Download PDF
Back to stories list

Magozee Magozwe

Written by Lesley Koyi

Illustrated by Wiehan de Jager

Translated by Demoze Degefa

Language Oromo

Level Level 5

Narrate full story The audio for this story is currently not available.


Magaala Nyiroobii irraa fagooti ijooleen mana dhabiyyin manaan ala jiraata turan. Guyyaa maraa akkuma dhufite kessumessu. Guyyaa ganama tokko ijooleen kun afaa irra rafanii bulan marachu jalqaban. Akka isaaniti hinqorrinee waan garagaraa boobesanii o’ifatu. Magozeen garee ijoole kana kessa namtokko dha. Magozeenis umriidhan isa xiqqa ture.

Kwenye jiji la Nairobi lenye pilikapilika nyingi, mbali na malezi ya nyumbani, paliishi kikundi cha wavulana wasiokuwa na makwao. Waliipokea kila siku ijayo kama ilivyo. Siku moja asubuhi, walikuwa wanakusanya virago vyao baada ya kulala kwenye baridi kando ya barabara. Ili kuondoa baridi, walikoka moto kwa kutumia takataka. Miongoni mwa kikundi hicho cha wavulana alikuwepo Magozwe. Alikuwa ni mdogo kuliko wote.


Yeroo matiin isaa du’u Magozee waggaa shan qofa ture. Magozeenis essumaa isa wajjiiin jirachuf bira dhaqee. Namni kuni garauu mucaa kanaf bayee hindhimamnee. Magozeedhaf nyataa gahaa hinkenninef. Mucichi garu hojii bayee akka hojaatu godhe.

Wakati wazazi wa Magozwe walipofariki, alikuwa na miaka mitano tu. Alienda kuishi na mjomba wake. Mjomba hakumjali Magozwe. Hakumpa chakula cha kutosha. Alimfanyisha kazi nyingi nzito.


Yeroo Magozee gaafi kasuu essumina isa isa tumaa. Yeroo immo Magozeen gara mana barnoota nandeema jedhe gaafatu, essumini isaa akan jedhe: “Bayee raata’a waan tateef barumsi sif galu hindanda’u.” Wagga sadi booda Magozee mana essuma isa dhisee deeme. Daandi gubba jirachu calqabee.

Magozwe alipolalamika au kuuliza, mjomba wake alimpiga. Magozwe alipouliza kama ataweza kwenda shule, mjomba wake alimpiga na kumwambia, “Wewe ni mjinga, hutaweza kujifunza chochote.” Baada ya miaka mitatu ya kunyanyaswa, Magozwe alitoroka kwa mjomba wake. Akaanza kuishi mtaani.


Jiruun dandii gubba hamaa ture. Ijooleen waan nyaatan argachuuf bayee dhama’aa turan. Ijollen kun yeroo tokko tokko nihidhaamu, nitumaamus. Yeroo dhibaman namni isaan gargaruu hinturre. Gareen kuni kan jiraatu mallaqa kadhaafi meshaale xixinno gurguratuuni. Jireenya isaani irra caala kan hammesse waldhanis gareen kuni garee biraa wajjiin qabudha.

Maisha ya mtaani yalikuwa magumu na wavulana wengi walipambana kila siku ili wapate chakula tu. Mara nyingine walikamatwa, mara nyingine walipigwa. Walipougua, kulikuwa hakuna mtu wa kuwasaidia. Kikundi kilitegemea hela ndogo ndogo walizopata kwa kuomba omba, na kwa kuuza plastiki na vitu kuukuu. Maisha yalikuwa magumu zaidi hasa kwa sababu ya vita dhidi ya vikundi pinzani vilivyotaka kudhibiti baadhi ya maeneo ya jiji.


Guyyaa tokko Magozee yeroo qawwaa balfa kessa yeroo ilaalu kitaaba senaa duloomaa tokko argate. Kitaabicha qulqullesse keeshaa isa kessa godhate. Guyyaa sana irra caalqabee kitaabicha banee suraawan adda adda ilaala ture. Kitaabicha akka itti dubbisu hinbeeku ture.

Siku moja Magozwe alipokuwa anachakura kwenye mapipa ya takataka, alikuta kitabu cha hadithi kilichokuwa kimechakaa. Aliondoa uchafu kwenye kitabu na kukiweka ndani ya mfuko wake. Kila siku baada ya hapo, alikitoa kitabu na kuangalia picha. Hakujua kusoma maandishi.


