Download PDF
Back to stories list

Anansi et la sagesse Anansi na hekima Anansi and Wisdom

Written by Ghanaian folktale

Illustrated by Wiehan de Jager

Translated by Alexandra Danahy

Read by Monique Bournot-Trites

Language French

Level Level 3

Narrate full story

Reading speed

Autoplay story


Il y a longtemps, les gens ne savaient rien. Ils ne savaient pas comment ensemmencer et cultiver leurs champs, ou comment tisser, ou comment fabriquer des outils de fer. Le dieu Nyame dans le ciel avait toute la sagesse du monde. Il la gardait en sécurité dans un pot en argile.

Hapo zamani za kale, watu hawakujua chochote. Hawakujua kupanda mimea, hawakujua kushona nguo, wala hawakujua kuunda zana za chuma. Nyame, mungu aliyekuwa mbinguni, ndiye aliyekuwa mwenye hekima zote za dunia. Alihifadhi hekima hiyo kwenye chungu cha udongo.

Long long ago people didn’t know anything. They didn’t know how to plant crops, or how to weave cloth, or how to make iron tools. The god Nyame up in the sky had all the wisdom of the world. He kept it safe in a clay pot.


Un jour, Nyame décida qu’il donnerait le pot de la sagesse à Anansi. Chaque fois qu’Anansi regardait dans le pot en argile, il apprenait quelque chose de nouveau. C’était tellement excitant !

Siku moja, Nyame aliamua kumpa Anansi chungu hicho cha hekima. Kila Anansi alipotazama ndani ya chungu cha udongo, alijifunza jambo jipya. Alifurahi sana!

One day, Nyame decided that he would give the pot of wisdom to Anansi. Every time Anansi looked in the clay pot, he learned something new. It was so exciting!


Anansi, l’avide, pensa: « Je vais garder le pot en sécurité en haut d’un grand arbre. Comme ça je pourrai l’avoir à moi seul ! » Il fila un fil long, l’enroula autour du pot en argile et l’attacha à son estomac. Il commença à grimper à l’arbre. Mais c’était difficile de grimper à l’arbre avec le pot qui lui cognait les genoux tout le temps.

Anansi mlafi alinong’ona moyoni, “Nitakificha chungu hiki juu ya mti mrefu ili nikifaidi mwenyewe.” Akasokota uzi mrefu na kuuzungusha kwenye chungu. Kisha, akajifunga tumboni. Akaanza kupanda kwenye mti. Lakini ilikuwa vigumu kupanda kwenye mti huku chungu kikimgonga magotini kila mara.

Greedy Anansi thought, “I’ll keep the pot safe at the top of a tall tree. Then I can have it all to myself!” He spun a long thread, wound it round the clay pot, and tied it to his stomach. He began to climb the tree. But it was hard climbing the tree with the pot bumping him in the knees all the time.


Pendant tout ce temps, le jeune fils d’Anansi était debout en bas de l’arbre en train de regarder. « Au lieu de faire ceci, ne serait-il pas plus facile d’attacher le pot à ton dos ? » Anansi essaya d’attacher le pot rempli de sagesse à son dos et ce fut vraiment plus facile.

Wakati huo wote, mwanawe alikuwa amesimama chini ya ule mti akimtazama baba yake. Akamwambia, “Baba, si ingekuwa rahisi kupanda endapo ungekifungia chungu mgongoni?” Basi Anansi akajaribu kukifungia chungu kilichojaa hekima mgongoni mwake, na kweli ikawa rahisi zaidi.

All the time Anansi’s young son had been standing at the bottom of the tree watching. He said, “Wouldn’t it be easier to climb if you tied the pot to your back instead?” Anansi tried tying the clay pot full of wisdom to his back, and it really was a lot easier.


En peu de temps il atteignit le sommet de l’arbre. Mais il arrêta et pensa, « Je suis censé être celui qui a toute la sagesse et voici que mon fils est plus sage que moi ! » Anansi était tellement fâché à propos de ceci qu’il lança le pot en argile en bas de l’arbre.

Punde tu alipofika juu ya mti, aliwaza, “Natakiwa kuwa ndiye mwenye hekima zote, lakini hapa mwanangu ndiye mwenye akili kuliko mimi.” Anansi alikasirishwa sana kiasi kwamba alikitupa kile chungu chini ya mti.

In no time he reached the top of the tree. But then he stopped and thought, “I’m supposed to be the one with all the wisdom, and here my son was cleverer than me!” Anansi was so angry about this that he threw the clay pot down out of the tree.


Le pot se cassa en mille morceaux sur le sol. La sagesse fut accessible à tous. Et c’est ainsi que les gens apprirent à cultiver, tisser, fabriquer des outils de fer, et toutes les autres choses que les gens savent faire.

Chungu kilivunjika vipandevipande pale chini. Hekima zikawa za bure kwa mtu yeyote kujichukulia. Na hivyo ndivyo watu walivyojifunza kulima, kushona nguo, kuunda zana za chuma, na mambo yote mengine ambayo watu wanajua kuyafanya.

It smashed into pieces on the ground. The wisdom was free for everyone to share. And that is how people learned to farm, to weave cloth, to make iron tools, and all the other things that people know how to do.


Written by: Ghanaian folktale
Illustrated by: Wiehan de Jager
Translated by: Alexandra Danahy
Read by: Monique Bournot-Trites
Language: French
Level: Level 3
Source: Anansi and Wisdom from African Storybook
Creative Commons License
This work is licensed under a Creative Commons Attribution 3.0 International License.
Options
Back to stories list Download PDF