Download PDF
Back to stories list

Kwa nini Viboko Hawana Nywele Kwa nini Viboko Hawana Nywele

Written by Basilio Gimo, David Ker

Illustrated by Carol Liddiment

Translated by Matteo E. Mwita

Read by Lauwo George

Language Kiswahili

Level Level 2

Narrate full story

Reading speed

Autoplay story


Siku moja, Sungura alikuwa akitembea pembeni ya mto.

Siku moja, Sungura alikuwa akitembea pembeni ya mto.


Kiboko alikuwepo pia, akitembea huku akila majani mazuri ya kijani.

Kiboko alikuwepo pia, akitembea huku akila majani mazuri ya kijani.


Kiboko hakumwona Sungura na kwa bahati mbaya akaukanyaga mguu wa Sungura. Sungura akaanza kumpigia Kiboko kelele. “We Kiboko huoni kama umeukanyaga mguu wangu?”

Kiboko hakumwona Sungura na kwa bahati mbaya akaukanyaga mguu wa Sungura. Sungura akaanza kumpigia Kiboko kelele. “We Kiboko huoni kama umeukanyaga mguu wangu?”


Kiboko akamwomba Sungura msamaha, “Samahani, sikukuona, tafadhali nisamehe!” Lakini Sungura hakukubali na akaendelea kumbwatukia Kiboko, “Umefanya makusudi! Kuna siku utakiona, na nitakulipizia!”

Kiboko akamwomba Sungura msamaha, “Samahani, sikukuona, tafadhali nisamehe!” Lakini Sungura hakukubali na akaendelea kumbwatukia Kiboko, “Umefanya makusudi! Kuna siku utakiona, na nitakulipizia!”


Sungura alienda kumtafuta moto na akamwambia, “Nenda, ukamchome Kiboko akitoka majini kuja kula majani. Alinikanyaga!” Moto ukajibu, “Hakuna tatizo, rafiki yangu Sungura, nitafanya ulichoniomba kufanya.”

Sungura alienda kumtafuta moto na akamwambia, “Nenda, ukamchome Kiboko akitoka majini kuja kula majani. Alinikanyaga!” Moto ukajibu, “Hakuna tatizo, rafiki yangu Sungura, nitafanya ulichoniomba kufanya.”


Baadaye, Kiboko alikuwa akila majani mbali na mto, aliposhtuka moto umelipuka. Miale ya moto ikaanza kuzichoma nywele za Kiboko.

Baadaye, Kiboko alikuwa akila majani mbali na mto, aliposhtuka moto umelipuka. Miale ya moto ikaanza kuzichoma nywele za Kiboko.


Kiboko akaanza kulia na kukimbilia kwenye maji. Nywele zake zote zilikuwa zimeungua na moto. Kiboko aliendelea kulia, “Nywele zangu zimeungua na moto! Nywele zangu zote zimeisha! Nywele zangu nzuri!”

Kiboko akaanza kulia na kukimbilia kwenye maji. Nywele zake zote zilikuwa zimeungua na moto. Kiboko aliendelea kulia, “Nywele zangu zimeungua na moto! Nywele zangu zote zimeisha! Nywele zangu nzuri!”


Sungura alikuwa na furaha kwa kuwa nywele za Kiboko ziliungua. Hadi leo kwa kuogopa moto, Kiboko hawezi kwenda mbali na maji.

Sungura alikuwa na furaha kwa kuwa nywele za Kiboko ziliungua. Hadi leo kwa kuogopa moto, Kiboko hawezi kwenda mbali na maji.


Written by: Basilio Gimo, David Ker
Illustrated by: Carol Liddiment
Translated by: Matteo E. Mwita
Read by: Lauwo George
Language: Kiswahili
Level: Level 2
Source: Why hippos have no hair from African Storybook
Creative Commons License
This work is licensed under a Creative Commons Attribution 3.0 International License.
Options
Back to stories list Download PDF