Download PDF
Back to stories list

Granmaa banaana dem Ndizi za bibi

Written by Ursula Nafula

Illustrated by Catherine Groenewald

Translated by Georgette McGlashen

Language Jamaican Creole

Level Level 4

Narrate full story The audio for this story is currently not available.


Granmaa gyaadn did nais-nais, fol a sogm, milet, an kasaava. Bot di bes a did di banaana dem. Alduo Granmaa did av nof granpikni, mi di nuo anda di kwaiyat se mi a did ar fievarit. Shi mek mi kom a ar yaad aal di taim. Shi tel mi likl siikrit tingz. Bot shi did av wan siikrit we shi no tel mi: which paat shi mek ar banaana dem raip.

Bibi alikuwa na bustani nzuri iliyojaa mtama, ulezi na mihogo. Lakini kati ya mazao yote, alipenda zaidi ndizi. Japo bibi alikuwa na wajukuu wengi, nilikuja kubaini kuwa alikuwa ananipenda mimi zaidi ya wote. Mara nyingi alikuwa akinialika nyumbani kwake. Pia alikuwa ananiambia siri ndogo ndogo. Lakini kulikuwa na siri moja ambayo hakunishirikisha: alipokuwa anavundika ndizi.


Wan die mi si wahn big schraa baaskit inna di son outsaid a Granmaa ous. Wen mi aks ar se a we it fa, di onggl ansa mi get a did, “a mi majik baaskit.” Said a di baaskit, a di nof banaana liif we Granmaa ton uova evritaim. Mi did wel waahn nuo a wa. “We di liif dem fa, Granmaa?” mi aks ar se. Di onggl ansa mi get a did, “Dem a mi majik liif dem.”

Siku moja niliona tenga kubwa limeanikwa juani nje ya nyumba ya bibi. Nilipouliza lilikuwa la nini, jibu pekee nililopata lilikuwa, “Hilo ni tenga langu la maajabu.” Pembeni mwa tenga lile kulikuwa na majani ya ndizi ambayo bibi alikuwa akiyageuza kila mara. Nilipatwa na shauku. “Bibi, hayo majani ni ya nini?” niliuliza. Jibu pekee nililopata lilikuwa, “Ni majani yangu ya maajabu.”


It did intrestin fi wach Granmaa, di banaana dem, di banaana liif dem an di big schraa baaskit. Bot Granmaa sen mi go tu mi mada fi go du sopm. “Granmaa, du, mek mi wach we yu a go mek…” “No bi aadiez pikni, du we mi tel yu fi du,” shi se siiros. Mi ron go.

Nilikuwa na shauku kubwa kumwangalia bibi, ndizi, majani ya ndizi na tenga kubwa. Lakini bibi alinituma kwenda kwa mama. “Bibi, tafadhali naomba nitazame unavyoandaa…” “Usiwe msumbufu, fanya ulichoambiwa,” alisisitiza. Nikaondoka nikikimbia.


Wen mi kom bak, Granmaa did a siddong outsaid bot sho neva av no baaskit ar no banaana. “Granmaa, which paat di baaskit de, we aal a di banaana dem de, an we…” Bot di onggl ansa mi get a did, “Dem de inna mi majik plies.” Mi did disapaintid!

Niliporudi, bibi alikuwa amekaa nje, ila hakukuwa na tenga wala ndizi. “Bibi, tenga liko wapi, zile ndizi ziko wapi, na…” Jibu pekee nililopata lilikuwa, “Zipo kwenye eneo la maajabu.” Ilikuwa inasikitisha.


Tuu die afta dat, Granmaa sen mi inna ar bedruum fi ar waakin stik. Az suuhn az mi uopm di duor, wahn schrang raip banaana smel lik mi. Pan di insaid a di ruum a di Granmaa majik schraa baaskit. It did wel aid wid wahn uol blangkit. Mi lif it op an tek iihn di nais-nais smel.

