Download PDF
Back to stories list

Wa Vuusi Sista Se Alichokisema dada yake Vusi

Written by Nina Orange

Illustrated by Wiehan de Jager

Translated by Georgette McGlashen

Language Jamaican Creole

Level Level 4

Narrate full story The audio for this story is currently not available.


Wan maanin orli Vuusi grani kaal im, “Vuusi, du kyari da eg ya go a yu pierens yaad. Dem waan fi mek wahn big kiek fi yu sista wedn”.

Siku moja asubuhi bibi yake Vusi alimwita na kumwambia, “Tafadhali peleka yai hili kwa wazazi wako. Wanataka kutengeneza keki kubwa kwa ajili ya harusi ya dada yako.”


Pan im wie go a im pierens, Vuusi bok op inna tuu bwaai pikni a pik fruut. Wan a di bwaai pikni dem grab di eg frahn Vuusi an fling it aafa wahn chrii. Di eg brok.

Alipokuwa njiani kuelekea kwa wazazi wake, Vusi akakutana na vijana wawili wanaokota matunda. Kijana mmoja akanyakua yai kutoka kwa Vusi na akalirusha kwenye mti. Yai likavunjika.


“A we yu du?” Vuusi baal out. “Da eg de a fi wahn kiek. Di kiek a fi mi sista wedn. Wa mi sista ago se ef shi no av no wedn kiek?”

“Umefanya nini?” Vusi akalia. “Yai lile lilikuwa kwa ajili ya keki. Keki ilikuwa kwa ajili ya harusi ya dada yangu. Dada yangu atasemaje kama hakutakuwa na keki ya harusi?”


Di bwaai pikni did sari fi a tiiz Vuusi. “Wi kyaahn elp wid di kiek, bot si wahn waakin stik ya fi yu sista,” wan a dem se. Vuusi kantinyu pan im jorni.

Vijana wale waliomba msamaha kwa kumchokoza Vusi. “Hatuna la kufanya kuhusu keki, lakini hii hapa ni fimbo kwa ajili ya dada yako,” mmoja alisema. Vusi akaendelea na safari yake.


Pan di wie im bok op inna tuu man a bil a ous. “Wi kyan yuuz da chrang stik de?” wan a dem aks se. Bot di stik no chrang inof fi bil ous, an it brok.

Njiani alikutana na wanaume wawili wakijenga nyumba. “Tunaweza kutumia hiyo fimbo imara?” mmoja akaomba. Lakini fimbo haikuwa imara kwa kujengea, na ikavunjika.


“A we yu du?” Vuusi baal out se. “Da stik de a did wahn prezent fi mi sista. Di fruut-pika gi mi di stik kaaz dem brok di eg fi di kiek. Di kiek a did fi mi sista wedn. Nou no eg no de-de, no kiek, an no prezent. Wa mi sista ago se?”

“Mmefanya nini?” Vusi akalia. “Fimbo hii ilikuwa zawadi kwa ajili ya dada yangu. Waangua matunda walinipa fimbo hiyo kwa sababu walivunja yai la keki. Keki ilikuwa ni kwa ajili ya harusi ya dada yangu. Sasa hakuna yai, hakuna keki, na hakuna zawadi. Dada yangu atasemaje?”


Di bilda dem did sari fi brok di stik. “Wi kyaahn elp wid di kiek, bot si som schraa ya fi yu sista,” wan a dem se. An den Vuusi kantinyu pan im jorni.

Wajenzi waliomba msamaha kwa kuvunja fimbo. “Hatuna la kufanya kuhusu keki, lakini tutakupa makuti umpelekee dada yako,” mmoja alisema. Na Vusi akaendelea na safari yake.


Pan di wie, Vuusi bok op inna wahn faama an wahn kou. “Da schraa de luk laik it ties nais, mi kyan ties it?” di kou se. Bot di schraa did ties so gud dat di kou nyam aaf aal a it.

