Download PDF
Back to stories list

Magozwe Magozwe

Written by Lesley Koyi

Illustrated by Wiehan de Jager

Translated by Eunice Mukonde-Mulenga

Language IciBemba

Level Level 5

Narrate full story The audio for this story is currently not available.


Mwi tauni lya Nairobi, ukutali nendupwa, kwaleeikala abalumendo abaabula indupwa. Baaleeikalafye cikulu bwaca. Uluceelo lumo, abalumendo baaleelonga impasa shabo panuma yakulala mumpepo mumbali yanshila. Ukubomfya ifisooso, baalikoseshe umulilo pakutamye mpepo. Pali ili bumba paali Magozwe. Ewaali umwaice saana.

Kwenye jiji la Nairobi lenye pilikapilika nyingi, mbali na malezi ya nyumbani, paliishi kikundi cha wavulana wasiokuwa na makwao. Waliipokea kila siku ijayo kama ilivyo. Siku moja asubuhi, walikuwa wanakusanya virago vyao baada ya kulala kwenye baridi kando ya barabara. Ili kuondoa baridi, walikoka moto kwa kutumia takataka. Miongoni mwa kikundi hicho cha wavulana alikuwepo Magozwe. Alikuwa ni mdogo kuliko wote.


Ilyo abafyashi bakwa Magozwe baafwile, aalifye neemyaka isaano. Aile mukwikala na banalume. Banalume tabapooseleko amaano kumwana. Magozwe tabaaleemupeela ifyakulya fyakumanina. Baaleemupupeela incito shakubomba ishingi.

Wakati wazazi wa Magozwe walipofariki, alikuwa na miaka mitano tu. Alienda kuishi na mjomba wake. Mjomba hakumjali Magozwe. Hakumpa chakula cha kutosha. Alimfanyisha kazi nyingi nzito.


Nga Magozwe ati epushe neelyo ukuilishanya, banalume baaleemuma. Ilyo Magozwe aipwishe palwa kuya kusukulu, banalume baalimumine nookutila, “Iwe taumfwa. Tapali ico wingasambilila.” Panuma yamyaka itatatu iya kumusunga ifi, Magozwe aalibuutwike ukufuma pang’anda yabanalume. Aambile ukwikala mumusebo.

Magozwe alipolalamika au kuuliza, mjomba wake alimpiga. Magozwe alipouliza kama ataweza kwenda shule, mjomba wake alimpiga na kumwambia, “Wewe ni mjinga, hutaweza kujifunza chochote.” Baada ya miaka mitatu ya kunyanyaswa, Magozwe alitoroka kwa mjomba wake. Akaanza kuishi mtaani.


Ukwikala pamusebo kwali ukwayafya kabili abalumendo abengi baaleecuula cila bushiku pakusanga icakulya. Inshiku shimo baaleebooma, shimbi baaleebeekata kuli bakapokola. Nga baalwaala takwaleeba aba kubaafwa. Ulupiya baaleesanga mukulombalomba, mukushitisha amapulasitiki nafimbi elwaleebaafwilishako. Ubuumi bwalyafisheko pantu amabumba yambi aya balumendo yaaleefwaya ukupoka incende shapusanapusana mutauni.

Maisha ya mtaani yalikuwa magumu na wavulana wengi walipambana kila siku ili wapate chakula tu. Mara nyingine walikamatwa, mara nyingine walipigwa. Walipougua, kulikuwa hakuna mtu wa kuwasaidia. Kikundi kilitegemea hela ndogo ndogo walizopata kwa kuomba omba, na kwa kuuza plastiki na vitu kuukuu. Maisha yalikuwa magumu zaidi hasa kwa sababu ya vita dhidi ya vikundi pinzani vilivyotaka kudhibiti baadhi ya maeneo ya jiji.


Bushiku bumo ilyo Magozwe aleefwayafwaya mufisooso, asangile ibuuku ilyakale ilyalepauka. Afumisheko ifiko aalibikile namwisaaka. Cila bushiku, aleefumya ibuuku nookwamba ukulolesha pafikope. Taishibe ukubelenga.

Siku moja Magozwe alipokuwa anachakura kwenye mapipa ya takataka, alikuta kitabu cha hadithi kilichokuwa kimechakaa. Aliondoa uchafu kwenye kitabu na kukiweka ndani ya mfuko wake. Kila siku baada ya hapo, alikitoa kitabu na kuangalia picha. Hakujua kusoma maandishi.


