Download PDF
Back to stories list

Magozwe Magozwe

Written by Lesley Koyi

Illustrated by Wiehan de Jager

Translated by Georgette McGlashen

Language Jamaican Creole

Level Level 5

Narrate full story The audio for this story is currently not available.


Inna di bizi siti a Nairuobi, faar fram a laif a uom kier, yu did av wahn gruup a bwaai pikni we no liv no we. Dem tek evridie jos az it kom. Pan wan a di maanin dem di bwaai pikni dem did a pak op dem mat dem fram aafa di kuol kangkriit we dem did a sliip. Fi fait aaf di kuol dem kech op faiya wid gyaabij. Mongs di gruup a bwaai pikni dem a did Magozwe. Im a did di liklis.

Kwenye jiji la Nairobi lenye pilikapilika nyingi, mbali na malezi ya nyumbani, paliishi kikundi cha wavulana wasiokuwa na makwao. Waliipokea kila siku ijayo kama ilivyo. Siku moja asubuhi, walikuwa wanakusanya virago vyao baada ya kulala kwenye baridi kando ya barabara. Ili kuondoa baridi, walikoka moto kwa kutumia takataka. Miongoni mwa kikundi hicho cha wavulana alikuwepo Magozwe. Alikuwa ni mdogo kuliko wote.


Wen Magozwe pierens dem did ded, im a did onggl faiv iez-uol. Im did go liv wid im ongkl. Di man neva bizniz bout di pikni. Im neva gi Magozwe inof fuud. Im mek di bwaai pikni du uol iip a aad wok.

Wakati wazazi wa Magozwe walipofariki, alikuwa na miaka mitano tu. Alienda kuishi na mjomba wake. Mjomba hakumjali Magozwe. Hakumpa chakula cha kutosha. Alimfanyisha kazi nyingi nzito.


Ef Magozwe komplien ar aks no kwestiyan, im ongkl biit im. Wen Magozwe aks ef im kuda go skuul, im ongkl biit im an se, “Yu tuu fuul-fuul fi lorn notn.” Afta chrii ierz a da chriitment de Magozwe ronwe fram im ongkl. Im did staat liv pan di schriit.

Magozwe alipolalamika au kuuliza, mjomba wake alimpiga. Magozwe alipouliza kama ataweza kwenda shule, mjomba wake alimpiga na kumwambia, “Wewe ni mjinga, hutaweza kujifunza chochote.” Baada ya miaka mitatu ya kunyanyaswa, Magozwe alitoroka kwa mjomba wake. Akaanza kuishi mtaani.


Schriit laif did aad an nof a di bwaai pikni dem did fain it aad evridie jos fi get fuud. Somtaim dem get lak op bai poliis, somtaim dem get biitn. Wen dem get sik, nobadi no de fi elp dem. Di gruup a bwaai pikni dipen pan di likl moni we dem get fram wen dem beg, an fram wen dem sel plaskit an ada tingz we yuuz agen. Laif di iivn muor aada kaaz a faitin wid kantenshos piipl uu waahn kantruol a som paat a di siti.

Maisha ya mtaani yalikuwa magumu na wavulana wengi walipambana kila siku ili wapate chakula tu. Mara nyingine walikamatwa, mara nyingine walipigwa. Walipougua, kulikuwa hakuna mtu wa kuwasaidia. Kikundi kilitegemea hela ndogo ndogo walizopata kwa kuomba omba, na kwa kuuza plastiki na vitu kuukuu. Maisha yalikuwa magumu zaidi hasa kwa sababu ya vita dhidi ya vikundi pinzani vilivyotaka kudhibiti baadhi ya maeneo ya jiji.


Wan die wen Magozwe did a luk chuu di gyaabij pan dem, im fain wahn uol tier op stuoribuk. Im kliin di dort aaf a it an put it inna im bag. Evridie afta dat im wuda tek out di buk an luk pan di picha dem. Im neva nuo ou fi riid di wod dem.

Siku moja Magozwe alipokuwa anachakura kwenye mapipa ya takataka, alikuta kitabu cha hadithi kilichokuwa kimechakaa. Aliondoa uchafu kwenye kitabu na kukiweka ndani ya mfuko wake. Kila siku baada ya hapo, alikitoa kitabu na kuangalia picha. Hakujua kusoma maandishi.