Njiani, Vusi akakutana na mkulima akiwa na ng’ombe. “Una makuti mazuri, naweza kupata kidogo?” Ng’ombe akaomba. Lakini makuti yalikuwa matamu ng’ombe akayala yote!


“A we yu du?” Vuusi baal out se. “Da schraa de a did wahn prezent fi mi sista. Di bilda dem gi mi di schraa bikaaz dem brok di stik we di fruut-pika gi mi. Di fruut-pika gi mi di stik kaaz dem brok di eg fi mi sista kiek. Di kiek a did fi mi sista wedn. Nou no eg no de-de, no kiek, an no prezent. We mi sista a go se?”

“Umefanya nini?” Vusi akalia. “Makuti haya yalikuwa zawadi ya dada yangu. Wajenzi walinipa makuti kwa kuwa walivunja fimbo yangu niliyopewa na waangua matunda. Waangua matunda walinipa fimbo kwa kuwa walivunja yai kwa ajili ya keki ya dada yangu. Keki ilikuwa kwa ajili ya harusi ya dada yangu. Sasa hakuna yai, hakuna keki, na hakuna zawadi. Dada yangu atasemaje?”


Di kou did sari se shi did so krievn. Di faama agrii se di kou kuda go wid Vuusi az a prezent fi im sista. An so, Vuusi gwaan we im did a go.

Ng’ombe aliomba msamaha kwa kuwa mlafi. Mkulima alikubali kumpa Vusi ng’ombe aende naye kama zawadi kwa ajili ya dada yake. Vusi akaendelea na safari yake.


Bot di kou ron go bak tu di faama wen a dina taim. An Vuusi get laas pan im wie. Im riich liet-liet fi im sista wedn. Di ges dem did a nyam aredi.

Lakini wakati wa chakula cha jioni ng’ombe alikimbia kurudi kwa mkulima. Na Vusi akapotea njiani. Akafika kwa kuchelewa sana kwenye harusi ya dada yake. Wageni walikuwa tayari wanakula.


“A we mi a go du?” Vuusi baal out se. “Di kou we ron we a did wahn prezent, fi di schraa we di bilda dem gi mi. Di bilda dem gi mi di schraa bikaaz dem brok di stik we di fruut-pika dem gi mi. Di fruut-pika gi mi di stik bikaaz dem brok di eg fi di kiek. Di kiek a did fi di wedn. Nou no eg, no kiek, an no prezent.”

“Nifanye nini?” alilia Vusi. “Ng’ombe aliyekimbia alikuwa ni zawadi, ambayo nilipewa kama mbadala wa makuti niliyopewa na wajenzi. Wajenzi walinipa makuti kwa sababu walivunja fimbo niliyopewa na waangua matunda. Waangua matunda walinipa fimbo kwa sababu walivunja yai la keki. Keki ilikuwa kwa ajili ya harusi. Kwa hiyo hakuna yai, hakuna keki, na hakuna zawadi.”


Vuusi sista tingk fi a wail, den shi se, “Vuusi mi breda, mi no riili bizniz bout no prezent. Mi no iivn kier bout no kiek! Aal a wi de ya tugeda, an mi api. Nou, go put aan yu gud kluoz an mek wi selibriet tide!” An so, a dat Vuusi did du.

Dada yake Vusi alifikiria kwa muda, halafu akasema, “Kaka yangu Vusi, usijali zawadi, pia usijali keki! Tupo hapa pamoja, nina furaha. Nenda kavae nguo zako nadhifu na uje tusherehekee siku hii!”


Written by: Nina Orange
Illustrated by: Wiehan de Jager
Translated by: Georgette McGlashen
Language: Jamaican Creole
Level: Level 4
Source: What Vusi's sister said from African Storybook
Creative Commons License
This work is licensed under a Creative Commons Attribution 3.0 International License.
Options
Back to stories list Download PDF