Download PDF
Back to stories list

Kuku na Tai Kuku na Tai

Written by Ann Nduku

Illustrated by Wiehan de Jager

Translated by Matteo E. Mwita

Read by Lauwo George

Language Kiswahili

Level Level 3

Narrate full story

Reading speed

Autoplay story


Hapo zamani za kale, Kuku na Tai walikuwa marafiki. Waliishi kwa amani na ndege wengine. Hakuna kati yao aliyeweza kupaa.

Hapo zamani za kale, Kuku na Tai walikuwa marafiki. Waliishi kwa amani na ndege wengine. Hakuna kati yao aliyeweza kupaa.


Kuna siku njaa ilitokea. Ikamlazimu Tai kutembea umbali mrefu kutafuta chakula. Alirudi akiwa amechoka sana. “Lazima kuwe na njia rahisi ya kusafiri!” Tai alisema.

Kuna siku njaa ilitokea. Ikamlazimu Tai kutembea umbali mrefu kutafuta chakula. Alirudi akiwa amechoka sana. “Lazima kuwe na njia rahisi ya kusafiri!” Tai alisema.


Baada ya usingizi mnono wa usiku, Kuku alijiwa na wazo zuri sana. Akaanza kukusanya manyoya yaliyodondoka kutoka kwa ndege wenzao. “Tuyashonee haya manyoya juu ya manyoya yetu,” Kuku alisema. “Labda itaturahisishia kusafiri.”

Baada ya usingizi mnono wa usiku, Kuku alijiwa na wazo zuri sana. Akaanza kukusanya manyoya yaliyodondoka kutoka kwa ndege wenzao. “Tuyashonee haya manyoya juu ya manyoya yetu,” Kuku alisema. “Labda itaturahisishia kusafiri.”


Tai pekee ndiye aliyekuwa na sindano kijijini, kwa hiyo akaanza kushona wa kwanza. Akajitengenezea mabawa mawili mazuri na akapaa juu ya kuku. Kuku aliazima sindano lakini akachoka kushona baada ya muda mfupi. Akaacha sindano kabatini na akaenda jikoni kuandaa chakula kwa ajili ya watoto wake.

Tai pekee ndiye aliyekuwa na sindano kijijini, kwa hiyo akaanza kushona wa kwanza. Akajitengenezea mabawa mawili mazuri na akapaa juu ya kuku. Kuku aliazima sindano lakini akachoka kushona baada ya muda mfupi. Akaacha sindano kabatini na akaenda jikoni kuandaa chakula kwa ajili ya watoto wake.


Lakini ndege wengine walimwona Tai akipaa. Wakamwomba Kuku awaazime sindano ili nao wajishonee mabawa pia. Muda si mrefu ndege wakawa wamepaa na kuzagaa anga zima.

Lakini ndege wengine walimwona Tai akipaa. Wakamwomba Kuku awaazime sindano ili nao wajishonee mabawa pia. Muda si mrefu ndege wakawa wamepaa na kuzagaa anga zima.


Ndege wa mwisho aliporudisha sindano aliyoazima, Kuku hakuwepo. Kwa hiyo watoto wake wakachukua sindano na wakaanza kuichezea. Walipochoka na mchezo wao, wakaiacha sindano kwenye mchanga.

Ndege wa mwisho aliporudisha sindano aliyoazima, Kuku hakuwepo. Kwa hiyo watoto wake wakachukua sindano na wakaanza kuichezea. Walipochoka na mchezo wao, wakaiacha sindano kwenye mchanga.


Baadaye jioni Tai akarudi. Akaomba sindano ili aweze kushona baadhi ya manyoya yaliyokuwa yameanza kulegea alipokuwa safarini. Akaangalia kwenye kabati. Akaangalia jikoni. Akaangalia uani. Ila sindano haikupatikana.

Baadaye jioni Tai akarudi. Akaomba sindano ili aweze kushona baadhi ya manyoya yaliyokuwa yameanza kulegea alipokuwa safarini. Akaangalia kwenye kabati. Akaangalia jikoni. Akaangalia uani. Ila sindano haikupatikana.


“Nipatie siku moja,” Kuku alimwomba Tai. “Halafu utaweza kushona bawa lako na kuruka tena kwenda kutafuta chakula.” “Siku moja tu,” alisema Tai. “Kama hutaipata sindano, itabidi unipe kimoja cha vifaranga vyako kama malipo.”

“Nipatie siku moja,” Kuku alimwomba Tai. “Halafu utaweza kushona bawa lako na kuruka tena kwenda kutafuta chakula.” “Siku moja tu,” alisema Tai. “Kama hutaipata sindano, itabidi unipe kimoja cha vifaranga vyako kama malipo.”


Tai aliporudi siku iliyofuata, alimkuta Kuku akichakura mchangani, ila hakukuwa na sindano. Kwa hiyo Tai alishuka kwa kasi na kukwapua kifaranga kimoja. Akaondoka nacho. Tangu hapo, kila Tai anapojitokeza humkuta Kuku akichakura kwenye mchanga akitafuta sindano.

Tai aliporudi siku iliyofuata, alimkuta Kuku akichakura mchangani, ila hakukuwa na sindano. Kwa hiyo Tai alishuka kwa kasi na kukwapua kifaranga kimoja. Akaondoka nacho. Tangu hapo, kila Tai anapojitokeza humkuta Kuku akichakura kwenye mchanga akitafuta sindano.


Kila kivuli cha mabawa ya Tai kinapoonekana ardhini, Kuku huwatahadharisha vifaranga vyake. “Tokeni kwenye eneo la wazi.” Na wanajibu: “Sisi si wajinga. Tutakimbia.”

Kila kivuli cha mabawa ya Tai kinapoonekana ardhini, Kuku huwatahadharisha vifaranga vyake. “Tokeni kwenye eneo la wazi.” Na wanajibu: “Sisi si wajinga. Tutakimbia.”


Written by: Ann Nduku
Illustrated by: Wiehan de Jager
Translated by: Matteo E. Mwita
Read by: Lauwo George
Language: Kiswahili
Level: Level 3
Source: Hen and Eagle from African Storybook
Creative Commons License
This work is licensed under a Creative Commons Attribution 3.0 International License.
Options
Back to stories list Download PDF