Ifikope fyaleelanga umulumendo uwaishileba kensha wandeke ilyo aakulile. Magozwe aleeloota namukasuba palwakuba kensha wandeke. Inshita shimo aleemona ukuti emulumendo wine uwa mwibuku.

Picha zilikuwa zinaongelea hadithi ya mvulana ambaye alikuja kuwa rubani. Magozwe aliota kuwa rubani. Mara nyingine alifikiria kwamba yeye ni yule mvulana kwenye hadithi.


Kwalitaleele kabili Magozwe aiminine pamusebo aleelombalomba. Umwaume umo aishile mupeepi napo aali. “Uli shaani? Nine Thomas. Momba mupeepi napano, pancende wingapoka icakulya,” efyo atiile. Asontele kung’anda yayeelo noomutenge wabuluu. “Ninjishiba, walaayapoka ifyakulya?” efyo aipwishe. Magozwe aloleeshe umwaume elyo aloleeshe kung’anda. “Limbi ndeeya,” efyo aaswike afumanapo.

Kulikuwa na baridi na Magozwe alikuwa amesimama barabarani akiomba omba. Mtu alimkaribia. “Hujambo? Naitwa Thomas. Nafanya kazi karibu na hapa, mahali unapoweza kupata kitu cha kula,” mtu yule alisema. Alionyesha nyumba ya njano yenye paa la buluu. “Natumaini utaenda pale kupata chakula kidogo?” Thomas aliuliza. Magozwe alimwangalia yule mtu, kisha akaiangalia ile nyumba. “Labda,” akasema, halafu akaondoka.


Imyeshi yakonkelepo, abalumendo baalibeeleshe ukumona Thomas. Alitemenwe ukulanda nabantu makamaka abaleeikala mumusebo. Thomas aleeumfwa amalyashi ya bantu aba. Aali uuposa amano kufintu kabili uwacikuuku noomucinshi. Abalumendo bamo, baambile ukuya kung’anda yayeelo nabuluu mukupoka ifyakulya akasuba.

Miezi iliyofuata, wavulana wale wa mtaani walizoea kumwona Thomas hapa na pale. Alipenda kuzungumza na watu, hasa walioishi mitaani. Thomas alisikiliza simulizi za maisha ya watu. Alikuwa makini na mwenye subira, na hakuwa na kiburi wala dharau. Baadhi ya wavulana walianza kwenda kwenye ile nyumba ya njano na buluu ili kupata chakula cha mchana.


Magozwe aikele mumbali yanshila aleetamba ifikope mwibuuku lyakwe ilyo Thomas aishileeikala mupeepi nawene. “Lileelanda pali cinshi ilyashi?” efyo Thomas aipwishe. “Lileelanda pamulumendo uwasangwike kensha wandeke,” efyaaswike Mazongwe. “Naani ishina umulumendo?” Thomas aipwishe. “Katwishi, nshaishiba ukubelenga,” efyaaswike Mazongwe panoono.

Magozwe alikuwa amekaa kando ya barabara akiangalia kitabu chake cha picha Thomas alipokaa pembeni mwake. “Hadithi hiyo inahusu nini?” Thomas akauliza. “Inahusu mvulana aliyekuja kuwa rubani,” Magozwe akajibu. “Jina lake ni nani?” Thomas akauliza. “Sijui, siwezi kusoma,” Magozwe akasema kwa sauti ya chini.


Ilyo baakumeene, Magozwe atendeke ukweba Thomas ilyashi pa buumi bwakwe. Amwebele ifyo abuutwike ukufuma kuli banalume. Thomas taalaandile ifingi kabili taebele Magozwe ifyakucita leelo aleeumfwikishafye. Limolimo baleelanshanya ilyo baleelya mung’anda yamutenge wabuluu.

Walipokutana, Magozwe alianza kumsimulia Thomas maisha yake. Alimwelezea kuhusu mjomba wake na sababu zilizomfanya atoroke. Thomas hakuongea sana, wala hakumwambia Magozwe nini cha kufanya, bali alisikiliza kwa makini kila mara. Wakati mwingine waliongea wakiwa wanakula kwenye ile nyumba yenye paa la buluu.


Ilyo Magozwe aali nemyaka ikumi Thomas alimupeele ibuuku. Ibuuku lyali pamulumendo wamumushi uwaleeteya umupila uwalumbwike saana. Thomas alimubelengele Magozwe ili lyashi imiku iingi mpakafye bushiku bumo atiile, “Ndetontonkanyefyo ulingile ukutampeesukulu pakuti usambilile ukubelenga. Uleetontonkanyapo shani?” Thomas atiile alishibepo incende uko abaana benga laala nookuya kusukulu.

