Download PDF
Back to stories list

La canzone di Sakima Wimbo wa Sakima

Written by Ursula Nafula

Illustrated by Peris Wachuka

Translated by Laura Pighini

Read by Sonia Pighini

Language Italian

Level Level 3

Narrate full story

Reading speed

Autoplay story


Sakima viveva con i suoi genitori e sua sorella di quattro anni. Vivevano nella terra di un uomo molto ricco. La loro capanna di fieno era alla fine di una fila d’alberi.

Sakima aliishi na wazazi wake na dada yake wa miaka minne. Waliishi katika shamba la mtu tajiri. Nyumba yao ya nyasi ilikuwa mwisho wa safu ya miti iliyopendeza.


Quando Sakima aveva tre anni, si ammalò e perse la vista. Sakima era un ragazzo pieno di talento.

Sakima alipokuwa na umri wa miaka mitatu, aliugua na kupoteza uwezo wa kuona. Hata hivyo, Sakima alikuwa mvulana mwenye kipaji.


Sakima faceva tante cose che gli altri bambini di sei anni non facevano. Per esempio, lui poteva sedersi con i membri più anziani del villaggio e discutere questioni importanti.

Sakima alitenda mambo mengi ambayo wavulana wengine wa umri wake hawakufanya. Kwa mfano, aliketi na watu wazima na kujadili mambo muhimu.


I genitori di Sakima lavoravano nella casa dell’uomo ricco. Uscivano di casa la mattina presto e tornavano la sera tardi. Sakima veniva lasciato con la sorellina piccola.

Wazazi wa Sakima walifanya kazi katika nyumba ya yule tajiri. Walitoka nyumbani asubuhi na mapema na kurudi jioni. Sakima aliachwa na dada yake.


Sakima amava cantare canzoni. Un giorno sua madre gli chiese: “Dove impari queste canzoni Sakima?”

Sakima alipenda kuimba nyimbo. Siku moja mama yake alimuuliza, “Sakima, unajifunza nyimbo hizi kutoka wapi?”


Sakima rispose “Mi vengono e basta madre. Le sento nella mia testa e poi le canto.”

Sakima alimjibu, “Nazisikia akilini mwangu kisha naziimba.”


A Sakima piaceva cantare per la sua sorellina, specialmente se lei aveva fame. Sua sorella lo ascoltava cantare la sua canzone preferita. Ondeggiava alla calmante sinfonia.

Sakima alipenda kumwimbia mdogo wake hasa akihisi njaa. Dada yake alimsikiliza na kucheza.


“Puoi cantare ancora e ancora Sakima?” Sua sorella lo pregava. Sakima accettava e la cantava e ricantava.

“Naomba uimbe tena na tena, Sakima,” mdogo wake alimsihi. Sakima alikubali na kuimba mara nyingine.


Una sera, Quando i suoi genitori tornarono a casa, erano molto silenziosi. Sakima sapeva che c’era qualcosa che non andava.

Jioni moja, wazazi wake waliporudi nyumbani, walikuwa kimya sana. Sakima alijua kwamba lazima kulikuwa na jambo baya.


“Cosa succede, Mamma, Papà?” Chiese Sakima. Sakima scoprì che il figlio dell’uomo ricco era scomparso. L’uomo era molto triste e solo.

“Kuna shida gani, mama, baba?” Sakima aliuliza. Sakima aligundua kwamba mwana wa tajiri wao alikuwa amepotea. Tajiri alihuzunika na kuwa na upweke mkubwa.


“Io posso cantare per lui, potrebbe renderlo felice di nuovo,” disse Sakima ai suoi genitori. Ma i suoi genitori lo destituirono. “Lui è molto ricco, tu sei solo un ragazzo cieco. Pensi che la tua canzone lo aiuterà?”

“Labda atafurahi tena nikimwimbia,” Sakima aliwaambia wazazi wake. Wazazi wake walidharau wazo lake. “Yeye ni tajiri sana. Wewe ni mvulana asiyeona. Unadhani wimbo wako utamsaidia?”


Tuttavia, Sakima non si arrese. La sua sorellina lo appoggiò. Disse “Le canzoni di Sakima mi calmano quando sono affamata. Calmeranno anche l’uomo ricco.”

Hata hivyo, Sakima hakukata tamaa. Mdogo wake alimpa moyo. Alisema, “Nyimbo za Sakima hunituliza mimi nikiwa na njaa. Zitamtuliza tajiri vile vile.”


Il giorno seguente, Sakima chiese alla sorellina di accompagnarlo alla casa dell’uomo ricco.

Siku iliyofuata, Sakima alimwomba mdogo wake amwongoze hadi kwenye nyumba ya tajiri.


Si fermò sotto una grande finestra e cominciò a cantare la sua canzone preferita. Lentamente, la testa dell’uomo ricco cominciò a mostrarsi attraverso la finestra.

Alisimama chini ya dirisha moja kubwa na kuanza kuimba wimbo wake alioupenda. Pole pole, kichwa cha tajiri kilionekana dirishani.


I lavoratori smisero di fare quello che stavano facendo e ascoltarono la bellissima canzone di Sakima. Ma un uomo disse “Nessuno è stato in grado di consolare il capo. Questo ragazzo cieco pensa di potercela fare?”

Wafanyakazi waliacha kazi zao. Wakasikiliza wimbo mzuri wa Sakima. Hata hivyo, mwanamume mmoja alisema, “Hakuna aliyefaulu kumtuliza bwana. Je, huyu mvulana asiyeona anafikiri atamtuliza?”


Sakima finì di cantare la sua canzone e si girò per andarsene. Ma l’uomo ricco uscì fuori di corsa e disse “Per favore, canta ancora.”

Sakima alipomaliza kuimba wimbo wake alianza kuondoka. Tajiri alitoka nje kwa haraka na kusema, “Tafadhali, imba tena.”


In quell’esatto momento, due uomini arrivarono portando qualcuno su una barella. Avevano trovato il figlio dell’uomo ricco, era stato picchiato e lasciato sul ciglio della strada.

Wakati huo huo, watu wawili walikuja wakiwa wamembeba mtu kwenye machela. Walimkuta mwana wa tajiri akiwa amechapwa na kuachwa kando ya barabara.


L’uomo ricco fu felicissimo di rivedere suo figlio. Ricompensò Sakima per averlo consolato. Portò suo figlio e Sakima in ospedale, così che potessero curare la sua vista.

Tajiri alifurahi sana kumwona mwana wake tena. Alimzawadia Sakima kwa kumliwaza. Aliwapeleka mwanawe na Sakima hosipitali ili Sakima aweze kusaidiwa kuona tena.


Written by: Ursula Nafula
Illustrated by: Peris Wachuka
Translated by: Laura Pighini
Read by: Sonia Pighini
Language: Italian
Level: Level 3
Source: Sakima's song from African Storybook
Creative Commons License
This work is licensed under a Creative Commons Attribution 4.0 International License.
Options
Back to stories list Download PDF