Download PDF
Back to stories list

Azeninfano Mtoto Punda

Written by Lindiwe Matshikiza

Illustrated by Meghan Judge

Translated by dohliam

Language Esperanto

Level Level 3

Narrate full story The audio for this story is currently not available.


Estis knabineto kiu unue vidis la misteran formon en la malproksimo.

Ilikuwa ni msichana mdogo aliyekuwa wa kwanza kuona umbo la ajabu kwa mbali.


Kiam la formo proksimiĝis, ŝi vidis ke ĝi estas tre graveda virino.

Kadiri umbo lilipokaribia, aliona kwamba lilikuwa ni mwanamke mwenye ujauzito mkubwa.


Sinĝena sed kuraĝa, la knabineto proksimiĝis al la virino. “Ni devas teni ŝin kun ni,” la popolo de la knabineto decidis. “Ni gardos ŝin kaj ŝian infanon sekure.”

Kwa upole na ujasiri, msichana alimsogelea mwanamke yule. “Lazima tumhifadhi,” watu wa msichana yule walisema. “Tutawaweka yeye na mtoto wake salama.”


La infano baldaŭ ekvenis. “Puŝu!” “Alportu kovrilojn!” “Akvo!” “Puuuuuŝŝŝŝŝuuu!!!”

Mtoto alikuwa njiani kuzaliwa si muda mrefu. “Sukuma!” “Leteni mablanketi!” “Maji!” “Suuukuuumaaaa!!!”


Sed kiam ili vidis la infaneton, ĉiuj saltis malantaŭen ŝokite. “Azeno?!”

Lakini walipomwona mtoto, wote waliruka kwa mshtuko. “Punda?!”


Ĉiuj ekdisputis. “Ni diris ke ni gardus la patrinon kaj la infanon sekure, kaj tion ni faros,” diris iuj. “Sed ili alportos al ni malbonŝancon!” diris aliuloj.

Wakaanza kubishana. “Tulisema tutawaweka mama na mtoto salama, na hivyo ndivyo tutakavyofanya,” baadhi wakasema. “Lakini watatuletea mkosi!” wengine wakadai.


Kaj tiel la virino trovis sin sola denove. Ŝi demandis sin, kion ŝi faru kun tiu stranga infano. Ŝi demandis sin, kion ŝi faru kun si mem.

Kwa hiyo mwanamke yule alijikuta yuko peke yake kwa mara nyingine tena. Akajiuliza atafanya nini na mtoto huyo wa ajabu. Akajiuliza atafanya nini na yeye mwenyewe.


Sed finfine ŝi devis akcepti ke li estas ŝia infano kaj ŝi estas lia patrino.

Lakini hatimaye alikubali kwamba huyo ni mwanaye na yeye ni mama yake.


Nu, se la infano restis same malgranda, ĉio eble okazus alie. Sed la azeninfano grandiĝis kaj grandiĝis, ĝis li ne plu trovisi lokon sur la dorso de sia patrino. Kaj kiom ajn li klopodis, li ne povis konduti sin kiel homo. Lia patrino estis ofte laca kaj ĉagrenita. Iufoje ŝi devigis lin fari bestan laboron.

Endapo mtoto huyo angebaki kuwa vilevile, na umbo dogo, labda kila kitu kingekuwa tofauti. Lakini mtoto Punda aliendelea kukua na kukua mpaka hakuweza kutoshea tena mgongoni mwa mama yake. Pamoja na kujaribu kwa bidii, hakuweza kuwa na tabia za kibinadamu. Mara nyingi mama yake alichoka na kuvunjika moyo. Wakati mwingine alimlazimisha kufanya kazi walizostahili wanyama.


Konfuzo kaj kolero kreskiĝis en Azeno. Li ne faru ĉi tion kaj li ne faru tion ĉi. Li ne kondutu sin tiel kaj li ne kondutu sin tiel. Li tiel koleriĝis ke iutage li piedbatis sian patrinon al la tero.