Suuraawan sun wa’ee mucaa paylata ta’uf fedhii qabu akkamit akka guddate agarsiisa. Magazeenis paylata ta’uf yaddan balali’ee. Yeroo tokko tokko akkan mucaa seenaa sanati of ilaala,

Picha zilikuwa zinaongelea hadithi ya mvulana ambaye alikuja kuwa rubani. Magozwe aliota kuwa rubani. Mara nyingine alifikiria kwamba yeye ni yule mvulana kwenye hadithi.


Guyyaan bayee qorraa dha yeroo Magazeeen kara gubba dhabate kadhatu. Namni tokko itti kiiqee akan jedheen,” Ashamaa, ani Tomaas jedham. Ani lafa ati waan nyaatu argatutaan hojadha.” Namni kunis karkaan gara mana kelloo kan gubbaan isaa dokiyyee ta’ee it agarsisee.” Bakka mana sana dhaqtee akka nyaata argatu abdiin qaba?” jedhe gafatee. Magazzenis yeroo tokko gara manichaa yeroo biraa immo gara namichaa ilaale. “Akka tasa,” jedhe gara mannicha deeme.

Kulikuwa na baridi na Magozwe alikuwa amesimama barabarani akiomba omba. Mtu alimkaribia. “Hujambo? Naitwa Thomas. Nafanya kazi karibu na hapa, mahali unapoweza kupata kitu cha kula,” mtu yule alisema. Alionyesha nyumba ya njano yenye paa la buluu. “Natumaini utaenda pale kupata chakula kidogo?” Thomas aliuliza. Magozwe alimwangalia yule mtu, kisha akaiangalia ile nyumba. “Labda,” akasema, halafu akaondoka.


Ji’oota ittiaanan kessatti manadhabeyyni kun Tomaasni walarguu cimsanii qaban. Innis immo namoota wajjiin kessaahu namoota karaa gubbaa jirataniin hasa’u jallata. Senaa namoota dhaggefachu jallata. Tomaas nama amala garii qabuufi nama namaa tufatu mit. Ijoolen tokko tokko gara guyyaa walakaa irrati gara mana kelloo fi doqiyoo sana deemudhan waan nyataan argatan.

Miezi iliyofuata, wavulana wale wa mtaani walizoea kumwona Thomas hapa na pale. Alipenda kuzungumza na watu, hasa walioishi mitaani. Thomas alisikiliza simulizi za maisha ya watu. Alikuwa makini na mwenye subira, na hakuwa na kiburi wala dharau. Baadhi ya wavulana walianza kwenda kwenye ile nyumba ya njano na buluu ili kupata chakula cha mchana.


Yeroo Tomaas dhufee Magozee bira ta’u Magozeen immo kitaaba dubbisa ture. Tomaas akkan jedhe isa gafate, “Seenaa malii dubsitaa?” “Wa’ee mucaa paylata ta’eeti” jedhene Magozee. Tomaas, “Maqaa isaa enyuu jedhe gaafate?” “Anni himbekku, dubbisu hindanda’u,” jedhe Magozeen.

Magozwe alikuwa amekaa kando ya barabara akiangalia kitabu chake cha picha Thomas alipokaa pembeni mwake. “Hadithi hiyo inahusu nini?” Thomas akauliza. “Inahusu mvulana aliyekuja kuwa rubani,” Magozwe akajibu. “Jina lake ni nani?” Thomas akauliza. “Sijui, siwezi kusoma,” Magozwe akasema kwa sauti ya chini.


Yeroo walqunnaman Magozee seenaa mataa isaa Tomaasiti himuu calaqabee. Seenaan isaas wa’ee essuma isaatif akka inni itti mana bahee ilaalchisee ture. Tomaas bayee hindubbannes waan Magozeen godhuu qabuus itti hinmnee. Yeroo tokko tokko manaa nyataa kelloo sanaa kessati hasa’u.

Walipokutana, Magozwe alianza kumsimulia Thomas maisha yake. Alimwelezea kuhusu mjomba wake na sababu zilizomfanya atoroke. Thomas hakuongea sana, wala hakumwambia Magozwe nini cha kufanya, bali alisikiliza kwa makini kila mara. Wakati mwingine waliongea wakiwa wanakula kwenye ile nyumba yenye paa la buluu.


Woggaa kurnaffa Magozee irrati, Tomaas kitaaba seenaa tokko kennef. Kitaabichis wa’ee mucaa badiyya tokko kan guddate taphaata kubba milaa ta’eedha. Tomaasis seenaa kana yeroo bayee dubbiseef, akkan jedheen, Amma yeroo ati mana barmusaa dhaqixee dubbisufi barressu barrachuu qabdu dha. Mal yaddaa jedhee gafatee?” Tomaasis lafaa ijoolen itti dhaqxee barattu itti ibsee.

