Download PDF
Back to stories list

Tom muuza ndizi Tom muuza ndizi

Written by Humphreys Odunga

Illustrated by Zablon Alex Nguku

Translated by Matteo E. Mwita

Read by Lauwo George

Language Kiswahili

Level Level 2

Narrate full story

Reading speed

Autoplay story


Tom anabeba tenga la ndizi zilizoiva.

Tom anabeba tenga la ndizi zilizoiva.


Tom anaenda sokoni kuuza ndizi.

Tom anaenda sokoni kuuza ndizi.


Sokoni watu wananunua matunda.

Sokoni watu wananunua matunda.


Lakini hakuna anayenunua ndizi za Tom. Wanapenda kununua matunda kutoka kwa akina mama.

Lakini hakuna anayenunua ndizi za Tom. Wanapenda kununua matunda kutoka kwa akina mama.


“Kwenye jamii yetu, ni wanawake pekee ndio wanaouza matunda,” watu wanasema. “Ni mwanamume wa aina gani huyu?” watu wanahoji.

“Kwenye jamii yetu, ni wanawake pekee ndio wanaouza matunda,” watu wanasema. “Ni mwanamume wa aina gani huyu?” watu wanahoji.


Lakini Tom hakati tamaa. Anaita, “Nunua ndizi zangu! Nunueni ndizi zangu tamu zilizoiva!”

Lakini Tom hakati tamaa. Anaita, “Nunua ndizi zangu! Nunueni ndizi zangu tamu zilizoiva!”


Mwanamke mmoja anachukua kichane cha ndizi kutoka kwenye tenga. Anaziangalia ndizi kwa umakini.

Mwanamke mmoja anachukua kichane cha ndizi kutoka kwenye tenga. Anaziangalia ndizi kwa umakini.


Mwanamke ananunua ndizi.

Mwanamke ananunua ndizi.


Watu wengine wanakuja kwenye kichanja. Wananunua ndizi za Tom na kuzila.

Watu wengine wanakuja kwenye kichanja. Wananunua ndizi za Tom na kuzila.


Mara, tenga linakuwa tupu. Tom anahesabu pesa alizopata.

Mara, tenga linakuwa tupu. Tom anahesabu pesa alizopata.


Tom ananunua sabuni, sukari, na mkate. Anaweka vitu kwenye tenga lake.

Tom ananunua sabuni, sukari, na mkate. Anaweka vitu kwenye tenga lake.


Tom anajitwisha tenga kichwani na kwenda nyumbani.

Tom anajitwisha tenga kichwani na kwenda nyumbani.


Written by: Humphreys Odunga
Illustrated by: Zablon Alex Nguku
Translated by: Matteo E. Mwita
Read by: Lauwo George
Language: Kiswahili
Level: Level 2
Source: Tom the banana seller from African Storybook
Creative Commons License
This work is licensed under a Creative Commons Attribution 4.0 International License.
Options
Back to stories list Download PDF