Di picha dem did a tel di stuori bout wahn bwaai pikni we gruo op an ton wahn pailat. Magozwe wuda diejriim bout se im a wahn pailat. Somtaim, im imajin se im a did di bwaai pikni inna di stuori.

Picha zilikuwa zinaongelea hadithi ya mvulana ambaye alikuja kuwa rubani. Magozwe aliota kuwa rubani. Mara nyingine alifikiria kwamba yeye ni yule mvulana kwenye hadithi.


It did kuol an Magozwe did a stan op pan di ruod a beg. Wahn man waak op tu im. “Eluo, mi a Tamas. Mi wok nier ya so, a wahn plies we yu kyahn get sopm fi nyam,” di man se. Im paint pan wahn yelo ous wid wahn bluu oustap. “Mi uop se yu wi go de go get som fuud?” im aks se. Magozwe luk pan di man, an den pan di ous. “Miebi,” im se, an waak we.

Kulikuwa na baridi na Magozwe alikuwa amesimama barabarani akiomba omba. Mtu alimkaribia. “Hujambo? Naitwa Thomas. Nafanya kazi karibu na hapa, mahali unapoweza kupata kitu cha kula,” mtu yule alisema. Alionyesha nyumba ya njano yenye paa la buluu. “Natumaini utaenda pale kupata chakula kidogo?” Thomas aliuliza. Magozwe alimwangalia yule mtu, kisha akaiangalia ile nyumba. “Labda,” akasema, halafu akaondoka.


Uova di neks kopl a monts dem, di bwaai pikni dem we no liv no we get yuuz tu si Tamas roun di plies. Tamas did laik taak tu piipl, espeshali piipl we liv pan di schriit. Tamas wuda lisn tu di stuori dem bout ou piipl liv. Im did siiros, an pieshent, neva ruud ar shuo no disrispek. Som a di bwaai pikni dem did staat go a di yelo an bluu ous inna di migl a di die fi get fuud.

Miezi iliyofuata, wavulana wale wa mtaani walizoea kumwona Thomas hapa na pale. Alipenda kuzungumza na watu, hasa walioishi mitaani. Thomas alisikiliza simulizi za maisha ya watu. Alikuwa makini na mwenye subira, na hakuwa na kiburi wala dharau. Baadhi ya wavulana walianza kwenda kwenye ile nyumba ya njano na buluu ili kupata chakula cha mchana.


Magozwe did a siddong pan di kangkriit a luk pan im picha buk wen Tamas kom siddong bisaid a im. “We di stuori bout?” Tamas aks se. “A bout wahn bwaai pikni we ton a pailat,” im ansa se. “We di bwaai pikni niem?” Tamas aks se. “Mi no nuo, mi kyaahn riid,” Magozwe wispa se.

Magozwe alikuwa amekaa kando ya barabara akiangalia kitabu chake cha picha Thomas alipokaa pembeni mwake. “Hadithi hiyo inahusu nini?” Thomas akauliza. “Inahusu mvulana aliyekuja kuwa rubani,” Magozwe akajibu. “Jina lake ni nani?” Thomas akauliza. “Sijui, siwezi kusoma,” Magozwe akasema kwa sauti ya chini.


Wen dem di miit, Magozwe did staat tel Tamas di stuori bout imself. A did di stuori bout im ongkl an wai im ron we. Tamas neva taak nof, an im neva tel Magozwe wa fi du, bot im alwiez lisn gud tu evriting. Somtaim dem wuda taak wentaim dem a nyam a di ous wid di bluu oustap.

Walipokutana, Magozwe alianza kumsimulia Thomas maisha yake. Alimwelezea kuhusu mjomba wake na sababu zilizomfanya atoroke. Thomas hakuongea sana, wala hakumwambia Magozwe nini cha kufanya, bali alisikiliza kwa makini kila mara. Wakati mwingine waliongea wakiwa wanakula kwenye ile nyumba yenye paa la buluu.


Roun wen Magozwe a go bi ten iez-uol, Tamas gi’im wahn nyuu stuori buk. A did wahn stuori bout wahn bwaai pikni fram di vilij we gruo op fi bi wahn fiemos futbaala. Tamas riid di stuori tu Magozwe uol iip a taim, so til wan die im se, “Mi tingk a taim nou yu go a skuul an lorn fi riid. We yu tingk?” Tamas tel im se im nuo bout wahn plies we pikni kuda stie, an go a skuul.