Mnamo mwaka wa kumi wa kuzaliwa kwa Magozwe, Thomas alimzawadia kitabu kipya cha hadithi. Ilikuwa ni hadithi inayohusu mvulana wa kijijini aliyekuja kuwa mcheza mpira maarufu. Thomas alimsomea Magozwe hadithi hiyo mara nyingi, mpaka siku moja akasema, “Nafikiri wakati umewadia wa kwenda shule kujifunza kusoma. Unaonaje?” Thomas alieleza kwamba anajua sehemu ambayo watoto wanaweza kuishi na kwenda shule.


Magozeenis wa’ee iddoo hara’a kana fi wa’ee gara mana barnoota deemu ittiyada ture. Yoo wanti essumni isaa jedhe sirri ta’e garuu inni barachuu hodadhabee? Yoo lafa hara’a kanati issa rukutan? Bayee sodaate. “Gara gubba jirachu wayya ta’a jedhe yaade.”

Magozwe alifikiria kuhusu sehemu hii mpya, na kuhusu kwenda shule. Itakuwaje kama mjomba wake alikuwa sahihi kwamba alikuwa mjinga kiasi cha kutoweza kujifunza chochote? Itakuwaje kama watampiga sehemu hii mpya? Aliogopa. “Labda ni heri kuendelea kuishi mtaani,” aliwaza.


Sodaa isas Tomaasit himee. Yeroo dheera booda Tomaas jiruun lafa hara’a kanati mishaa akka ta’u itti hime.

Alimshirikisha Thomas juu ya hofu aliyokuwa nayo. Baada ya muda Thomas alimhakikishia kwamba maisha yatakuwa bora huko sehemu mpya.


Haaluma kanan Magozeen lafa hara’a sana dhaqee mana doqiyye sana kessa gale. Namoota lama wajjiin kutaa tokko kessaa walwajjiin jiratan. walmaa galatti ijoolee 10 mana sana kessa gala. Anitee, sisii fi abbaa manaa ishee, saree 3 fi addurre tokko fi ra’ee dullooma taokko mana sana kessa gala.

Kwa hiyo Magozwe alihamia kwenye chumba katika nyumba yenye paa la kijani. Alikaa chumba kimoja na wavulana wengine wawili. Kwa ujumla kulikuwa na watoto kumi walioishi kwenye nyumba ile. Waliishi pamoja na Shangazi Cissy na mume wake, mbwa watatu, paka mmoja, na mbuzi aliyezeeka.


Magozeen barmusaa calqabee garu barmusi itti cimee. Bayee dubati hafee ture. Yeroo tokko tokko dhisulee yaada. Garuu wa’ee paylata fi taphaata kubbaa milaa yeroo yaddu immo yada isaa jijjira. Mana barmusaa kessaa hinbanee.

Magozwe alianza shule na ilikuwa ngumu. Alikuwa na mengi ya kujifunza. Mara nyingine alitaka kukata tamaa. Lakini aliwaza kuhusu rubani na mcheza mpira kwenye vitabu vya hadithi. Kama wao, hakukata tamaa.


Magozeen oddoo kessa ta’ee kitaabaa mana magarisaa irra argatee san dubbisaa. Tomaas dhufee mal godhaa jirta jedhe isa gafate. “Wa’ee mal dubistaa?” “Wa’ee mucaa barsiisaa ta’eti,” jedhe Magozeen. “Maqaan mucaa sani enyuu dha?” jedhe Tomaas. “Maqaan isaa, Magozee,” jedhama.

Magozwe alikuwa amekaa uani kwenye nyumba yenye paa la kijani, akisoma kitabu cha hadithi cha shule. Thomas alikuja na kukaa kando yake. “Hadithi inahusu nini?” Thomas akauliza. “Inahusu mvulana aliyekuja kuwa mwalimu,” Magozwe akajibu. “Jina lake ni nani?” akauliza Thomas. “Jina lake ni Magozwe,” Magozwe akasema kwa tabasamu.


Written by: Lesley Koyi
Illustrated by: Wiehan de Jager
Translated by: Demoze Degefa
Language: Oromo
Level: Level 5
Source: Magozwe from African Storybook
Creative Commons License
This work is licensed under a Creative Commons Attribution 4.0 International License.
Read more level 5 stories:
Options
Back to stories list Download PDF