Download PDF
Back to stories list

Nozibele na nywele tatu Nozibele na nywele tatu Nozibele and the three hairs

Written by Tessa Welch

Illustrated by Wiehan de Jager

Translated by Matteo E. Mwita

Read by Lauwo George

Language Kiswahili

Level Level 3

Narrate full story

Reading speed

Autoplay story


Hapo zamani za kale, wasichana watatu walienda kukusanya kuni.

Hapo zamani za kale, wasichana watatu walienda kukusanya kuni.

A long time ago, three girls went out to collect wood.


Ilikuwa ni siku yenye jua kali na wakaamua kwenda mtoni kuogelea. Wakaogelea huku wakicheza na kurushiana maji.

Ilikuwa ni siku yenye jua kali na wakaamua kwenda mtoni kuogelea. Wakaogelea huku wakicheza na kurushiana maji.

It was a hot day so they went down to the river to swim. They played and splashed and swam in the water.


Ghafla waligundua kuwa muda umekwenda. Wakaharakisha kurudi nyumbani.

Ghafla waligundua kuwa muda umekwenda. Wakaharakisha kurudi nyumbani.

Suddenly, they realised that it was late. They hurried back to the village.


Walipokuwa wanakaribia kufika nyumbani, Nozibele akajishika shingoni. Alikuwa amesahau shanga zake! “Tafadhali turudini!” aliwasihi rafiki zake. Lakini rafiki zake wakasema tumechelewa.

Walipokuwa wanakaribia kufika nyumbani, Nozibele akajishika shingoni. Alikuwa amesahau shanga zake! “Tafadhali turudini!” aliwasihi rafiki zake. Lakini rafiki zake wakasema tumechelewa.

When they were nearly home, Nozibele put her hand to her neck. She had forgotten her necklace! “Please come back with me!” she begged her friends. But her friends said it was too late.


Kwa hiyo Nozibele akarudi mwenyewe mtoni. Akapata shanga zake na akakimbia kurudi nyumbani. Lakini akapotea gizani.

Kwa hiyo Nozibele akarudi mwenyewe mtoni. Akapata shanga zake na akakimbia kurudi nyumbani. Lakini akapotea gizani.

So Nozibele went back to the river alone. She found her necklace and hurried home. But she got lost in the dark.


Kwa mbali akaona mwanga unatoka kwenye nyumba. Akakimbilia kwenye nyumba na kugonga mlango.

Kwa mbali akaona mwanga unatoka kwenye nyumba. Akakimbilia kwenye nyumba na kugonga mlango.

In the distance she saw light coming from a hut. She hurried towards it and knocked at the door.


Akastaajabu kumwona mbwa akifungua mlango na akasema, “Unataka nini?” “Nimepotea na ninatafuta sehemu ya kulala,” akasema Nozibele. “Ingia ndani, la sivyo nitakung’ata!” mbwa akamwambia. Nozibele akaingia ndani.

Akastaajabu kumwona mbwa akifungua mlango na akasema, “Unataka nini?” “Nimepotea na ninatafuta sehemu ya kulala,” akasema Nozibele. “Ingia ndani, la sivyo nitakung’ata!” mbwa akamwambia. Nozibele akaingia ndani.

To her surprise, a dog opened the door and said, “What do you want?” “I’m lost and I need a place to sleep,” said Nozibele. “Come in, or I’ll bite you!” said the dog. So Nozibele went in.


Mbwa akamwambia, “Nipikie!” “Sijawahi kumpikia mbwa,” akajibu. “Pika, la sivyo nitakung’ata!” mbwa akasema. Nozibele akampikia mbwa chakula.

Mbwa akamwambia, “Nipikie!” “Sijawahi kumpikia mbwa,” akajibu. “Pika, la sivyo nitakung’ata!” mbwa akasema. Nozibele akampikia mbwa chakula.

Then the dog said, “Cook for me!” “But I’ve never cooked for a dog before,” she answered. “Cook, or I’ll bite you!” said the dog. So Nozibele cooked some food for the dog.


Mbwa akamwambia, “Nitandikie kitanda!” Nozibele akajibu, “Sijawahi kumtandikia mbwa kitanda.” “Tandika kitanda, la sivyo nitakung’ata!” mbwa akasema. Nozibele akatandika kitanda.

