Download PDF
Back to stories list

Dangki Pikni Mtoto Punda

Written by Lindiwe Matshikiza

Illustrated by Meghan Judge

Translated by Georgette McGlashen

Language Jamaican Creole

Level Level 3

Narrate full story The audio for this story is currently not available.


A did wahn likl gyal pikni uu fos si di schrienj shiep fram faar out.

Ilikuwa ni msichana mdogo aliyekuwa wa kwanza kuona umbo la ajabu kwa mbali.


Az di shiep kom nier, shi si se a did wahn prignant uman uu suuhn av biebi.

Kadiri umbo lilipokaribia, aliona kwamba lilikuwa ni mwanamke mwenye ujauzito mkubwa.


Fried bot briev, di likl gyal pikni go niera tu di uman. “Wi afi kip ar wid wi,” di likl gyal pikni piipl dem se. “We a go kip ar an di pikni sief.”

Kwa upole na ujasiri, msichana alimsogelea mwanamke yule. “Lazima tumhifadhi,” watu wa msichana yule walisema. “Tutawaweka yeye na mtoto wake salama.”


Di pikni did suuhn baan. “Push!” “Kyari som blangkit!” “Waata!” “Puuuuuuush!”

Mtoto alikuwa njiani kuzaliwa si muda mrefu. “Sukuma!” “Leteni mablanketi!” “Maji!” “Suuukuuumaaaa!!!”


Bot wen dem si di biebi, evribadi jomp bak an fraitn. “Wahn dangki?!”

Lakini walipomwona mtoto, wote waliruka kwa mshtuko. “Punda?!”


Evribadi staat kos. “Wi se wi wuda kip mada an pikni sief, an a dat wi a go du,” som a dem se. “Bot dem a go bring bad lok!” som se.

Wakaanza kubishana. “Tulisema tutawaweka mama na mtoto salama, na hivyo ndivyo tutakavyofanya,” baadhi wakasema. “Lakini watatuletea mkosi!” wengine wakadai.


An so di uman en op bai ar self agen. Shi did a wanda wa fi du wid dis foni pikni. Shi did a wanda wa fi du wid ar self.

Kwa hiyo mwanamke yule alijikuta yuko peke yake kwa mara nyingine tena. Akajiuliza atafanya nini na mtoto huyo wa ajabu. Akajiuliza atafanya nini na yeye mwenyewe.


Bot in a di en shi afi aksep se im a fi ar pikni an shi a im mada.

Lakini hatimaye alikubali kwamba huyo ni mwanaye na yeye ni mama yake.


Nou, ef di pikni did stie a di siem likl saiz, evriting wuda difrant. Bot di dangki pikni gruo an gruo so til im kudn fit pan im mada bak no muor. An no mata ou aad im chrai, im kudn biyiev laik a yuuman biin. Im mada di taiyad aal di taim an no nuo we fi du. Somtaim shi mek im du animal wok.

Endapo mtoto huyo angebaki kuwa vilevile, na umbo dogo, labda kila kitu kingekuwa tofauti. Lakini mtoto Punda aliendelea kukua na kukua mpaka hakuweza kutoshea tena mgongoni mwa mama yake. Pamoja na kujaribu kwa bidii, hakuweza kuwa na tabia za kibinadamu. Mara nyingi mama yake alichoka na kuvunjika moyo. Wakati mwingine alimlazimisha kufanya kazi walizostahili wanyama.


Ignarans an beksieshan bil op ina di Dangki. Im kudn du dis an im kudn du dat. Im kudn bi laik dis an im kudn bi laik dat. Im get so opset das, wan die, im kik dong im uona mada pan di grong.

Kuchanganyikiwa na hasira vilianza kujengeka ndani mwa Punda. Alishindwa kufanya hivi wala vile. Alishindwa kuwa hivi wala vile. Alipatwa na hasira sana kiasi kwamba, siku moja, alimpiga teke mama yake mpaka akaanguka chini.


Dangki did shiem-shiem. Im ronwe az faar an a faas az im kud.

Punda alijawa na aibu. Akaanza kukimbilia mbali kwa haraka kadiri awezavyo.


Bai taim im stap ron, a did nait, an Dangki did laas. “Iihn aahn?” im bieli se ina di daak. “Iihn aahn?” it eko bak. Im did bai imself. Im korl op ina wahn tait baal, an jrap ina a diip an taamentin sliip.

Wakati aliposimama, ilikuwa ni usiku, na alikuwa amepotea. “Hii hoo?” alinong’ona gizani. “Hii hoo?” giza likatoa mwangwi. Alikuwa mwenyewe. Alijikunyata katika umbo dogo, akalala fofofo usingizi wa mang’amung’amu.


Dangki wiek op an si wahn schrienj uol man a luk pan im. Im luk ina di uol man yai dem an staat fiil a likl beta.

Punda aliamka na kumkuta mzee mmoja wa ajabu akimtazama. Akamwangalia mzee yule machoni na akaanza kuhisi ishara ya matumaini.


Dangki go an go stie wid di uol man, uu tiich im nof difrant wie fi liv. Dangki lisn an lorn, an di uol man lisn an lorn tu. Dem elp wan aneda, an dem laaf tugeda.

Punda alienda kuishi na mzee yule, na mzee alimfundisha mbinu nyingi za kuishi. Punda alisikiliza na kujifunza, na mzee vivyo hivyo pia. Walisaidiana na kucheka pamoja.


Wan maanin, di uol man aks Dangki fi kyari im go op wahn moutn tap.

Asubuhi moja, mzee alimwomba Punda ambebe hadi kwenye kilele cha mlima.


Wie op ina di kloud dem, dem jrap asliip. Dangki jriim se im mada did sik an a kaal im. An wen im wiek op…

Walipofika juu kwenye mawingu, walipatwa na usingizi. Punda akaota kuwa mama yake alikuwa mgonjwa na alimhitaji. Na alipoamka…


… di kloud dem an im fren di uol man, gaan.

…mawingu yalikuwa yametoweka pamoja na rafiki yake, yule mzee.


Dangki nou nuo we fi du.

Hatimaye, Punda alijua alichotakiwa kufanya.


Dangki fain im mada bai ar self a baal fi ar pikni. Dem luk pan wan aneda fi a lang taim. An den dem og op wan aneda tait-tait.

Punda alimkuta mama yake akiwa peke yake huku akimwomboleza mwanaye aliyepotea. Wakaangaliana kwa muda mrefu. Na kisha wakakumbatiana kwa hisia.


Di dangki pikni an im mada gruo tugeda an fain uol iip a wie fi liv wid wan aneda. Afta a wail, ada fambili staat fi liv roun dem.

Mtoto Punda na mama yake wamekuwa kitu kimoja na kuishi kwa ushirikiano. Taratibu, familia nyingine zimeanza kuhamia na kuishi miongoni mwao.


Written by: Lindiwe Matshikiza
Illustrated by: Meghan Judge
Translated by: Georgette McGlashen
Language: Jamaican Creole
Level: Level 3
Source: Donkey Child from African Storybook
Creative Commons License
This work is licensed under a Creative Commons Attribution 4.0 International License.
Options
Back to stories list Download PDF