Download PDF
Back to stories list

Chikin an Milipiid Kuku na Jongoo

Written by Winny Asara

Illustrated by Magriet Brink

Translated by Georgette McGlashen

Language Jamaican Creole

Level Level 3

Narrate full story The audio for this story is currently not available.


Chikin an Milipiid a did fren. Bot dem alwiez inna kompitishan wid wananeda. Wan die dem mek op dem main fi plie futbaal fi si uu a di bes plieya.

Kuku na Jongoo walikuwa marafiki. Ila walikuwa wanashindana kila mara. Siku moja wakaamua kucheza mpira wa miguu ili waweze kubaini nani alikuwa mchezaji bora zaidi.


Dem go a di futbaal fiil an staat dem giem. Chikin did faas, bot Milipiid did faasa. Chikin kik faar, bot Milipiid kik faara. Chikin did staat get kraas.

Wakaenda uwanjani na wakaanza kucheza. Kuku alikuwa na kasi ila Jongoo alikuwa na kasi zaidi. Kuku alipiga mpira mbali, ila Jongoo alipiga mbali zaidi. Kuku akaanza kupandwa na hasira.


Dem mek op dem main fi av penalti shuut-out. Fos, Milipiid a did guol kiipa. Chikin skuor onggl wan guol. Den a did Chikin torn fi plie guoli.

Wakaamua kupigiana penati. Jongoo akaenda golini. Kuku alifunga goli moja pekee. Ikawa zamu ya kuku kwenda golini.


Milipiid kik di baal an skuor. Milipiid jribl di baal an skuor. Milipiid bok di baal an skuor faiv guol.

Jongoo alipiga mpira akafunga. Jongoo akapiga chenga akafunga. Jongoo akapiga kichwa akafunga. Jongoo akafunga magoli matano.


Chikin did wel beks se shi luuz. Shi neva tek luuzin gud. Milipiid did staat laaf kaaz im fren did a fos op arself.

Kuku akakasirika kwa kuwa amefungwa. Hakuwa mshindani mzuri. Jongoo akaanza kucheka kwa sababu rafiki yake alikuwa analalamika.


Chikin did so beks dat shi uopm ar biik waid an swola op Milipiid.

Kuku alipatwa na hasira kiasi kwamba akafungua mdomo wake mkubwa na akammeza Jongoo.


Jos az Chikin a waak go a ar yaad, shi bok op inna Mada Milipiid. Mada Milipiid aks ar se, “Yu si mi pikni?” Chikin neva se notn. Mada Milipiid did kansorn.

Kuku alipokuwa anarudi nyumbani alikutana na Mama yake Jongoo. Mama Jongoo akamuuliza, “Umemwona mwanangu?” Kuku hakujibu kitu. Mama Jongoo akapatwa na wasiwasi.


Den Mada Milipiid ier wahn likl vais. “Elp mi mama!” di vais did a baal. Mada Milipiid luk roun an lisn gud. Di vais did a kom fram outta di chikin.

Mama Jongoo akasikia sauti kwa mbali. “Nisaidie mama!” ile sauti ililia. Mama Jongoo akaangalia huku na kule na kusikiliza kwa makini. Sauti ilitokea tumboni mwa kuku.


Mada Milipiid baal out se, “Yuuz yu speshal powa mi pikni!” Milipiid kyan mek wahn bad smel an wahn bad ties inna yu mout. Chikin staat fi fiil sik.

Mama Jongoo alipiga kelele, “Tumia nguvu yako ya kipekee mwanangu!” Majongoo wanaweza kutoa harufu mbaya na ladha ya ajabu. Kuku akaanza kujisikia mgonjwa.


Chikin belch. Den shi swola an spit. Den shi sniiz an kaaf. An kaaf. Di milipiid di sik stomok!

Kuku akabeuwa. Akameza mate na kutema. Halafu akapiga chafya na kukohoa. Akakohoa tena. Jongoo alimfanya ajisikie vibaya.


Chikin kaaf so til shi kaaf op di milipiid we did inna ar beli. Mada Milipiid an ar pikni kraal go op inna wahn chrii go aid.

Kuku alikohoa, hadi akamtema jongoo aliyekuwa tumboni mwake. Mama Jongoo na mwanaye wakakwea mti kujificha.


Fram dat taim, chikin an milipiid ton enimi.

Tangu hapo, Kuku na Jongoo ni maadui.


Written by: Winny Asara
Illustrated by: Magriet Brink
Translated by: Georgette McGlashen
Language: Jamaican Creole
Level: Level 3
Source: Chicken and Millipede from African Storybook
Creative Commons License
This work is licensed under a Creative Commons Attribution 3.0 International License.
Options
Back to stories list Download PDF