Download PDF
Back to stories list

दादी माँ के केले Ndizi za bibi

Written by Ursula Nafula

Illustrated by Catherine Groenewald

Translated by Nandani

Language Hindi

Level Level 4

Narrate full story The audio for this story is currently not available.


दादी माँ का बगीचा बहुत सुंदर था और ज्वार, बाजरा और कसावा से भरा हुआ था। पर उनमें से सबसे अच्छे केले थे। ऐसे तो दादी माँ के बहुत सारे नाती-पोते थे, पर यह राज़ मुझे ही पता था कि मैं उनकी सबसे ज़्यादा लाडली हूँ। वह कई बार मुझे अपने घर बुलातीं। वे मुझे अपने छोटे-छोटे राज़ भी बतातीं। लेकिन एक राज़ जो वह मुझे से नहीं बताती थीं, वह यह था कि वह केले कहाँ पकाती हैं।

Bibi alikuwa na bustani nzuri iliyojaa mtama, ulezi na mihogo. Lakini kati ya mazao yote, alipenda zaidi ndizi. Japo bibi alikuwa na wajukuu wengi, nilikuja kubaini kuwa alikuwa ananipenda mimi zaidi ya wote. Mara nyingi alikuwa akinialika nyumbani kwake. Pia alikuwa ananiambia siri ndogo ndogo. Lakini kulikuwa na siri moja ambayo hakunishirikisha: alipokuwa anavundika ndizi.


एक दिन मैंने देखा कि दादी माँ के घर के बाहर धूप में घास से बनी टोकरी रखी हुई है। जब मैंने उनसे ये पूछा ये किसलिए है तो मुझे बस इतना ही उत्तर मिला की “यह मेरी जादुई टोकरी है।” टोकरी के बगल में बहुत सारे केले के पत्ते थे जिन्हें दादी माँ समय-समय पर पलटती रहती थीं। मैं जानना चाहती थी कि “दादी माँ के ये पत्ते किस लिए हैं?” जब मैंने यह पूछा तो उन्होंने मुझे केवल ये बताया कि “ये जादुई पत्ते हैं।”

Siku moja niliona tenga kubwa limeanikwa juani nje ya nyumba ya bibi. Nilipouliza lilikuwa la nini, jibu pekee nililopata lilikuwa, “Hilo ni tenga langu la maajabu.” Pembeni mwa tenga lile kulikuwa na majani ya ndizi ambayo bibi alikuwa akiyageuza kila mara. Nilipatwa na shauku. “Bibi, hayo majani ni ya nini?” niliuliza. Jibu pekee nililopata lilikuwa, “Ni majani yangu ya maajabu.”


दादी माँ के केलों, केले के पत्तों और उस बड़ी सी घास की टोकरी को देखना बड़ा ही मज़ेदार था। उन्होंने किसी ज़रूरी काम से मुझे मेरी माँ के पास भेज दिया। मैंने कहा “दादी माँ आप जो बना रही हैं मुझे देखने दीजिए न…” “बच्ची, ज़िद मत करो, जो कहा गया है वह करो,” उन्होंने चेताया। मैं भाग गई।

Nilikuwa na shauku kubwa kumwangalia bibi, ndizi, majani ya ndizi na tenga kubwa. Lakini bibi alinituma kwenda kwa mama. “Bibi, tafadhali naomba nitazame unavyoandaa…” “Usiwe msumbufu, fanya ulichoambiwa,” alisisitiza. Nikaondoka nikikimbia.


जब मैं लौटी, दादी माँ बाहर बैठी थीं पर वहाँ न तो केले थे और न ही उसके पत्ते। “दादी माँ, टोकरी और सारे केले कहाँ हैं, और … कहा, “लेकिन मुझे एक ही उत्तर मिला कि “वे सब मेरे जादुई स्थान पर हैं।” यह सुनकर मुझे बहुत निराशा हुई!

Niliporudi, bibi alikuwa amekaa nje, ila hakukuwa na tenga wala ndizi. “Bibi, tenga liko wapi, zile ndizi ziko wapi, na…” Jibu pekee nililopata lilikuwa, “Zipo kwenye eneo la maajabu.” Ilikuwa inasikitisha.


दो दिन बाद, दादी माँ ने मुझे अपनी छड़ी लाने के लिए अपने कमरे में भेजा। जैसे ही मैंने दरवाज़ा खोला वैसे ही पके केलों की मीठी सुगंध से मेरा मन खुश हो गया। अंदर के कमरे में दादी माँ की बड़ी सी घास की जादुई टोकरी थी। उसे पुराने कंबल से अच्छी तरह छुपाया गया था। मैंने उसे हटाया और मुझे एक लाजवाब खुशबू आई।

Siku mbili baadaye, bibi alinituma kwenda chumbani kwake kumletea mkongojo. Mara tu baada ya kufungua mlango, nilikaribishwa na harufu kali ya ndizi mbivu. Pembeni mwa chumba kulikuwa na tenga kubwa la maajabu la bibi. Lilikuwa limefichwa na blanketi la zamani. Nikaliinua na kunusa ile harufi nzuri.


