Download PDF
Back to stories list

Di Onigaid Rivenj Kisasi cha Kiongozi

Written by Zulu folktale

Illustrated by Wiehan de Jager

Translated by Georgette McGlashen

Language Jamaican Creole

Level Level 4

Narrate full story The audio for this story is currently not available.


Dis a di stuori bout Hngede di Onigaid bod, an wahn krievn yong man niem Gingiile. Wan die wail Gingiile did de out a ont im ier Hngede a mek naiz. Gingiile mout staat waata az im a tingk bout oni. Im stap an lisn gud, an a sorch so til im did si di bod pan di chrii lim uova im ed. “Chitik-chitik-chitik,” di likl bod a shiek op imself, wail im a flai go uova di neks chrii, an di neks wan. “Chitik-chitik-chitik,” im did a kaal an a stap nou an den fi mek shuor se dat Gingiile did a fala im.

Hii ni hadithi ya Ngede, ambaye ni ndege mpenda asali, na mvulana mmoja mlafi anayeitwa Gingile. Siku moja Gingile alipokuwa akiwinda alisikia mwito wa Ngede. Kinywa chake kilianza kutokwa mate kwa kufikiria asali. Alisimama, akasikiliza na kuangalia vizuri hadi alipomwona yule ndege akiwa ametua kwenye matawi yaliyokuwa juu ya kichwa chake. “Chitik-chitik-chitik,” yule ndege mdogo alitatarika aliporuka na kutua kwenye mti mmoja hadi mwingine, na mwingine tena. “Chitik-chitik-chitik,” aliita, huku akinyamaza na kuhakikisha kwamba Gingile alikuwa amemfuata.


Afta aafan-owa, dem did riich wahn big wail fig chrii. Hngede a jomp op an dong laik im mad aal bout di chrii lim dem. Den im stap pan wahn lim an kak im ed tuwaadz Gingiile laik im a se, “Siit ya! Kom nou! Wa a tek yu so lang?” Gingiile kudn si no biiz fram anda di chrii, bot im did chos Hngede.

Baada ya nusu saa, walifika kwenye mti wa matini. Ngede aliruka kama mwenda wazimu kutoka tawi moja hadi jingine. Kisha alitulia kwenye tawi moja na kupindua kichwa chake akimwangalia Gingile kana kwamba anasema, “Ipo hapa! Njoo sasa! Kwa nini unachukua muda mrefu?” Gingile hakuweza kuona nyuki wowote kutoka chini ya mti, lakini alimwamini Ngede.


So Gingiile pudong im ontin spier anda di chrii, gyada som jrai stik an kech op wahn sumaal faiya. Wen di faiya staat bon gud, im put wahn lang jrai stik inna di migl a di faiya. Di ud di nuon espeshali fi mek op uol iip a sumuok wen it a bon. Im staat klaim, a uol aan pan di kuul en a di stik we a sumuok wid im tiit.

Kwa hivyo Gingile aliweka mkuki wake alioutumia kuwinda chini ya mti, akakusanya vijiti vilivyokauka na kuwasha moto mdogo. Moto ulipokuwa ukiwaka vizuri, alichomeka kijiti kirefu kwenye moto. Mti huu ulijulikana kwa kutoa moshi mwingi ulipokuwa unaungua. Alianza kukwea mti huku akishika kijiti kwa meno upande usiofuka moshi.


Likl afta dat im kuda ier di bizi biiz dem a boz loud. Dem did a go in an out a wahn uol inna di chrii chonk – dem aiv. Wen Gingiile riich di aiv im push di en a di stik wid di sumuok pan it inna di uol. Di biiz dem rosh kom out, mad an beks. Dem flai we bikaaz dem neva laik di sumuok – bot nat bifuor dem gi Gingiile som at sting!

Muda mfupi baadaye, aliweza kusikia sauti ya nyuki wenye harakati nyingi ikivuma. Walikuwa wakiingia na kutoka kwenye upenyo wa mti, yaani mzinga wao. Gingile alipoufikia mzinga, alisukuma ile kuni ya moto ndani ya ule upenyo. Nyuki waliharakisha kutoka ndani wakiwa na hasira na uchungu. Waliruka na kwenda mbali kwa sababu hawakupenda moshi – lakini walifanya hivyo baada ya kumuuma Gingile kwa uchungu!


Wen di biiz dem kom out, Gingiile push im an dem inna di nes. Im tek out som anfol a wieti onikuom, a jrip wid rich oni an fol a fat, wait bruud. Im put di kuom gud-gud inna di pouch we im did a kyari pan im shoulda, an staat klaim dong di chrii.

Nyuki walipokuwa nje, Gingile aliingiza mikono yake ndani ya kiota. Alitoa kipande kikubwa cha sega kilichokuwa kinadondoka urojo mzito wa asali, na kilichojaa wadudu weupe wanene. Aliiweka taratibu ndani ya mkoba aliokuwa nao na kuanza kushuka kutoka mtini.


Hngede did ankshos a wach evriting we Gingiile did a du. Im did a wiet fi im lef a fat piis a onikuom az a tangk yuu prezent fi di Onigaid. Hngede jomp fram lim tu lim, niera an niera tu di grong. Fainali Gingiile riich di batam a di chrii. Hngede siddong pan wahn rak stuon nier di bwaai pikni an a wiet fi im riwaad.

