Download PDF
Back to stories list

Bwezela ya Msogoleli wa njuci Kisasi cha Kiongozi

Written by Zulu folktale

Illustrated by Wiehan de Jager

Translated by Sitwe Benson Mkandawire

Read by Christine Mwanza

Language Nyanja

Level Level 4

Narrate full story The audio for this story is currently not available.


Iyi ndi nkhani ya Ngede, msogoleli wa njuci, ndi munyamata ozikonda ochedwa Gingile. Tsiku lina pamene Gingile anacokapo kukasaka nyama mthengo, anamva Ngede kuitana. Gingile anamva njala ya uci kwambiri. Anaimilira ndikumvetsetsa, kusakira mpaka anaona mbalame m’mwamba mwamtengo. “Chiti-chiti-chiti,” mbalame inalira pamene inai kuluka ku kumtengo wina ndi winanso. “Chiti-chiti-chiti,” mbalame inaitana, ndikuimilira kawirikawiri kuyembekezela kuti Agingile alikubwela.

Hii ni hadithi ya Ngede, ambaye ni ndege mpenda asali, na mvulana mmoja mlafi anayeitwa Gingile. Siku moja Gingile alipokuwa akiwinda alisikia mwito wa Ngede. Kinywa chake kilianza kutokwa mate kwa kufikiria asali. Alisimama, akasikiliza na kuangalia vizuri hadi alipomwona yule ndege akiwa ametua kwenye matawi yaliyokuwa juu ya kichwa chake. “Chitik-chitik-chitik,” yule ndege mdogo alitatarika aliporuka na kutua kwenye mti mmoja hadi mwingine, na mwingine tena. “Chitik-chitik-chitik,” aliita, huku akinyamaza na kuhakikisha kwamba Gingile alikuwa amemfuata.


Pakanapita phindi zokwanila 30, anafika pa m’tengo ukulu ochedwa mkuyu. Ngede analumphalumpha mu m’tengo cimeneci kuuza Gingile kuti tafika. Gingile sanaone njuci pansi pa mtengo koma anadalira Ngede.

Baada ya nusu saa, walifika kwenye mti wa matini. Ngede aliruka kama mwenda wazimu kutoka tawi moja hadi jingine. Kisha alitulia kwenye tawi moja na kupindua kichwa chake akimwangalia Gingile kana kwamba anasema, “Ipo hapa! Njoo sasa! Kwa nini unachukua muda mrefu?” Gingile hakuweza kuona nyuki wowote kutoka chini ya mti, lakini alimwamini Ngede.


Gindile anaika pansi mkondo wake panyansi pa mtengo, anatenga nkhuni nakuyasha moto. Pamene moto unayaka bwino, anaika kamtengo katali pakati pamoto. Kamtengo kameneka kanali kuziwika pankhani yopanga chusi cambili pakupya. Anayamba kukwela cimtengo ndi kamtengo ka chusi pakamwa.

Kwa hivyo Gingile aliweka mkuki wake alioutumia kuwinda chini ya mti, akakusanya vijiti vilivyokauka na kuwasha moto mdogo. Moto ulipokuwa ukiwaka vizuri, alichomeka kijiti kirefu kwenye moto. Mti huu ulijulikana kwa kutoa moshi mwingi ulipokuwa unaungua. Alianza kukwea mti huku akishika kijiti kwa meno upande usiofuka moshi.


Posacedwa, anamva kulira kwa njuci. Zinali kulowa ndi kucoka m’mphako. Pamene Gingile anafika, anaika kamtengo kausi m’mphako. Njuci zinacoka mofulumira ndikukalipa. Zinathawa cifukwa sizinakonde usi ndiponso zikalibe kuyenda, zinamuluma Gingile.

Muda mfupi baadaye, aliweza kusikia sauti ya nyuki wenye harakati nyingi ikivuma. Walikuwa wakiingia na kutoka kwenye upenyo wa mti, yaani mzinga wao. Gingile alipoufikia mzinga, alisukuma ile kuni ya moto ndani ya ule upenyo. Nyuki waliharakisha kutoka ndani wakiwa na hasira na uchungu. Waliruka na kwenda mbali kwa sababu hawakupenda moshi – lakini walifanya hivyo baada ya kumuuma Gingile kwa uchungu!


Pamene njuci zinacoka, Gingile analowetsa dzanja lake mu m’mphako nakucosa uci umene unali ndi mafuta oyela. Anaika uci wake mukacola kamene ananyamula pephewa ndipo iye anayamba kuseluka m’mtengo.

Nyuki walipokuwa nje, Gingile aliingiza mikono yake ndani ya kiota. Alitoa kipande kikubwa cha sega kilichokuwa kinadondoka urojo mzito wa asali, na kilichojaa wadudu weupe wanene. Aliiweka taratibu ndani ya mkoba aliokuwa nao na kuanza kushuka kutoka mtini.


Ngede anali kuyangana zonse zamene Gingile anali kucita. Anali kuyembeza kuti amusiyileko uci kuthokoza pomulangiza. Ngede anayesa kufedera pafupi kuti amuoneko. Gingile anafika pansi pa mtengo ndiponse ngede anaimilira pa mwala kuyembekezera kuti amupaseko.

