Download PDF
Back to stories list

Simbegwiere Simbegwire

Written by Rukia Nantale

Illustrated by Benjamin Mitchley

Translated by Georgette McGlashen

Language Jamaican Creole

Level Level 5

Narrate full story The audio for this story is currently not available.


Wen Simbegwiere mada did ded, shi did sad-sad. Simbegwiere faada did du im bes fi tek kier a im daata. Likl bai likl, dem lorn fi fiil api agen, wid out Simbegwiere mada. Evri maanin dem siddong an taak bout di die infronta dem. Evri iivlin dem mek dina tugeda. Afta dem wash di pliet dem, Simbegwiere faada elp ar wid ar uomwok.

Simbegwire alihuzunika mama yake alipofariki. Baba yake alijitahidi kumtunza mwanaye. Taratibu wakaanza kuwa wenye furaha tena, bila ya Mama Simbegwire. Kila asubuhi walikaa na kupanga mipango ya siku inayofuata. Kila jioni waliandaa chakula cha jioni pamoja. Baada ya kuosha vyombo, baba yake Simbegwire alimsaidia kufanya kazi zake za shule.


Wan die Simbegwiere faada kom uom lieta dan yuuzhal. “We yu de mi pikni?” im kaal. Simbegwiere ron go to ar faada. Shi stap wan plies wen shi si se ar faada did a uol aan pan wahn uman an. “Mi waahn yu fi miit sumadi speshal, mi pikni. Dis a Aniita,” im se a smail.

Siku moja baba yake Simbegwire alirudi nyumbani kwa kuchelewa. “Mwanangu uko wapi?” aliita. Simbegwire alimkimbilia baba yake. Alisimama ghafla baada ya kumwona baba yake akiwa ameshika mkono wa mwanamke. “Nataka ukutane na mtu muhimu, mwanangu. Huyu ni Anita,” alisema huku akitabasamu.


“Eluo Simbegwiere, yu faada tel mi uol iip bout yu,” Aniita se. Bot shi neva smail ar tek di pikni an. Simbegwiere faada did api an fiil gud bout we apm. Im did a taak bout di chrii a dem a liv tugeda, an ou gud dem laif wuda bi. “Mi pikni, mi uop yu wi tek Aniita fi yu mada,” im se.

“Hujambo Simbegwire? Baba yako amenisimulia mengi kukuhusu,” alisema Anita. Lakini hakutabasamu wala kumpa Simbegwire mkono. Baba yake Simbegwire alijaa na furaha. Aliongelea jinsi maisha yatakavyokuwa mazuri watatu hao wakiishi pamoja. “Mwanangu, ni matumaini yangu kuwa utamkubali Anita kuwa mama yako,” alisema.


Simbegwiere laif chienj. Shi neva av no muor taim fi siddong wid ar faada inna di maanin dem. Aniita did gi ar so moch ous wok fi du dat shi did tuu taiyad fi du ar skuul wok inna di iivlin. Shi go schriet a ar bed afta dina. Ar ongl komfat a did di priti-priti blangkit we ar mada did gi ar. Simbegwiere faada neva siim fi nuotis se im daata did sad.

Maisha ya Simbegwire yakabadilika. Hakuwa na muda tena wa kukaa na baba yake asubuhi. Anita alimpa kazi nyingi za nyumbani zilizomchosha sana kiasi cha kushindwa kufanya kazi zake za shuleni jioni. Alikuwa anaenda moja kwa moja kulala baada ya chakula cha jioni. Faraja pekee aliyokuwa nayo ni blanketi lenye rangi nyingi alilopewa na mama yake. Baba yake Simbegwire hakugundua kwamba binti yake alikuwa hana furaha.


Afta a kopl monts, Simbegwiere faada did tel dem se im wuda gaan we fram uom fi a wail. “Mi jab mek mi afi chravl,” im se. “Bot mi nuo se yu wi luk afta unu wananeda.” Simbegwiere fies did jrap, bot ar faada neva nuotis. Aniita neva se notn. Shi neva api naida.

Baada ya miezi michache, baba yake Simbegwire aliwaambia kwamba ana mpango wa kusafiri. “Itanibidi nisafiri kikazi,” alisema. “Lakini najua hakutakuwa na tatizo.” Uso wa Simbegwire ulijawa huzuni, lakini baba yake hakugundua. Anita hakusema lolote. Hakuwa na furaha.