Siku mbili baadaye, bibi alinituma kwenda chumbani kwake kumletea mkongojo. Mara tu baada ya kufungua mlango, nilikaribishwa na harufu kali ya ndizi mbivu. Pembeni mwa chumba kulikuwa na tenga kubwa la maajabu la bibi. Lilikuwa limefichwa na blanketi la zamani. Nikaliinua na kunusa ile harufi nzuri.


Granmaa vais fraitn mi wen shi kaal mi, “We yu a du? Ori op an bring mi stik kom.” Mi ori op an kom out wid ar waakin stik. “We yu a smail bout?” Granmaa aks se. A wen shi aks mi riyalaiz se mi stil did a smail bout ou mi fain out ar majik plies.

Sauti ya bibi ilinishtua alipoita, “Unafanya nini? Fanya haraka niletee mkongojo.” Nikaharakisha kwenda nje na mkongojo wake. “Unatabasamu nini?” bibi aliuliza. Swali lake likanifanya nigundue kuwa kumbe bado nilikuwa ninatabasamu baada ya kugundua eneo lake la maajabu.


Di neks die wen Granmaa kom vizit mi mada, mi buolt go a ar yaad fi chek di banaana agen. Wahn wel raip bonch did de de. Afta mi kova di baaskit agen, mi go biyain a di ous an it wan kwik-kwik. A did di swiitis banaana mi eva ties.

Siku iliyofuata bibi alipokuja kumtembelea mama yangu, nikakimbilia nyumbani kwake kuangalia ndizi tena. Kulikuwa na vichane vya ndizi zilizoiva. Nikachukua ndizi moja na kuificha kwenye nguo yangu. Baada ya kufunika tenga tena, nikaenda nyuma ya nyumba na harakaharaka nikaila. Ilikuwa ni ndizi tamu ambayo sijawahi kula kamwe.


Di neks die, wen Granmaa did inna di gyaadn a pik vejitebl, mi sniik go iihn an luk pan di banaana dem. Nieli aal a dem raip. Mi kudn elp bot fi tek a bonch a fuor a dem. Az mi a tiptuo go a di duor, mi ier Granmaa a kaaf outsaid. Mi bieli manij fi aid di banaana dem anda mi frak an waak paas ar.

Siku iliyofuata, bibi alipokuwa bustanini akichuma mboga, nikanyemelea ndani kuchungulia ndizi. Karibu zote zilikuwa zimeiva. Nikashindwa kujizuia nikachukua kichane cha ndizi nne. Nilipokuwa nanyata kuelekea mlangoni, nikamsikia bibi akikohoa nje. Nilifanikiwa kuzificha ndizi ndani ya nguo yangu na tukapishana bila ya kugundua.


Di neks die a did maakit die. Granmaa wiek op orli. Shi alwiez kyari raip banaana an kasaava go sel a di maakit. Mi neva ori op fi go luk fi ar da die de. Bot mi kudn avaid ar fi lang.

Siku iliyofuata ilikuwa siku ya gulio. Bibi aliamka asubuhi sana. Huwa anapeleka ndizi mbivu na mihogo kuuza gulioni. Siku hiyo sikuwa na haraka kwenda kumsalimia. Ila sikuweza kumkwepa kwa muda mrefu.


Lieta inna di iivnin mi mada an faada kaal mi, an Granmaa. Mi did nuo a fi wa. Da nait de az mi lie dong fi sliip, mi nuo se mi kudn tiif agen, no fram granmaa, no fram mi pierens an fi shuor no fram nobadi els.

Jioni ile niliitwa na mama, baba na bibi. Nilijua kwanini. Usiku ule nilipokwenda kulala, nilijua siwezi kuiba tena. Siwezi kumwibia bibi, wazazi wangu na mtu yeyote yule.


Written by: Ursula Nafula
Illustrated by: Catherine Groenewald
Translated by: Georgette McGlashen
Language: Jamaican Creole
Level: Level 4
Source: Grandma's bananas from African Storybook
Creative Commons License
This work is licensed under a Creative Commons Attribution 3.0 International License.
Options
Back to stories list Download PDF