Mnamo mwaka wa kumi wa kuzaliwa kwa Magozwe, Thomas alimzawadia kitabu kipya cha hadithi. Ilikuwa ni hadithi inayohusu mvulana wa kijijini aliyekuja kuwa mcheza mpira maarufu. Thomas alimsomea Magozwe hadithi hiyo mara nyingi, mpaka siku moja akasema, “Nafikiri wakati umewadia wa kwenda shule kujifunza kusoma. Unaonaje?” Thomas alieleza kwamba anajua sehemu ambayo watoto wanaweza kuishi na kwenda shule.


Magozwe atontonkenye pancende ukwakulaala kabili nookuya kusukulu. Nga limbi ifyo banalume bamwebele ati toomfwa teeti asambilile icili conse fyaciine? Nga cakuti kulya kuncende bamuuma? Alitiinine. “Limbi cawamapo ukutwalilila ukwikala mumusebo,” efyaatontonkenye.

Magozwe alifikiria kuhusu sehemu hii mpya, na kuhusu kwenda shule. Itakuwaje kama mjomba wake alikuwa sahihi kwamba alikuwa mjinga kiasi cha kutoweza kujifunza chochote? Itakuwaje kama watampiga sehemu hii mpya? Aliogopa. “Labda ni heri kuendelea kuishi mtaani,” aliwaza.


Aebele Thomas ati aali no mwenso. Thomas alimwebekesha ati akeekala bwino kuncende ilya.

Alimshirikisha Thomas juu ya hofu aliyokuwa nayo. Baada ya muda Thomas alimhakikishia kwamba maisha yatakuwa bora huko sehemu mpya.


Lyene Magozwe aile mukwikala mumuputule mung’anda yamutenge wagilini. Aleeikalamo na balumendo babili bambi. Bonse pamo abaana baali ikumi abaleeikala muli ilya ng’anda. Elyo naba Baamaama Cissy nabalume baabo neembwa shitatu, puushi elyo neembushi iikote.

Kwa hiyo Magozwe alihamia kwenye chumba katika nyumba yenye paa la kijani. Alikaa chumba kimoja na wavulana wengine wawili. Kwa ujumla kulikuwa na watoto kumi walioishi kwenye nyumba ile. Waliishi pamoja na Shangazi Cissy na mume wake, mbwa watatu, paka mmoja, na mbuzi aliyezeeka.


Magozwe alyambile isukulu kabili lyalikosele. Fingi ashaishibe ifyo aalingile ukwishiba pakuti alingane nabanankwe. Limolimo aleefwaya ukuleka. Leelo pamulandu weetontonkanyo pali kensha wandeke nakateya wamupila abamumabuuku yakwe, taalekele nga filya fine nabo bashalekele.

Magozwe alianza shule na ilikuwa ngumu. Alikuwa na mengi ya kujifunza. Mara nyingine alitaka kukata tamaa. Lakini aliwaza kuhusu rubani na mcheza mpira kwenye vitabu vya hadithi. Kama wao, hakukata tamaa.


Magozwe aikeele panse mulubansa lwang’anda yamutenge wagilini, aleebelenga ibuuku lya kusukulu. Elyo Thomas aikeele mupeepi nankwe. “Lilelanda pali cinshi ilyashi?” Thomas aipwishe. “Lileelanda pamulumendo asangwike kafundisha,” efyaaswike Magozwe. “Naani ishina umulumendo?” efyaipwishe Thomas. “Ishina lyakwe ni Magozwe,” efyaaswike Magozwe aleemwentula.

Magozwe alikuwa amekaa uani kwenye nyumba yenye paa la kijani, akisoma kitabu cha hadithi cha shule. Thomas alikuja na kukaa kando yake. “Hadithi inahusu nini?” Thomas akauliza. “Inahusu mvulana aliyekuja kuwa mwalimu,” Magozwe akajibu. “Jina lake ni nani?” akauliza Thomas. “Jina lake ni Magozwe,” Magozwe akasema kwa tabasamu.


Written by: Lesley Koyi
Illustrated by: Wiehan de Jager
Translated by: Eunice Mukonde-Mulenga
Language: IciBemba
Level: Level 5
Source: Magozwe from African Storybook
Creative Commons License
This work is licensed under a Creative Commons Attribution 4.0 International License.
Read more level 5 stories:
Options
Back to stories list Download PDF