Download PDF
Back to stories list

Bimbo asino Mtoto Punda

Written by Lindiwe Matshikiza

Illustrated by Meghan Judge

Translated by Laura Pighini

Read by Sonia Pighini

Language Italian

Level Level 3

Narrate full story

Reading speed

Autoplay story


Fu una piccola bimba a vedere per prima la misteriosa figura in lontananza.

Ilikuwa ni msichana mdogo aliyekuwa wa kwanza kuona umbo la ajabu kwa mbali.


Man mano che la figura si avvicinava, vide che si trattava di una donna molto incinta.

Kadiri umbo lilipokaribia, aliona kwamba lilikuwa ni mwanamke mwenye ujauzito mkubwa.


Timida ma coraggiosa, la bimba si avvicinò alla donna. “Dobbiamo tenerla con noi,” decise la gente della piccola bimba. “Terremo lei e il suo bimbo al sicuro.”

Kwa upole na ujasiri, msichana alimsogelea mwanamke yule. “Lazima tumhifadhi,” watu wa msichana yule walisema. “Tutawaweka yeye na mtoto wake salama.”


Il bimbo stava arrivando. “Spingi!” “Portate delle coperte!” “Acqua!” “SPINGIIIIII!!”

Mtoto alikuwa njiani kuzaliwa si muda mrefu. “Sukuma!” “Leteni mablanketi!” “Maji!” “Suuukuuumaaaa!!!”


Ma quando videro il bimbo tutti fecero un salto indietro scioccati. “Un asino?!?”

Lakini walipomwona mtoto, wote waliruka kwa mshtuko. “Punda?!”


Tutti cominciarono a discutere. “Avevamo detto che li avremmo tenuti al sicuro e questo è quello che faremo!” Dissero alcuni. “Ma ci porteranno sfortuna!” Dissero altri.

Wakaanza kubishana. “Tulisema tutawaweka mama na mtoto salama, na hivyo ndivyo tutakavyofanya,” baadhi wakasema. “Lakini watatuletea mkosi!” wengine wakadai.


Al che, la donna si ritrovò da sola di nuovo. Si chiese cosa fare con questo strano bimbo. Si chiese cosa fare con se stessa.

Kwa hiyo mwanamke yule alijikuta yuko peke yake kwa mara nyingine tena. Akajiuliza atafanya nini na mtoto huyo wa ajabu. Akajiuliza atafanya nini na yeye mwenyewe.


Ma alla fine dovette accettare che quello era suo figlio e che lei era sua madre.

Lakini hatimaye alikubali kwamba huyo ni mwanaye na yeye ni mama yake.


Ora, se il bimbo fosse rimasto di quella stessa piccola taglia, tutto sarebbe stato diverso. Ma il bimbo asino crebbe e crebbe finché non poté più stare sulle spalle della mamma. E per quanto lei ci provasse, non poteva comportarsi come un essere umano. Sua madre era spesso stanca e frustrata. A volte gli faceva fare lavori da bestia.

Endapo mtoto huyo angebaki kuwa vilevile, na umbo dogo, labda kila kitu kingekuwa tofauti. Lakini mtoto Punda aliendelea kukua na kukua mpaka hakuweza kutoshea tena mgongoni mwa mama yake. Pamoja na kujaribu kwa bidii, hakuweza kuwa na tabia za kibinadamu. Mara nyingi mama yake alichoka na kuvunjika moyo. Wakati mwingine alimlazimisha kufanya kazi walizostahili wanyama.


Confusione e rabbia crebbero dentro Asino. Non poteva fare questo, non poteva fare quello. Non poteva essere così e non poteva essere cosà. Un giorno si arrabbiò così tanto che scalciò al suolo sua madre.

Kuchanganyikiwa na hasira vilianza kujengeka ndani mwa Punda. Alishindwa kufanya hivi wala vile. Alishindwa kuwa hivi wala vile. Alipatwa na hasira sana kiasi kwamba, siku moja, alimpiga teke mama yake mpaka akaanguka chini.


Asino si vergognò. Cominciò a correre via il più veloce e lontano che poté.

Punda alijawa na aibu. Akaanza kukimbilia mbali kwa haraka kadiri awezavyo.


Quando smise di correre, era notte e Asino si era perso. “Hi-ho?” ragliò nell’oscurità. “Hi-ho?” rispose l’eco. Era da solo. Acciambellatosi su se stesso si addormentò in un sonno profondo e tormentato.

Wakati aliposimama, ilikuwa ni usiku, na alikuwa amepotea. “Hii hoo?” alinong’ona gizani. “Hii hoo?” giza likatoa mwangwi. Alikuwa mwenyewe. Alijikunyata katika umbo dogo, akalala fofofo usingizi wa mang’amung’amu.


Asino si sveglio trovando uno strano vecchio a osservarlo. Asino lo guardò negli occhi e cominciò a sentire un barlume di speranza.

Punda aliamka na kumkuta mzee mmoja wa ajabu akimtazama. Akamwangalia mzee yule machoni na akaanza kuhisi ishara ya matumaini.


Asino andò a vivere con il vecchio che gli insegnò tanti modi diversi per sopravvivere. Asino ascoltava e imparava e lo stesso valeva per il vecchio. Si aiutavano vicenda e ridevano insieme.

Punda alienda kuishi na mzee yule, na mzee alimfundisha mbinu nyingi za kuishi. Punda alisikiliza na kujifunza, na mzee vivyo hivyo pia. Walisaidiana na kucheka pamoja.


Una mattina, il vecchio chiese a Asino di portarlo in cima ad una montagna.

Asubuhi moja, mzee alimwomba Punda ambebe hadi kwenye kilele cha mlima.


Al di sopra delle nuvole si addormentarono. Asino sognò che sua madre era ammalata e lo chiamava. E quando si svegliò..

Walipofika juu kwenye mawingu, walipatwa na usingizi. Punda akaota kuwa mama yake alikuwa mgonjwa na alimhitaji. Na alipoamka…


…Le nuvole erano sparite insieme al suo amico, il vecchio.

…mawingu yalikuwa yametoweka pamoja na rafiki yake, yule mzee.


Asino finalmente capì cosa doveva fare.

Hatimaye, Punda alijua alichotakiwa kufanya.


Asino trovò sua madre, da sola che piangeva la scomparsa di suo figlio. Si fissarono a vicenda a lungo. E poi si abbracciarono molto forte.

Punda alimkuta mama yake akiwa peke yake huku akimwomboleza mwanaye aliyepotea. Wakaangaliana kwa muda mrefu. Na kisha wakakumbatiana kwa hisia.


Il bambino asino e sua madre crebbero insieme e trovarono tanti modi per vivere l’uno affianco all’altro. Lentamente, intorno a loro, altre famiglie cominciarono a sistemarsi.

Mtoto Punda na mama yake wamekuwa kitu kimoja na kuishi kwa ushirikiano. Taratibu, familia nyingine zimeanza kuhamia na kuishi miongoni mwao.


Written by: Lindiwe Matshikiza
Illustrated by: Meghan Judge
Translated by: Laura Pighini
Read by: Sonia Pighini
Language: Italian
Level: Level 3
Source: Donkey Child from African Storybook
Creative Commons License
This work is licensed under a Creative Commons Attribution 4.0 International License.
Options
Back to stories list Download PDF