Download PDF
Back to stories list

Sakiima Sang Wimbo wa Sakima

Written by Ursula Nafula

Illustrated by Peris Wachuka

Translated by Georgette McGlashen

Language Jamaican Creole

Level Level 3

Narrate full story The audio for this story is currently not available.


Sakiima did liv wid im pierens dem an im fuor iez uol sista. Dem did liv pan wahn rich man lan. Dem tach ous did de a di en a wahn lain a chrii.

Sakima aliishi na wazazi wake na dada yake wa miaka minne. Waliishi katika shamba la mtu tajiri. Nyumba yao ya nyasi ilikuwa mwisho wa safu ya miti iliyopendeza.


Wen Sakiima a did chrii iez uol, im get sik an im get blain. Sakiima a did wahn talentid bwaai pikni.

Sakima alipokuwa na umri wa miaka mitatu, aliugua na kupoteza uwezo wa kuona. Hata hivyo, Sakima alikuwa mvulana mwenye kipaji.


Sakiima du uoliip a tingz we ada siks iez uol bwaai pikni kudn du. Far instans, im kuda siddong wid di uol piipl dem fram di vilij an taak bout impuotant mattaz.

Sakima alitenda mambo mengi ambayo wavulana wengine wa umri wake hawakufanya. Kwa mfano, aliketi na watu wazima na kujadili mambo muhimu.


Sakiima pierens dem did wok a di rich man yaad. Dem lef out orli inna di maanin an kom bak liet inna di iivlin. Sakiima stie wid im likl sista.

Wazazi wa Sakima walifanya kazi katika nyumba ya yule tajiri. Walitoka nyumbani asubuhi na mapema na kurudi jioni. Sakima aliachwa na dada yake.


Sakiima did lov fi sing sang. Wan die im mada aks im se, “A we yu lorn dem song de fram, Sakiima?”

Sakima alipenda kuimba nyimbo. Siku moja mama yake alimuuliza, “Sakima, unajifunza nyimbo hizi kutoka wapi?”


Sakiima ansa se, “Dem jos kom tu mi, mama. Mi ier dem inna mi ed an den mi sing dem.”

Sakima alimjibu, “Nazisikia akilini mwangu kisha naziimba.”


Sakiima laik wen im sing fi im likl sista, espeshali, ef shi did fiil onggri. Im sista uda lisn tu im a sing im fievarit sang. Shi wuda tek taim rak tu di myuuzik an it wuda mek shi kaam dong.

Sakima alipenda kumwimbia mdogo wake hasa akihisi njaa. Dada yake alimsikiliza na kucheza.


“Sing it agen an agen, Sakiima,” im sista wuda beg im se. Sakiima wuda du it an sing it uova an uova agen.

“Naomba uimbe tena na tena, Sakima,” mdogo wake alimsihi. Sakima alikubali na kuimba mara nyingine.


Wan iivlin wen im pierens dem kom bak uom, dem did kwaiyat-kwaiyat. Sakiima did nuo se sopm did rang.

Jioni moja, wazazi wake waliporudi nyumbani, walikuwa kimya sana. Sakima alijua kwamba lazima kulikuwa na jambo baya.


“A wa rang mama, papa?” Sakiima aks dem se. Sakiima fain out se di rich man son misn. Di man did fiil bad an laik im neva av nobadi.

“Kuna shida gani, mama, baba?” Sakima aliuliza. Sakima aligundua kwamba mwana wa tajiri wao alikuwa amepotea. Tajiri alihuzunika na kuwa na upweke mkubwa.


“Mi kyan sing fiim. Im mait fiil api agen,” Sakiima tel im pierens dem se. Bot im pierens dem neva pie im no main. “Im a wahn rich-rich man. Yu a jos wahn blain bwaai pikni. Yu tingk se yu sang kyan elp im?”

“Labda atafurahi tena nikimwimbia,” Sakima aliwaambia wazazi wake. Wazazi wake walidharau wazo lake. “Yeye ni tajiri sana. Wewe ni mvulana asiyeona. Unadhani wimbo wako utamsaidia?”


Bot Sakiima neva stap. Im likl sista bak im. Shi se, “Sakiima sang dem mek mi fiil beta wen mi onggri. Dem wi mek di rich man fiil beta tu.”

Hata hivyo, Sakima hakukata tamaa. Mdogo wake alimpa moyo. Alisema, “Nyimbo za Sakima hunituliza mimi nikiwa na njaa. Zitamtuliza tajiri vile vile.”


Di neks die, Sakiima aks im likl sista fi kyari im go a di rich man yaad.

Siku iliyofuata, Sakima alimwomba mdogo wake amwongoze hadi kwenye nyumba ya tajiri.


Im stan op anda wahn big winda an staat fi sing im fievarit sang. Likl bai likl yu kuda si di rich man ed staat shuo chuu di big winda.

Alisimama chini ya dirisha moja kubwa na kuanza kuimba wimbo wake alioupenda. Pole pole, kichwa cha tajiri kilionekana dirishani.


Di woka dem stap we dem a du. Dem lisn tu Sakiima nais sang. Bot wan man se, “Nobadi kudn komfat di baas. Da blain bwaai pikni ya tingk se im kyan komfat im?”

Wafanyakazi waliacha kazi zao. Wakasikiliza wimbo mzuri wa Sakima. Hata hivyo, mwanamume mmoja alisema, “Hakuna aliyefaulu kumtuliza bwana. Je, huyu mvulana asiyeona anafikiri atamtuliza?”


Sakiima di don sing im sang an ton roun fi lef. Bot di rich man ori op an se, “Du sing agen.”

Sakima alipomaliza kuimba wimbo wake alianza kuondoka. Tajiri alitoka nje kwa haraka na kusema, “Tafadhali, imba tena.”


Siem taim, tuu man kom a kyari sumadi pan wahn schrecha. Dem di fain di rich man son biit op an lef a ruod said.

Wakati huo huo, watu wawili walikuja wakiwa wamembeba mtu kwenye machela. Walimkuta mwana wa tajiri akiwa amechapwa na kuachwa kando ya barabara.


Di rich man did api so til fi siim son agen. Im gi Sakiima a prezent kaaz im did komfat im. Im kyari im son an Sakiima go a aaspital so Sakiima kuda get bak im sait.

Tajiri alifurahi sana kumwona mwana wake tena. Alimzawadia Sakima kwa kumliwaza. Aliwapeleka mwanawe na Sakima hosipitali ili Sakima aweze kusaidiwa kuona tena.


Written by: Ursula Nafula
Illustrated by: Peris Wachuka
Translated by: Georgette McGlashen
Language: Jamaican Creole
Level: Level 3
Source: Sakima's song from African Storybook
Creative Commons License
This work is licensed under a Creative Commons Attribution 4.0 International License.
Options
Back to stories list Download PDF