Download PDF
Back to stories list

ፍየል፣ ዉሻና ላም Mbuzi, Mbwa na Ng'ombe

Written by Fabian Wakholi

Illustrated by Marleen Visser, Ingrid Schechter

Translated by Mezemir Girma

Read by Abenezer Chane

Language Amharic

Level Level 2

Narrate full story

Reading speed

Autoplay story


ፍየል፣ ዉሻና ላም ጥሩ ጓደኛሞች ነበሩ። አንድ ቀን በታክሲ ጉዞ ለማድረግ ተነሱ።

Mbuzi, Mbwa na Ng’ombe walikuwa marafiki wa karibu sana. Siku moja walisafiri kwa teksi.


ከጉዟቸው መጨረሻ ሲደርሱም ታክሲ ነጂው መሳፈሪያቸውን እንዲከፍሉ ጠየቃቸው። ላም የራሷን ሒሳብ ከፈለች።

Walipofika mwisho wa safari yao, dereva aliwaomba walipe nauli zao. Ng’ombe alilipa nauli yake.


ዉሻ ትንሽ ተጨማሪ ከፈለች፤ ምክንያቱም ትክክለኛው ዓይነት ገንዘብ ስላልነበራት ነው።

Mbwa alilipa zaidi kidogo kwa sababu hakuwa na pesa taslimu.


ሹፌሩ ለዉሻው መልስ ሊሰጣት ሲል ፍየል ምንም ሳትከፍል ሮጠች።

Dereva alipokaribia kumpa Mbwa chenji yake, Mbuzi alitoroka bila kulipa chochote.


ሹፌሩ በጣም ስለተናደደ ለዉሻ ምንም መልስ ሳይሰጣት ሄደ።

Dereva alikasirika sana. Aliondoka bila kumrudishia Mbwa chenji yake.


ለዚያ ነው ዛሬ ድረስ ዉሻ መኪና በመጣ ቁጥር እየሮጠች መልሷን ያልሰጣትን ሹፌር ፍለጋ ወደ መኪናው ውስጥ ለማየት የምትሞክረው።

Hiyo ndiyo sababu hadi leo Mbwa hukimbiza magari ili achungulie ndani kuona kama atampata dereva mwenye chenji yake.


ፍየል የመኪና ድምጽ ስትሰማ ትሮጣለች። ምክንያቱም ሂሳብ ስላልከፈለች እንዳትታሰር ስለምትፈራ ነው።

Mbuzi hukimbia anaposikia mlio wa gari. Anaogopa atakamatwa kwa kutolipa nauli.


ላም ግን መኪና ሲመጣ ምንም አትጨናነቅም። መንገድም ስታቋርጥ ተረጋግታ ነው፤ ምክንያቱም ሂሳብ የለባትማ።

Na Ng’ombe hababaiki gari likiwa linakuja. Ng’ombe huvuka barabara bila wasiwasi kwa sababu anajua alilipa nauli yake yote.


Written by: Fabian Wakholi
Illustrated by: Marleen Visser, Ingrid Schechter
Translated by: Mezemir Girma
Read by: Abenezer Chane
Language: Amharic
Level: Level 2
Source: Goat, Dog and Cow from African Storybook
Creative Commons License
This work is licensed under a Creative Commons Attribution 3.0 International License.
Options
Back to stories list Download PDF