Mbwa akamwambia, “Nitandikie kitanda!” Nozibele akajibu, “Sijawahi kumtandikia mbwa kitanda.” “Tandika kitanda, la sivyo nitakung’ata!” mbwa akasema. Nozibele akatandika kitanda.

Then the dog said, “Make the bed for me!” Nozibele answered, “I’ve never made a bed for a dog.” “Make the bed, or I’ll bite you!” the dog said. So Nozibele made the bed.


Akawa kila siku anampikia, anamfulia na kumfagilia mbwa. Siku moja mbwa akasema, “Nozibele, leo naenda kuwatembelea rafiki zangu. Fagia nyumba, pika chakula na osha vitu vyangu kabla sijarudi.”

Akawa kila siku anampikia, anamfulia na kumfagilia mbwa. Siku moja mbwa akasema, “Nozibele, leo naenda kuwatembelea rafiki zangu. Fagia nyumba, pika chakula na osha vitu vyangu kabla sijarudi.”

Every day she had to cook and sweep and wash for the dog. Then one day the dog said, “Nozibele, today I have to visit some friends. Sweep the house, cook the food and wash my things before I come back.”


Mara baada tu ya mbwa kuondoka, Nozibele akanyofoa nywele tatu kutoka kwenye kichwa chake. Akaweka unywele mmoja chini ya kitanda, mmoja nyuma ya mlango, na mwingine akauweka kwenye uzio wa nyumba. Halafu, akakimbia kuelekea nyumbani kwa nguvu zote.

Mara baada tu ya mbwa kuondoka, Nozibele akanyofoa nywele tatu kutoka kwenye kichwa chake. Akaweka unywele mmoja chini ya kitanda, mmoja nyuma ya mlango, na mwingine akauweka kwenye uzio wa nyumba. Halafu, akakimbia kuelekea nyumbani kwa nguvu zote.

As soon as the dog had gone, Nozibele took three hairs from her head. She put one hair under the bed, one behind the door, and one in the kraal. Then she ran home as fast as she could.


Mbwa aliporudi akaanza kumtafuta Nozibele. “Nozibele, uko wapi?” akapiga kelele. “Niko hapa, chini ya kitanda,” unywele wa kwanza ukajibu. “Nipo hapa nyuma ya mlango,” unywele wa pili ukajibu. “Niko hapa kwenye uzio,” unywele wa tatu ukajibu.

Mbwa aliporudi akaanza kumtafuta Nozibele. “Nozibele, uko wapi?” akapiga kelele. “Niko hapa, chini ya kitanda,” unywele wa kwanza ukajibu. “Nipo hapa nyuma ya mlango,” unywele wa pili ukajibu. “Niko hapa kwenye uzio,” unywele wa tatu ukajibu.

When the dog came back, he looked for Nozibele. “Nozibele, where are you?” he shouted. “I’m here, under the bed,” said the first hair. “I’m here, behind the door,” said the second hair. “I’m here, in the kraal,” said the third hair.


Mbwa akagundua kuwa Nozibele amemkimbia. Kwa hiyo akakimbia kuelekea kijijini. Kaka zake Nozibele walikuwa wakimsubiri na fimbo. Mbwa alipowaona akageuka na kukimbia, na hajawahi kuonekana tena.

Mbwa akagundua kuwa Nozibele amemkimbia. Kwa hiyo akakimbia kuelekea kijijini. Kaka zake Nozibele walikuwa wakimsubiri na fimbo. Mbwa alipowaona akageuka na kukimbia, na hajawahi kuonekana tena.

Then the dog knew that Nozibele had tricked him. So he ran and ran all the way to the village. But Nozibele’s brothers were waiting there with big sticks. The dog turned and ran away and has never been seen since.


Written by: Tessa Welch
Illustrated by: Wiehan de Jager
Translated by: Matteo E. Mwita
Read by: Lauwo George
Language: Kiswahili
Level: Level 3
Source: Nozibele and the three hairs from African Storybook
Creative Commons License
This work is licensed under a Creative Commons Attribution 3.0 International License.
Options
Back to stories list Download PDF