Ngede alishuhudia kila kitu Gingile alichofanya. Alikuwa anamsubiri abakishe kiasi kidogo cha asali kama shukurani kwa Kiongozi. Ngede aliruka kutoka tawi hadi tawi huku akikaribia chini. Mwishowe Gingile alifika chini ya mti. Ngede alitua kwenye mwamba karibu na mvulana huyo na kusubiri zawadi yake.


Bot, Gingiile out di faiya, pik op im spier an staat waak go a im yaad, an naa pie di bod no main. Hngede baal out mad-mad, “Viktaa! Viktaa!” Gingiile stap, an luk pan di likl bod an bos out a loud laaf. “Yu waahn som oni, iihn, mi fren? Ha! Bot a mi du aal a di wok, an get aal a di sting dem. Wa mek mi shuda shier non a dis nais oni wid yu?” Den im waak aaf. Hngede did wel beks! Dis a no no wie fi chriit im! Bot im wuda av im rivenj.

Lakini Gingile alizima moto, akachukua mkuki wake na kuanza safari kwenda nyumbani bila kumjali ndege yule. Ngede aliita kwa hasira, “USH-ndi! USH-ndi!” Gingile alisimama, akamkodolea macho yule ndege kisha akacheka kwa sauti. “Unataka asali kidogo, rafiki yangu? Ha! Lakini ni mimi niliyefanya kazi yote pamoja na kuumwa na nyuki. Kwa nini nikugawie hii asali tamu?” Baada ya kusema hivyo, aliondoka na kwenda zake. Ngede alikasirika sana! Hivi sivyo alivyostahili kutendewa! Ila atalipiza kisasi.


Wan die bout kopl wiik afta Gingiile ier di oni kaal fram Hngede. Im memba di nais tiesin oni, an ori op an fala di bod agen. Afta im liid Gingiile schriet pan di ej a di faris, Hngede stap an res anda wahn big ambrela maka chrii. “Aaa,” Gingiile tingk tu imself. “Di aiv mos de inna di chrii.” Im ori op an kech wahn sumaal faiya an staat klaim, wid di lim we a sumuok inna im tiit. Hngede siddong an did a wach.

Siku moja baada ya majuma machache, Gingile tena alisikia mwito wa asali kutoka kwa Ngede. Aliikumbuka asali tamu, na kwa hamu alimfuata ndege yule kwa mara nyingine. Baada ya kumwongoza Gingile pembeni mwa msitu, Ngede alisimama na kupumzika chini ya mti wa mwavuli. “Ahh,” Gingile aliwaza. “Lazima mzinga umo ndani ya mti huu.” Kwa haraka aliwasha moto wake na kuanza kukwea mti huku akibeba kuni iliyotoa moshi katika meno yake. Ngede alikaa na kuangalia tu.


Gingiile did a klaim, an a wanda wai im no ier di yuuzhal boz. “Miebi di aiv did de diip inna di chrii,” im tingk tu imself. Im jrag imself op pan aneda lim. Bot insted a di aiv, im did a luk schriet inna wahn lepad fies! Lepad did wel beks kaaz ar sliip get badli distorb. Shi skwiiz ar yai dem tugeda, uopm ar mout an shuo ar big-big an wel shaap tiit dem.

Gingile alipopanda, alishangaa kwa nini hakusikia sauti ya nyuki. “Pengine mzinga umo ndani zaidi katika mti,” alifikiria. Alipanda tena juu ya tawi jingine. Lakini badala ya mzinga, alijikuta uso kwa uso na chui! Chui alikuwa na hasira sana kwa sababu usingizi wake ulikuwa umekatizwa. Aliyafanya macho yake kuwa madogo, akaufungua mdomo wake na kuonyesha meno yake makubwa na makali.


Bifuor Lepad kuda lik aafa Gingiile, im ori op dong di chrii. Inna im ori im mis a lim, an jrap wid a loud naiz pan di grong an twis im angkl. Im limp aaf az faas az im kud. Loki fiim, Lepad did tuu sliipi fi ron im dong. Hngede, di Onigaid get im rivenj. An Gingiile did lorn im lesn.

Kabla ya Chui kumvamia Gingile, alishuka chini haraka. Katika haraka hiyo, aliteleza na kuanguka kwa kishindo huku akiumia mguu wake. Alirukaruka akienda kwa haraka alivyoweza. Kwa bahati nzuri, Chui alikuwa bado amelala kwa hivyo hakumfukuza. Ngede, Kiongozi alikuwa amelipiza kisasi chake na Gingile alikuwa amejifunza funzo lake.


So, wen Gingiile pikni dem ier di stuori bout Hngede dem av rispek fi di likl bod. Enitaim dem riip oni, dem mek shuor se dem lef di bigis paat a di onikuom fi di Onigaid!

Kwa hivyo wakati watoto wa Gingile wanaposikia hadithi ya Ngede, wanamheshimu yule ndege. Kila wanapotoa asali, huhakikisha kwamba wanamwachia Kiongozi fungu kubwa!


Written by: Zulu folktale
Illustrated by: Wiehan de Jager
Translated by: Georgette McGlashen
Language: Jamaican Creole
Level: Level 4
Source: The Honeyguide's revenge from African Storybook
Creative Commons License
This work is licensed under a Creative Commons Attribution 3.0 International License.
Options
Back to stories list Download PDF