Tingz get wors fi Simbegwiere. Ef shi neva don ar ous wok, ar shi komplien, Aniita lik ar. An wen a dina taim, di uman nyam muos a di fuud, an lef likl bit fi Simbegwiere. Evri nait Simbegwiere baal til shi jrap asliip, a og op ar mada blangkit.

Mambo yakawa mabaya kwa Simbegwire. Aliposhindwa kumaliza kazi au alipolalamika, Anita alimpiga. Wakati wa chakula cha jioni Anita alikula chakula kingi, na kumwachia Simbegwire makombo. Kila usiku Simbegwire alikuwa analia, huku akilikumbatia blanketi la mama yake.


Wan maanin, Simbegwiere did wiek op liet. “Yu liezi gyal pikni!” Aniita baal out. Shi jrag Simbegwiere aaf a di bed. Di speshal blangkit kech pan wahn niel, an tier inna tuu.

Asubuhi moja, Simbegwire alichelewa kuamka. “Wewe mtoto mvivu,” Anita aliita kwa kelele. Akamvuta Simbegwire kutoka kitandani. Blanketi lake zuri likanasa kwenye msumari na kuchanika vipande viwili.


Simbegwiere did wel opset. Shi mek op ar main fi ron we fram uom. Shi did tek di piisiz dem fram ar mada blangkit, pak op som fuud, an lef di ous. Shi tek di ruod we ar faada di tek.

Simbegwire alikasirika sana. Akaamua kutoroka nyumbani. Akachukua vipande vya blanketi la mama yake. Akachukua na chakula na akaondoka nyumbani. Akaifuata barabara aliyopita baba yake.


Wen iivlin kom, shi klaim go op inna wahn taal chrii nier wahn riva an mek a bed fi arself inna di lim dem. Az shi a jrap asliip, si did a sing: “Maama, maama, maama yu lef mi. Yu lef mi an neva kom bak. Papa no lov mi no muor. Mama, wen yu ago kom bak? Yu lef me.”

Ilipofika jioni alipanda mti mrefu karibu na kijito na akaandaa kitanda kwenye matawi ya mti. Alipokuwa analala akaimba “Maama, maama, maama, umeniacha. Umeniacha na haukurudi tena. Baba hanipendi tena. Mama unarudi lini? Uliniacha.”


Di neks maanin Simbegwiere did a sing di sang agen. Wen di uman dem did kom wash dem kluoz dem a di riva, dem did ier di sad sang a kom fram di taal chrii. Dem did tingk se a did onggl di briiz a bluo di liif dem, an did gwaan du dem wok. Bot wan a dem lisn gud-gud tu di sang.

Asubuhi iliyofuata, Simbegwire aliimba ule wimbo tena. Wakina mama walipokuja kufua nguo zao walisikia wimbo wa huzuni kutoka kwenye mti mrefu. Wakafikiri ni upepo unatikisa matawi ya mti na wakaendelea na kazi zao. Lakini mama mmoja akasikiliza ule wimbo kwa makini.


Di uman did luk op inna di chrii. Wen shi si di gyal pikni an di piisiz a di priti-priti blangkit, shi baal, “Simbegwiere, mi breda pikni!” Di ada uman dem stap wash an elp Simbegwiere fi klaim dong outta di chrii. Ar anti og op di likl gyal pikni an chrai fi komfat ar.

Mama huyo akaangalia juu ya mti. Alipomwona msichana na vipande vya blanketi la rangi, akalia, “Simbegwire, mtoto wa kaka yangu!” Wakina mama wengine wakaacha kufua na wakamsaidia Simbegwire kushuka toka juu ya mti. Shangazi yake akamkumbatia na kumfariji.


Simbegwiere anti tek di pikni go a fi ar yaad. Shi did gi Simbegwiere waam fuud, an put ar fi sliip inna wan bed wid ar mada blangkit. Da nait de, Simbegwiere baal az shi a jrap asliip. Bot a did yai-waata kaaz shi fiil riliif. Shi nuo se dat ar anti wud a luk afta ar.