Mnamo mwaka wa kumi wa kuzaliwa kwa Magozwe, Thomas alimzawadia kitabu kipya cha hadithi. Ilikuwa ni hadithi inayohusu mvulana wa kijijini aliyekuja kuwa mcheza mpira maarufu. Thomas alimsomea Magozwe hadithi hiyo mara nyingi, mpaka siku moja akasema, “Nafikiri wakati umewadia wa kwenda shule kujifunza kusoma. Unaonaje?” Thomas alieleza kwamba anajua sehemu ambayo watoto wanaweza kuishi na kwenda shule.


Magozwe did tingk bout di nyuu plies, an bout fi go a skuul. Wa’apm ef im ongkl did rait an im did tuu fuul-fuul fi lorn notn. Wa’apm ef dem giim biitn a di nyuu plies? Im di fried. “Miebi a did beta fi stie an liv pan di schriit,” im tingk tu imself.

Magozwe alifikiria kuhusu sehemu hii mpya, na kuhusu kwenda shule. Itakuwaje kama mjomba wake alikuwa sahihi kwamba alikuwa mjinga kiasi cha kutoweza kujifunza chochote? Itakuwaje kama watampiga sehemu hii mpya? Aliogopa. “Labda ni heri kuendelea kuishi mtaani,” aliwaza.


Im tel Tamas di tingz dem we im di fried a. Likl bai likl di man kanvins di bwaai pikni se laif kuda beta a di nyuu plies.

Alimshirikisha Thomas juu ya hofu aliyokuwa nayo. Baada ya muda Thomas alimhakikishia kwamba maisha yatakuwa bora huko sehemu mpya.


So Magozwe did muuv iihn a wahn ruum inna di ous wid di griin oustap. Im shier di ruum wid tuu ada bwaai pikni. In aal a did ten pikni a liv a di ous. Inkluudn anti Sisi an ar osban, chrii daag, wahn kyat, an wan uol guot.

Kwa hiyo Magozwe alihamia kwenye chumba katika nyumba yenye paa la kijani. Alikaa chumba kimoja na wavulana wengine wawili. Kwa ujumla kulikuwa na watoto kumi walioishi kwenye nyumba ile. Waliishi pamoja na Shangazi Cissy na mume wake, mbwa watatu, paka mmoja, na mbuzi aliyezeeka.


Magozwe did staat skuul an it di aad. Im did afi kech op. Somtaim im did waahn gi op. Bot im did tingk bout di pailat an di futbaala inna di stuoribuk dem. Laik dem, im neva gi op.

Magozwe alianza shule na ilikuwa ngumu. Alikuwa na mengi ya kujifunza. Mara nyingine alitaka kukata tamaa. Lakini aliwaza kuhusu rubani na mcheza mpira kwenye vitabu vya hadithi. Kama wao, hakukata tamaa.


Magozwe did a siddong inna di yaad a di ous wid di griin oustap, a riid wahn stuoribuk fram skuul. Tamas kom op an did siddong bisaid a im. “Wa da stuori ya bout?” Tamas aks im se. “A bout wahn bwaai pikni uu ton wahn tiicha,” Magozwe ansa se. “We di bwaai pikni niem?” Tamas aks se. “Im niem Magozwe,” Magozwe ansa wid a smail.

Magozwe alikuwa amekaa uani kwenye nyumba yenye paa la kijani, akisoma kitabu cha hadithi cha shule. Thomas alikuja na kukaa kando yake. “Hadithi inahusu nini?” Thomas akauliza. “Inahusu mvulana aliyekuja kuwa mwalimu,” Magozwe akajibu. “Jina lake ni nani?” akauliza Thomas. “Jina lake ni Magozwe,” Magozwe akasema kwa tabasamu.


Written by: Lesley Koyi
Illustrated by: Wiehan de Jager
Translated by: Georgette McGlashen
Language: Jamaican Creole
Level: Level 5
Source: Magozwe from African Storybook
Creative Commons License
This work is licensed under a Creative Commons Attribution 4.0 International License.
Read more level 5 stories:
Options
Back to stories list Download PDF