Download PDF
Back to stories list

वुसी की बहन ने क्या कहा Alichokisema dada yake Vusi

Written by Nina Orange

Illustrated by Wiehan de Jager

Translated by Nandani

Language Hindi

Level Level 4

Narrate full story The audio for this story is currently not available.


एक दिन सुबह सुबह वुसी की दादी ने उसे बुलाया, “वुसी, कृपया इन अंडों को अपने माता-पिता के पास ले जाओ। वे तुम्हारी बहन की शादी के लिए एक बड़ा सा केक बनाना चाहते हैं।”

Siku moja asubuhi bibi yake Vusi alimwita na kumwambia, “Tafadhali peleka yai hili kwa wazazi wako. Wanataka kutengeneza keki kubwa kwa ajili ya harusi ya dada yako.”


माता-पिता के पास जाते समय रास्ते में, वुसी फल बटोरने वाले दो लड़कों से मिला। एक लड़के ने वुसी से अंडा छीना और उसे पेड़ पर फेंक दिया। अंडा टूट गया।

Alipokuwa njiani kuelekea kwa wazazi wake, Vusi akakutana na vijana wawili wanaokota matunda. Kijana mmoja akanyakua yai kutoka kwa Vusi na akalirusha kwenye mti. Yai likavunjika.


वुसी ने रोते हुए कहा “ये तुमने क्या किया?” “वे अंडे केक के लिए थे। वह केक मेरी बहन की शादी के लिए था। अगर मेरी बहन को शादी का केक नहीं मिल पाया तो वह क्या कहेगी?”

“Umefanya nini?” Vusi akalia. “Yai lile lilikuwa kwa ajili ya keki. Keki ilikuwa kwa ajili ya harusi ya dada yangu. Dada yangu atasemaje kama hakutakuwa na keki ya harusi?”


लड़के वुसी को परेशान करने के लिए शर्मिंदा थे। “हम केक का तो कुछ नहीं नहीं कर सकते, लेकिन अपनी बहन के लिए एक चलने वाली छड़ी तुम ले जाओ,” एक ने कहा। वुसी ने अपना सफ़र जारी रखा।

Vijana wale waliomba msamaha kwa kumchokoza Vusi. “Hatuna la kufanya kuhusu keki, lakini hii hapa ni fimbo kwa ajili ya dada yako,” mmoja alisema. Vusi akaendelea na safari yake.


रास्ते में वह दो आदमियों से मिला जो घर बना रहे थे। उनमें से एक ने पूछा “क्या हम उस मजबूत छड़ी का प्रयोग कर सकते हैं?” पर वह छड़ी मकान के लिए मजबूत नहीं थी, और वह टूट गई।

Njiani alikutana na wanaume wawili wakijenga nyumba. “Tunaweza kutumia hiyo fimbo imara?” mmoja akaomba. Lakini fimbo haikuwa imara kwa kujengea, na ikavunjika.


“यह तुमने क्या किया?” वुसी रोया। “यह छड़ी मेरी बहन के लिए उपहार था। इसे फलवालों ने मेरी बहन को दिया था क्योंकि उन्होंने उसके केक के लिए अंडे तोड़ दिए थे। केक मेरी बहन की शादी के लिए था। अब न अंडा है, न केक, और नहीं ही कोई उपहार। मेरी बहन क्या कहेगी?”

“Mmefanya nini?” Vusi akalia. “Fimbo hii ilikuwa zawadi kwa ajili ya dada yangu. Waangua matunda walinipa fimbo hiyo kwa sababu walivunja yai la keki. Keki ilikuwa ni kwa ajili ya harusi ya dada yangu. Sasa hakuna yai, hakuna keki, na hakuna zawadi. Dada yangu atasemaje?”


मजदूर छड़ी तोड़ने पर दुखी थे। उनमें से एक ने कहा “हम केक का तो कुछ नहीं कर सकते, पर तुम्हारी बहन के लिए हमारे पास कुछ भूसा है, ले जाओ “। और फिर वुसी ने अपना सफ़र जारी रखा।

Wajenzi waliomba msamaha kwa kuvunja fimbo. “Hatuna la kufanya kuhusu keki, lakini tutakupa makuti umpelekee dada yako,” mmoja alisema. Na Vusi akaendelea na safari yake.


रास्ते में, वुसी किसान और एक गाय से मिला। “क्या स्वादिष्ट भूसा है, क्या इसे मैं थोड़ा सा खा सकती हूँ?” गाय ने पूछा। पर भूसा इतना स्वादिष्ट था कि गाय ने उसे पूरा ही खा लिया!