Shangazi yake Simbegwire akampeleka nyumbani kwake. Akampatia chakula, akampeleka kitandani na akamfunika na blanketi la mama yake. Usiku ule Simbegwire akalia alipokwenda kulala. Lakini yalikuwa machozi ya furaha. Alijua shangazi yake atamtunza.


Wen Simbegwiere faada kom bak uom, im fain ar ruum emti. “A wa apm, Aniita?” im se wid a evi aat. Di uman tel im se Simbegwiere did ron we. “Mi did waahn ar fi rispek me,” shi se. “Bot miebi mi did tuu schrik pan ar.” Simbegwiere faada lef di ous an go inna di direkshan a di riva. Im kantinyuu go schriet a im sista vilij fi fain out ef shi did si Simbegwiere.

Baba yake Simbegwire aliporudi nyumbani, alikikuta chumba chake kikiwa tupu. “Nini kimetokea, Anita?” aliuliza kwa simanzi. Anita akaelezea kuwa Simbegwire alitoroka. “Nilitaka aniheshimu,” alisema. “Labda nilikuwa mkali sana.” Baba yake Simbegwire aliondoka nyumbani na akaelekea kwenye kijito. Akaenda kwenye kijiji cha dada yake kuuliza kama amemwona Simbegwire.


Simbegwiere did a ramp wid ar kozn dem wen shi did si ar faada fram wie out. Shi did fried im mait a beks, so shi ron go inna di ous fi aid. Bot ar faada go tu ar se, “Simbegwiere, yu fain di porfek mada fi yuself. Wan uu lov yu an andastan yu. Mi proud a yu an mi lov yu.” Dem agrii se Simbegwiere wud a stie wid ar anti fi az lang az shi waahn.

Simbegwire alikuwa anacheza na binamu zake alipomwona baba yake akija kwa mbali. Aliogopa kuwa baba yake angekuwa amekasirika, na akakimbilia ndani ya nyumba ili ajifiche. Baba yake alimwendea na akamwambia, “Simbegwire umempata mama mzuri. Anayekupenda na kukuelewa. Najivunia kuwa nawe na ninakupenda.” Walikubaliana kuwa Simbegwire angeishi na shangazi yake kwa muda wote atakaotaka.


Ar faada go luk fi ar evridie. Ivenshali, im did kom wid Aniita. Shi uol aan pan Simbegwiere an, “Mi sari-sari likl wan, mi did rang,” shi baal se. “Yu wi mek mi chrai agen?” Simbegwiere luk pan ar faada an im fies did luk kansorn. Den shi tek taim waak tuwaadz Aniita an og ar op.

Baba yake alikuwa akimtembelea kila siku. Mwishoe akaja na Anita. Akampa mkono Simbegwire. “Nisamehe, nilikosea,” akalia. “Utanipa nafasi kujaribu tena?” Simbegwire alimwangalia baba yake aliyekuwa na uso wa wasiwasi. Baadaye akamwendea Anita taratibu na akamkumbatia.


Di neks wiik, Aniita aks Simbegwiere an ar kozn dem an anti, fi kom a di yaad fi it fuud. Wat a fiis! Aniita mek aal a Simbegwiere fievarit fuud dem, an evribadi nyam so til dem beli ful. Den di pikni dem ramp miinwail di big piipl dem did a taak. Simbegwiere did fiil api an briev. Shi mek op ar main se suuhn-suuhn, shi wuda go bak uom fi liv wid ar faada an ar stepmada.

Wiki iliyofuata, Anita aliwaalika Simbegwire, binamu zake, na shangazi yake kwa ajili ya chakula. Anita akaandaa vyakula vyote ambavyo Simbegwire anavipenda, na kila mmoja akala hadi akashiba. Baada ya kula watoto wakaenda kucheza huku watu wazima wakiongea. Simbegwire akajisikia furaha na jasiri. Akaamua kuwa si muda mrefu atarejea nyumbani kuishi na baba yake na mama yake wa kambo.


Written by: Rukia Nantale
Illustrated by: Benjamin Mitchley
Translated by: Georgette McGlashen
Language: Jamaican Creole
Level: Level 5
Source: Simbegwire from African Storybook
Creative Commons License
This work is licensed under a Creative Commons Attribution 3.0 International License.
Read more level 5 stories:
Options
Back to stories list Download PDF