दादी माँ की आवाज़ सुनकर मैं चौंक गई “तुम क्या कर रही हो? जल्दी से मेरी छड़ी लाओ।” मैं जल्दी से उनकी छड़ी लेकर आ गई। “तुम किसलिए मुस्कुरा रही हो?” दादी माँ ने पूछा। जब उन्होंने यह पूछा तब मुझे एहसास हुआ कि मैं अभी भी उनके जादुई स्थान का पता लगने पर मुस्कुरा रही थी।

Sauti ya bibi ilinishtua alipoita, “Unafanya nini? Fanya haraka niletee mkongojo.” Nikaharakisha kwenda nje na mkongojo wake. “Unatabasamu nini?” bibi aliuliza. Swali lake likanifanya nigundue kuwa kumbe bado nilikuwa ninatabasamu baada ya kugundua eneo lake la maajabu.


अगले दिन जब वे मेरी माँ के पास आईं, तो मैं एक बार फिर केलों को देखने के लिए उनके घर भागी। वहाँ पर बहुत सारे पके केले थे। मैंने एक उठाया और उसे अपने कपड़ों में छिपा लिया। टोकरी को ढँकने के बाद मैं घर के पीछे गई और जल्दी से उसे खा लिया। यह उन सभी केलों से ज़्यादा मीठा था जो अब तक मैंने खाए थे।

Siku iliyofuata bibi alipokuja kumtembelea mama yangu, nikakimbilia nyumbani kwake kuangalia ndizi tena. Kulikuwa na vichane vya ndizi zilizoiva. Nikachukua ndizi moja na kuificha kwenye nguo yangu. Baada ya kufunika tenga tena, nikaenda nyuma ya nyumba na harakaharaka nikaila. Ilikuwa ni ndizi tamu ambayo sijawahi kula kamwe.


उसी दिन, जब दादी माँ बगीचे से सब्ज़ियाँ तोड़ रही थीं, मैं केलों की ओर झाँककर उनकी आँख बचाकर केलों की चोरी की। सभी केले लगभग पक चुके थे। मैं चार से ज़्यादा केले नहीं ले पाई। जैसे ही मैं दबे पाँव दरवाजे की तरफ़ बढ़ी, मैंने बाहर दादी माँ को खाँसते हुए सुना। मैंने जल्दी से केलों को कपड़ों के अंदर छिपाया और उनसे बचकर निकल गई।

Siku iliyofuata, bibi alipokuwa bustanini akichuma mboga, nikanyemelea ndani kuchungulia ndizi. Karibu zote zilikuwa zimeiva. Nikashindwa kujizuia nikachukua kichane cha ndizi nne. Nilipokuwa nanyata kuelekea mlangoni, nikamsikia bibi akikohoa nje. Nilifanikiwa kuzificha ndizi ndani ya nguo yangu na tukapishana bila ya kugundua.


अगले दिन बाज़ार था। दादी माँ जल्दी उठीं। वे हमेशा पके केले और कसावा को बाज़ार बेचने जाती थीं। मुझे उस दिन उनके घर जाने की जल्दी नहीं थी। लेकिन मैं उनसे ज़्यादा दिन दूर नहीं रह सकी।

Siku iliyofuata ilikuwa siku ya gulio. Bibi aliamka asubuhi sana. Huwa anapeleka ndizi mbivu na mihogo kuuza gulioni. Siku hiyo sikuwa na haraka kwenda kumsalimia. Ila sikuweza kumkwepa kwa muda mrefu.


उस शाम को मुझे मेरी माँ, पिता और दादी माँ ने बुलाया। मुझे पता था क्यों। उस ही रात जब मैं सोने के लिए लेटी, मैंने फैसला किया कि अब मैं कभी भी दादी माँ, अपने माता-पिता और किसी और की चोरी नहीं करूँगी।

Jioni ile niliitwa na mama, baba na bibi. Nilijua kwanini. Usiku ule nilipokwenda kulala, nilijua siwezi kuiba tena. Siwezi kumwibia bibi, wazazi wangu na mtu yeyote yule.


Written by: Ursula Nafula
Illustrated by: Catherine Groenewald
Translated by: Nandani
Language: Hindi
Level: Level 4
Source: Grandma's bananas from African Storybook
Creative Commons License
This work is licensed under a Creative Commons Attribution 3.0 International License.
Options
Back to stories list Download PDF