Njiani, Vusi akakutana na mkulima akiwa na ng’ombe. “Una makuti mazuri, naweza kupata kidogo?” Ng’ombe akaomba. Lakini makuti yalikuwa matamu ng’ombe akayala yote!


“यह तुमने क्या किया?” वुसी रोया। “वह भूसा मेरी बहन के लिए उपहार था। मजदूरों ने मुझे दिया था वह भूसा क्योंकि उन्होंने फलवालों से मिली छड़ी को तोड़ दिया था। फलवालों ने मुझे इसलिए दिया क्योंकि उन्होंने मेरी बहन के केक के लिए मिले अंडे को तोड़ दिया था। केक मेरी बहन की शादी के लिए था। अब न तो अंडा है, न केक, और न कोई उपहार। मेरी बहन क्या कहेगी?”

“Umefanya nini?” Vusi akalia. “Makuti haya yalikuwa zawadi ya dada yangu. Wajenzi walinipa makuti kwa kuwa walivunja fimbo yangu niliyopewa na waangua matunda. Waangua matunda walinipa fimbo kwa kuwa walivunja yai kwa ajili ya keki ya dada yangu. Keki ilikuwa kwa ajili ya harusi ya dada yangu. Sasa hakuna yai, hakuna keki, na hakuna zawadi. Dada yangu atasemaje?”


गाय को पछतावा हुआ कि उसने लालच किया। किसान उसकी बहन के उपहार के रूप में गाय देने के लिए तैयार हो गया। वुसी गाय को अपने साथ ले जाने लगा।

Ng’ombe aliomba msamaha kwa kuwa mlafi. Mkulima alikubali kumpa Vusi ng’ombe aende naye kama zawadi kwa ajili ya dada yake. Vusi akaendelea na safari yake.


लेकिन गाय रात के समय दौड़ कर किसान के पास वापस आ गई। और वुसी रास्ता भूल गया। वह अपनी बहन की शादी में बहुत देर से पहुँचा। मेहमान पहले से ही खाना खा रहे थे।

Lakini wakati wa chakula cha jioni ng’ombe alikimbia kurudi kwa mkulima. Na Vusi akapotea njiani. Akafika kwa kuchelewa sana kwenye harusi ya dada yake. Wageni walikuwa tayari wanakula.


“मैं क्या करूँ?” वुसी रोने लगा।” मज़दूरों से से मिले भूसे के बदले में उपहार में मिली गाय भाग गई। राजमिस्त्रियों ने मुझे भूसा इसीलिए दिया था क्योंकि उन्होंने फलवालों से मिली छड़ी को तोड़ दिया था। फलवालों ने मुझे छड़ी इसलिए दी थी क्योंकि उन्होंने मेरे अंडे तोड़ दिए थे जो केक के लिए थे। केक शादी के लिए था। अब न तो अंडा है, न केक, और न ही उपहार”।

“Nifanye nini?” alilia Vusi. “Ng’ombe aliyekimbia alikuwa ni zawadi, ambayo nilipewa kama mbadala wa makuti niliyopewa na wajenzi. Wajenzi walinipa makuti kwa sababu walivunja fimbo niliyopewa na waangua matunda. Waangua matunda walinipa fimbo kwa sababu walivunja yai la keki. Keki ilikuwa kwa ajili ya harusi. Kwa hiyo hakuna yai, hakuna keki, na hakuna zawadi.”


वुसी की बहन ने थोड़ी देर सोचा, फिर वह बोली, “वुसी मेरे भाई, मुझे सच में उपहारों से कोई फ़र्क नहीं पड़ता। मुझे केक से भी कोई फ़र्क नहीं पड़ता! हम सभी यहाँ साथ में हैं, मैं खुश हूँ। अब तुम अच्छे से कपड़े पहनो और आओ हम मिलकर इस दिन का जश्न मनाते हैं!” और फिर वुसी ने ऐसा ही किया।

Dada yake Vusi alifikiria kwa muda, halafu akasema, “Kaka yangu Vusi, usijali zawadi, pia usijali keki! Tupo hapa pamoja, nina furaha. Nenda kavae nguo zako nadhifu na uje tusherehekee siku hii!”


Written by: Nina Orange
Illustrated by: Wiehan de Jager
Translated by: Nandani
Language: Hindi
Level: Level 4
Source: What Vusi's sister said from African Storybook
Creative Commons License
This work is licensed under a Creative Commons Attribution 3.0 International License.
Options
Back to stories list Download PDF