Download PDF
Back to stories list

Kuku na Jongoo Kuku na Jongoo

Written by Winny Asara

Illustrated by Magriet Brink

Translated by Matteo E. Mwita

Read by Lauwo George

Language Kiswahili

Level Level 3

Narrate full story

Reading speed

Autoplay story


Kuku na Jongoo walikuwa marafiki. Ila walikuwa wanashindana kila mara. Siku moja wakaamua kucheza mpira wa miguu ili waweze kubaini nani alikuwa mchezaji bora zaidi.

Kuku na Jongoo walikuwa marafiki. Ila walikuwa wanashindana kila mara. Siku moja wakaamua kucheza mpira wa miguu ili waweze kubaini nani alikuwa mchezaji bora zaidi.


Wakaenda uwanjani na wakaanza kucheza. Kuku alikuwa na kasi ila Jongoo alikuwa na kasi zaidi. Kuku alipiga mpira mbali, ila Jongoo alipiga mbali zaidi. Kuku akaanza kupandwa na hasira.

Wakaenda uwanjani na wakaanza kucheza. Kuku alikuwa na kasi ila Jongoo alikuwa na kasi zaidi. Kuku alipiga mpira mbali, ila Jongoo alipiga mbali zaidi. Kuku akaanza kupandwa na hasira.


Wakaamua kupigiana penati. Jongoo akaenda golini. Kuku alifunga goli moja pekee. Ikawa zamu ya kuku kwenda golini.

Wakaamua kupigiana penati. Jongoo akaenda golini. Kuku alifunga goli moja pekee. Ikawa zamu ya kuku kwenda golini.


Jongoo alipiga mpira akafunga. Jongoo akapiga chenga akafunga. Jongoo akapiga kichwa akafunga. Jongoo akafunga magoli matano.

Jongoo alipiga mpira akafunga. Jongoo akapiga chenga akafunga. Jongoo akapiga kichwa akafunga. Jongoo akafunga magoli matano.


Kuku akakasirika kwa kuwa amefungwa. Hakuwa mshindani mzuri. Jongoo akaanza kucheka kwa sababu rafiki yake alikuwa analalamika.

Kuku akakasirika kwa kuwa amefungwa. Hakuwa mshindani mzuri. Jongoo akaanza kucheka kwa sababu rafiki yake alikuwa analalamika.


Kuku alipatwa na hasira kiasi kwamba akafungua mdomo wake mkubwa na akammeza Jongoo.

Kuku alipatwa na hasira kiasi kwamba akafungua mdomo wake mkubwa na akammeza Jongoo.


Kuku alipokuwa anarudi nyumbani alikutana na Mama yake Jongoo. Mama Jongoo akamuuliza, “Umemwona mwanangu?” Kuku hakujibu kitu. Mama Jongoo akapatwa na wasiwasi.

Kuku alipokuwa anarudi nyumbani alikutana na Mama yake Jongoo. Mama Jongoo akamuuliza, “Umemwona mwanangu?” Kuku hakujibu kitu. Mama Jongoo akapatwa na wasiwasi.


Mama Jongoo akasikia sauti kwa mbali. “Nisaidie mama!” ile sauti ililia. Mama Jongoo akaangalia huku na kule na kusikiliza kwa makini. Sauti ilitokea tumboni mwa kuku.

Mama Jongoo akasikia sauti kwa mbali. “Nisaidie mama!” ile sauti ililia. Mama Jongoo akaangalia huku na kule na kusikiliza kwa makini. Sauti ilitokea tumboni mwa kuku.


Mama Jongoo alipiga kelele, “Tumia nguvu yako ya kipekee mwanangu!” Majongoo wanaweza kutoa harufu mbaya na ladha ya ajabu. Kuku akaanza kujisikia mgonjwa.

Mama Jongoo alipiga kelele, “Tumia nguvu yako ya kipekee mwanangu!” Majongoo wanaweza kutoa harufu mbaya na ladha ya ajabu. Kuku akaanza kujisikia mgonjwa.


Kuku akabeuwa. Akameza mate na kutema. Halafu akapiga chafya na kukohoa. Akakohoa tena. Jongoo alimfanya ajisikie vibaya.

Kuku akabeuwa. Akameza mate na kutema. Halafu akapiga chafya na kukohoa. Akakohoa tena. Jongoo alimfanya ajisikie vibaya.


Kuku alikohoa, hadi akamtema jongoo aliyekuwa tumboni mwake. Mama Jongoo na mwanaye wakakwea mti kujificha.

Kuku alikohoa, hadi akamtema jongoo aliyekuwa tumboni mwake. Mama Jongoo na mwanaye wakakwea mti kujificha.


Tangu hapo, Kuku na Jongoo ni maadui.

Tangu hapo, Kuku na Jongoo ni maadui.


Written by: Winny Asara
Illustrated by: Magriet Brink
Translated by: Matteo E. Mwita
Read by: Lauwo George
Language: Kiswahili
Level: Level 3
Source: Chicken and Millipede from African Storybook
Creative Commons License
This work is licensed under a Creative Commons Attribution 3.0 International License.
Options
Back to stories list Download PDF