Kuchanganyikiwa na hasira vilianza kujengeka ndani mwa Punda. Alishindwa kufanya hivi wala vile. Alishindwa kuwa hivi wala vile. Alipatwa na hasira sana kiasi kwamba, siku moja, alimpiga teke mama yake mpaka akaanguka chini.


Azeno pleniĝis de honto. Li forkuris tiom malproksimen kaj tiom rapide kiom li povis

Punda alijawa na aibu. Akaanza kukimbilia mbali kwa haraka kadiri awezavyo.


Kiam li ĉesis kuri, estis jam nokto, kaj Azeno perdiĝis. “I-a?” li flustris al la mallumo. “I-a?” ĝi resonis al li. Li estis sola. Li buklis sin strikte en pilkoformo kaj eniris profundan kaj maltrankvilan dormadon.

Wakati aliposimama, ilikuwa ni usiku, na alikuwa amepotea. “Hii hoo?” alinong’ona gizani. “Hii hoo?” giza likatoa mwangwi. Alikuwa mwenyewe. Alijikunyata katika umbo dogo, akalala fofofo usingizi wa mang’amung’amu.


Azeno vekiĝis kaj vidis strangan maljunulon, kiu fikse rigardis lin desupre. Li rigardis en la okulojn de la maljunulo kaj eksentis iom da espero.

Punda aliamka na kumkuta mzee mmoja wa ajabu akimtazama. Akamwangalia mzee yule machoni na akaanza kuhisi ishara ya matumaini.


Azeno restis kun la maljunulo, kiu instruis lin pri multaj diversaj manieroj vivteni sin. Azeno aŭskultis kaj lernis, samkiel la maljunulo. Ili helpis unu la alian, kaj ili kune ridis.

Punda alienda kuishi na mzee yule, na mzee alimfundisha mbinu nyingi za kuishi. Punda alisikiliza na kujifunza, na mzee vivyo hivyo pia. Walisaidiana na kucheka pamoja.


Iun matenon la maljunulo petis Azeno-n porti lin al montopinto.

Asubuhi moja, mzee alimwomba Punda ambebe hadi kwenye kilele cha mlima.


Alte inter la nuboj ili dormiĝis. Azeno sonĝis, ke lia patrino malsanas kaj vokis lin. Kaj tiam li vekiĝis…

Walipofika juu kwenye mawingu, walipatwa na usingizi. Punda akaota kuwa mama yake alikuwa mgonjwa na alimhitaji. Na alipoamka…


… la nuboj estis malaperintaj, kune kun lia amiko, la maljunulo.

…mawingu yalikuwa yametoweka pamoja na rafiki yake, yule mzee.


Azeno finfine sciis, kion fari.

Hatimaye, Punda alijua alichotakiwa kufanya.


Azeno trovis sian patrinon, solan kaj funebrantan sian perditan infanon. Ili fikse rigardis unu la alian longtempe. Kaj tiam forte brakumis unu la alian.

Punda alimkuta mama yake akiwa peke yake huku akimwomboleza mwanaye aliyepotea. Wakaangaliana kwa muda mrefu. Na kisha wakakumbatiana kwa hisia.


La azeninfano kaj lia patrino kreskis kunen kaj trovis multajn manierojn vivi kune. Iom post iom aliaj familioj ekloĝis ĉirkaŭe.

Mtoto Punda na mama yake wamekuwa kitu kimoja na kuishi kwa ushirikiano. Taratibu, familia nyingine zimeanza kuhamia na kuishi miongoni mwao.


Written by: Lindiwe Matshikiza
Illustrated by: Meghan Judge
Translated by: dohliam
Language: Esperanto
Level: Level 3
Source: Donkey Child from African Storybook
Creative Commons License
This work is licensed under a Creative Commons Attribution 4.0 International License.
Options
Back to stories list Download PDF