Download PDF
Back to stories list

Imbewu Encane Mbegu Ndogo: Hadithi ya Wangari Maathai

Written by Nicola Rijsdijk

Illustrated by Maya Marshak

Translated by Nal’ibali

Read by Beauty Ngwenya

Language Zulu

Level Level 3

Narrate full story The audio for this story is currently not available.


Emuzini osekwehleleni kweNtaba iKenya eMpumalanga ye-Afrika, kwakunentombazanyana eyayisebenza emasimini nomama wayo.

Katika kijiji kimoja kwenye mteremko wa Mlima wa Kenya, katika Afrika Mashariki, msichana mdogo alifanya kazi za shambani pamoja na mama yake. Msichana huyu aliitwa Wangari.


UWangari wayekuthanda ukuba ngaphandle. Esivandeni sokudla somndeni wakhe wayelima khona umhlabathi ngegeja lakhe i-machete. Wayecindezela imbewu encane emhlabathini ofudumele.

Wangari alipenda kufanya kazi za nje. Alitumia jembe kulima katika bustani ya familia yake. Kisha alipanda mbegu ndogo katika ardhi yenye rutuba.


Isikhathi sosuku ayesithanda kwakungemvana kokushona kwelanga. Lapho sekumnyama kakhulu ukuthi angabona izitshalo, uWangari wayazi ukuthi sekuyisikhathi sokubuyela ekhaya.

Alipenda majira ya jioni, wakati jua linapozama. Giza lilipozidi mpaka aliposhindwa kuona mimea, Wangari alifahamu kuwa wakati wa kwenda nyumbani uliwadia. Alikuwa anafuata kinjia chembamba kilichopita uwanjani huku akivuka mito akielekea nyumbani.


UWangari wayeyingane ehlakaniphe kakhulu futhi wayeselangazelela ukuya esikoleni. Kodwa umama kanye nobaba wakhe babefuna ahlale ekhaya ukuze abasize.

Wangari alikuwa mtoto mwerevu na alikuwa na hamu ya kwenda shule. Lakini wazazi wake walitaka awasaidie nyumbani. Alipofika umri wa miaka saba, kaka yake aliwashawishi wazazi wake kumwacha aende shule.


Wayekuthanda ukufunda!

Alipenda kusoma! Wangari alijifunza zaidi na zaidi kwa kila kitabu alichokisoma. Alifanya vyema sana shuleni hadi akaalikwa kwenda Marekani kuendeleza masomo yake huko. Wangari alitiwa hamasa sana na nafasi hii! Alipenda kujua ulimwengu zaidi.


ENyuvesi yaseMelika uWangari wafunda izinto eziningi ezintsha. Wafunda ngezitshalo nangokuthi zikhula kanjani. Wakhumbula nangokuthi wakhula kanjani: edlala imidlalo nabafowabo emithunzini yezihlahla ezinkulu emahlathini amahle aseKenya.

Alipokuwa chuoni huko Marekani, Wangari alijifunza mengi mapya. Alisomea mimea na jinsi inavyokua. Na alikumbuka maisha yake yalivyokuwa utotoni: kucheza michezo na msitu zake katika kivuli cha miti kwenye misitu maridadi ya Kenya.


Lapho kwanda akufundayo, wabona nokuthi wayebathanda abantu baseKenya. Wayefuna ukuba bajabule futhi bakhululeke.

Jinsi alivyojifunza ndivyo alivyofahamu kuwa aliwapenda watu wa Kenya. Alitaka wafurahi na wawe wenye uhuru. Jinsi alivyojifunza ndivyo alivyokumbuka nyumbani kwao Afrika.


Lapho eseqede izifundo zakhe, wabuyela eKenya. Kodwa izwe lakhe lase liguqukile. Kwakukhona amapulazi amakhulu ayesendlaleke kulo mhlaba.

Alipokamilisha masomo yake, alirudi Kenya. Lakini nchi yake ilikuwa imebadilika. Kulikuwa na mashamba makubwa kila upande. Wanawake hawakupata kuni za kuwasha moto wa kupikia. Watu walikuwa maskini na watoto walikuwa na njaa.


UWangari wakwazi ukuthi kumele enzeni. Wafundisa abantu besifazane ukuthi batshale izihlahla ngembewu.

Wangari alijua la kufanya. Aliwafundisha wanawake jinsi ya kupanda miti kutokana na miche. Wanawake waliuza ile miti na pesa walizopata walizitumia kwa mahitaji ya familia zao. Wanawake walifurahi. Wangari alikuwa amewasaidia kuwa wenye nguvu na uwezo.


Ngokuhamba kwesikhathi, kwakhula izihlahla ezintsha zaba ngamahlathi, kwase kuqala ukugeleza kwemifula futhi. Umlayezo kaWangari wasabalala ne-Afrika.

Muda ulipopita, miti mipya ilikuwa misitu, na mito ilianza tena kupitisha maji. Ujumbe wa Wangari ulienea Afrika nzima. Leo, mamilioni ya miti imemea kutokana na mbegu za Wangari.


UWangari wayesebenze kanzima.

Wangari alikuwa amefanya bidii. Watu ulimwengu mzima walifahamu hili na wakampa tuzo. Tuzo hii inaitwa, ‘Tuzo ya Amani ya Nobel.’ Na alikuwa mwanamke wa Kiafrika wa kwanza kupokea tuzo hii.


UWangari washona ngowezi-2011, kodwa sicabanga ngaye njalo uma sibona isihlahla esihle.

Wangari alifariki mwaka 2011, lakini tunaweza kumkumbuka kila tunapoona mti maridadi.


Written by: Nicola Rijsdijk
Illustrated by: Maya Marshak
Translated by: Nal’ibali
Read by: Beauty Ngwenya
Language: Zulu
Level: Level 3
Source: A Tiny Seed: The Story of Wangari Maathai from African Storybook
Creative Commons License
This work is licensed under a Creative Commons Attribution 4.0 International License.
Options
Back to stories list Download PDF