Ngede alishuhudia kila kitu Gingile alichofanya. Alikuwa anamsubiri abakishe kiasi kidogo cha asali kama shukurani kwa Kiongozi. Ngede aliruka kutoka tawi hadi tawi huku akikaribia chini. Mwishowe Gingile alifika chini ya mti. Ngede alitua kwenye mwamba karibu na mvulana huyo na kusubiri zawadi yake.


Koma Gingile anazimya moto, ndi kunyamula mkondo wake nakuyenda kunyumba kosamukumbuka Ngede. Ngede anamuitana mokalipa, “VIC-torr! VIC-torrr!” Gingile anaimilira, anayangana ka mbalame ndi kuseka kwambiri. “Ufuna uci, ha mzanga? Ndasewenza ndi kulumiwa ndekha! Nicifukwa cani ufuna ndikupaseko uci wabwino tere?” Iye anayenda. Ngede anakalipa kwambiri! Anakalpa! Koma azabwezela tsiku limodzi.

Lakini Gingile alizima moto, akachukua mkuki wake na kuanza safari kwenda nyumbani bila kumjali ndege yule. Ngede aliita kwa hasira, “USH-ndi! USH-ndi!” Gingile alisimama, akamkodolea macho yule ndege kisha akacheka kwa sauti. “Unataka asali kidogo, rafiki yangu? Ha! Lakini ni mimi niliyefanya kazi yote pamoja na kuumwa na nyuki. Kwa nini nikugawie hii asali tamu?” Baada ya kusema hivyo, aliondoka na kwenda zake. Ngede alikasirika sana! Hivi sivyo alivyostahili kutendewa! Ila atalipiza kisasi.


Tsiku limodzi, Gingile anamveranso kuti Ngede aitana. Anakumbukira uci wabwino uja ndiponso iye anakakonkhanso kanyoni. Pamene Gingile anakonkha kanyoni, kanamupeleka kumalupiri koipa. Pamene anafika kuja, Ngede anaimilira kuti apumuleko mcimtengo ca minga. “Ahh,” anaganiza Gingile. “Mphako ya njuci ifunika kupezeka umu mwamene m’mtengo”. Anapanga moto mwamsanga nakuyamba kukwela nakamtengo ka cusi kukamwa. Ngede anakhala cete ndi kutamba.

Siku moja baada ya majuma machache, Gingile tena alisikia mwito wa asali kutoka kwa Ngede. Aliikumbuka asali tamu, na kwa hamu alimfuata ndege yule kwa mara nyingine. Baada ya kumwongoza Gingile pembeni mwa msitu, Ngede alisimama na kupumzika chini ya mti wa mwavuli. “Ahh,” Gingile aliwaza. “Lazima mzinga umo ndani ya mti huu.” Kwa haraka aliwasha moto wake na kuanza kukwea mti huku akibeba kuni iliyotoa moshi katika meno yake. Ngede alikaa na kuangalia tu.


Gingile anakwela, nakuganiza kuti ncifukwa cani saona njuci kuimba monga mwanthawizonse. “Kapena mphako ya njuci ili mukati mwa mtengo,” anaziganizila. Anayendelako pamwamba. Koma mwakuti aone mphako, anaonana ndi nyalugwe! Nyalungwe anakalipa kwambiri posokoneza tulo kwake. Nyalugwe anacepesa maso ake ndikusegula kamwa kulangiza meno yakuthwa.

Gingile alipopanda, alishangaa kwa nini hakusikia sauti ya nyuki. “Pengine mzinga umo ndani zaidi katika mti,” alifikiria. Alipanda tena juu ya tawi jingine. Lakini badala ya mzinga, alijikuta uso kwa uso na chui! Chui alikuwa na hasira sana kwa sababu usingizi wake ulikuwa umekatizwa. Aliyafanya macho yake kuwa madogo, akaufungua mdomo wake na kuonyesha meno yake makubwa na makali.


Pamene Nyalungwe anayesa kumuluma Gingile, anaseluka cimtengo mwamsanga. Mofulumira, anagwa kuipa kucoka m’mtengo nakuzicita kwendo. Anathamanga mwansanga kuyopa nyalungwe. Mwamwai, Nyalugwe anali natulo kwambiri ndiponso iye sanamupitikise. Ngede, musogoleli wa njuci anabwezera. Ndiponso Gingile anaphunzirilapo.

Kabla ya Chui kumvamia Gingile, alishuka chini haraka. Katika haraka hiyo, aliteleza na kuanguka kwa kishindo huku akiumia mguu wake. Alirukaruka akienda kwa haraka alivyoweza. Kwa bahati nzuri, Chui alikuwa bado amelala kwa hivyo hakumfukuza. Ngede, Kiongozi alikuwa amelipiza kisasi chake na Gingile alikuwa amejifunza funzo lake.


Ngati ana aGingile amvela nkhani ya Ngede, amakapasa ulemu kanyoni. Akacosa uci, amasiyako uci wambiri kuti musogoleli wa njuci adye!

Kwa hivyo wakati watoto wa Gingile wanaposikia hadithi ya Ngede, wanamheshimu yule ndege. Kila wanapotoa asali, huhakikisha kwamba wanamwachia Kiongozi fungu kubwa!


Written by: Zulu folktale
Illustrated by: Wiehan de Jager
Translated by: Sitwe Benson Mkandawire
Read by: Christine Mwanza
Language: Nyanja
Level: Level 4
Source: The Honeyguide's revenge from African Storybook
Creative Commons License
This work is licensed under a Creative Commons Attribution 3.0 International License.
Options
Back to stories list Download PDF