Tom muzii safaa gutuu baate deema.
Tom anabeba tenga la ndizi zilizoiva.
Tom muzii gurguruuf gara magaala deema.
Tom anaenda sokoni kuuza ndizi.
Namonni gabyaa kessa jiran fuduraa bitan.
Sokoni watu wananunua matunda.
Garuu namani tokkoyu muzii Tom hinbinne. Dubarti irraa bitu barbadan.
Lakini hakuna anayenunua ndizi za Tom. Wanapenda kununua matunda kutoka kwa akina mama.
Namonni akkan jedhu, “Ganda kenyyati dubartoota qofatu fudura gurgura.” “Kuni nama akkamiti,” jedhan gafatu.
“Kwenye jamii yetu, ni wanawake pekee ndio wanaouza matunda,” watu wanasema. “Ni mwanamume wa aina gani huyu?” watu wanahoji.
Hata’u malee Tom abdi hinkunne. Akkan jedhe, “Muzii kiyyaa bitaa! Muziin kiyyaa bayee mi’awadha!”
Lakini Tom hakati tamaa. Anaita, “Nunua ndizi zangu! Nunueni ndizi zangu tamu zilizoiva!”
Dubarti tokko dhufte muzii abazza tokko olkafte sirriti xinxaltee.
Mwanamke mmoja anachukua kichane cha ndizi kutoka kwenye tenga. Anaziangalia ndizi kwa umakini.
Dubartitin muzii sana bitee.
Mwanamke ananunua ndizi.
Namonni bayee ishee argani dhufan. Muzii Tom bitani nyaatan.
Watu wengine wanakuja kwenye kichanja. Wananunua ndizi za Tom na kuzila.
Yeroodhuma sana safaan isaa duwaa ta’e. Tomis qarshi argate lakka’u calqabe.
Mara, tenga linakuwa tupu. Tom anahesabu pesa alizopata.
Sana booda, Tom samuuna, sukkara fi dabboo bitate. Waantota kana safaa isaa kessa kayyate.
Tom ananunua sabuni, sukari, na mkate. Anaweka vitu kwenye tenga lake.
Tom safaa mataa isaa gubbati baate gara mana deeme.
Tom anajitwisha tenga kichwani na kwenda nyumbani.