሉ ነበር።

Wavulana wadogo waliranda randa kijijini na wengine walifanya kazi kwenye mashamba ya watu.


ነፋስ በነፈሰ ቁጥር ቆሻሻ ወረቀት በየአጥሩና በየዛፉ ላይ ይንጠለጠል ነበር።

Upepo ulipovuma, ulipeperusha karatasi chafu na kuzifikisha mitini na uani.


ሰዎችን በጥንቃቄ ጉድለት የተጣለ ብርጭቆ ይቆርጣቸው ነበር።

Watu walikatwa na vipande vya chupa vilivyotupwa ovyo ovyo.


አንድ ቀን ውሃው ቆመና የውሃ መያዣዎቻችን ባዶ ቀሩ።

Halafu siku moja, mfereji wa maji ulikauka na mitungi yetu ikawa mitupu.


አባቴ ሰዎች በመንደር ስብሰባ ላይ እንዲገኙ ለመቀስቀስ ከቤት ቤት ዞረ።

Baba yangu alitembea nyumba hadi nyumba akiwaomba watu kuhudhuria mkutano wa kijiji.


ሰዎች ከአንድ ትልቅ ዛፍ ስር ተቀምጠው ያዳምጡ ጀመር።

Watu walikusanyika chini ya mti mkubwa na kusikiliza.


አባቴ ተነስቶ ‹‹እነዚህን ችግሮቻችንን ለመፍታት በጋራ መስራት ይኖርብናል›› አለ።

Baba yangu alisimama na kusema, “Tunahitaji kusaidiana kutatua matatizo yetu.”


ግንድ ላይ የተቀመጠው የስምንት ዓመቱ ዓመቱ ጁማ ‹‹እኔ በማጽዳት እረዳለሁ›› ሲል ተናገረ።

Juma, mtoto wa miaka minane aliyekuwa amekaa kwenye tawi la mti, alisema kwa sauti, “Naweza kusaidia na usafi.”


አንዲት ሴትዮም ‹‹ሴቶቹ ከኔ ጋር እህል መዝራት ላይ መሰማራት ይችላሉ›› አሉ።

Mwanamke mmoja alisema, “Sisi wanawake tunaweza kuungana na kulima.”


ሌላ ሰውዬ ተነሳና ‹‹እኛ ወንዶቹ ጉድጓድ መቆፈር እንችላለን›› አለ።

Mwanamume mwingine alisimama na kusema, “Wanaume watachimba kisima cha maji.”


ሁላችንም በአንድ ድምጽ ‹‹ህይወታችንን መቀየር ይኖርብናል›› በማለት ጮህን። ከዚያች ቀን ጀምረን ችግሮቻችንን ለመፍታት አብረን እንሰራ ጀመር።

Sote tulisema kwa sauti moja, “Lazima tubadilishe maisha yetu.” Tangu siku hiyo, tulifanya kazi pamoja kutatua shida zetu.


Written by: Ursula Nafula
Illustrated by: Vusi Malindi
Translated by: Mezemir Girma
Read by: Abenezer Chane
Language: Amharic
Level: Level 2
Source: Decision from African Storybook
Creative Commons License
This work is licensed under a Creative Commons Attribution 4.0 International License.
Options
Back to stories list Download PDF