Download PDF
Back to stories list

瑪哥威 Magozwe

Written by Lesley Koyi

Illustrated by Wiehan de Jager

Translated by dohliam

Read by Zoe Lam

Language Cantonese

Level Level 5

Narrate full story

Reading speed

Autoplay story


內羅比係個繁忙嘅城市,嗰度有班流浪街頭嘅男仔,佢哋日復一日噉過日子,從來都唔知道乜嘢叫做舒適安逸嘅生活。一日朝頭早,班男仔喺凍冰冰嘅行人路上面瞓醒,摺埋佢哋攞嚟瞓街嘅氊仔。天氣太凍喇,為咗驅寒,佢哋就要用執返嚟嘅垃圾點著堆火。喺呢班男仔裡面,年紀最細嗰個叫做瑪哥威。

Kwenye jiji la Nairobi lenye pilikapilika nyingi, mbali na malezi ya nyumbani, paliishi kikundi cha wavulana wasiokuwa na makwao. Waliipokea kila siku ijayo kama ilivyo. Siku moja asubuhi, walikuwa wanakusanya virago vyao baada ya kulala kwenye baridi kando ya barabara. Ili kuondoa baridi, walikoka moto kwa kutumia takataka. Miongoni mwa kikundi hicho cha wavulana alikuwepo Magozwe. Alikuwa ni mdogo kuliko wote.


瑪哥威嘅爹哋媽咪過身嘅時候,佢只得五歲咋,之後佢就搬去同佢阿叔一齊住。佢阿叔從來都冇關心過瑪哥威。瑪哥威喺叔叔屋企度捱飢抵冷,仲要做好多粗重嘢添。

Wakati wazazi wa Magozwe walipofariki, alikuwa na miaka mitano tu. Alienda kuishi na mjomba wake. Mjomba hakumjali Magozwe. Hakumpa chakula cha kutosha. Alimfanyisha kazi nyingi nzito.


一旦瑪哥威有少少抱怨,阿叔就會打佢。有一次,瑪哥威問吓阿叔可唔可以去返學,佢阿叔就好兇狠噉打佢,仲話:「你咁蠢,讀幾多書都冇用啦!」瑪哥威過咗三年嘅辛苦日子,卒之離家出走,無家可歸。

Magozwe alipolalamika au kuuliza, mjomba wake alimpiga. Magozwe alipouliza kama ataweza kwenda shule, mjomba wake alimpiga na kumwambia, “Wewe ni mjinga, hutaweza kujifunza chochote.” Baada ya miaka mitatu ya kunyanyaswa, Magozwe alitoroka kwa mjomba wake. Akaanza kuishi mtaani.


流浪生活非常之艱難,每日班男仔好勉強先至可以搵到一餐晏仔。佢哋有時要俾差佬拉,有時又要捱打。當佢哋病嘅時候,仲冇人會照顧佢哋添。班男仔唯有靠揸兜乞食得返嚟嘅少少錢過活,有時亦都會賣啲膠品同舊嘢賺返少少錢。有時第二啲流浪漢會嚟撩交打,爭地頭,生活就更加辛苦。

Maisha ya mtaani yalikuwa magumu na wavulana wengi walipambana kila siku ili wapate chakula tu. Mara nyingine walikamatwa, mara nyingine walipigwa. Walipougua, kulikuwa hakuna mtu wa kuwasaidia. Kikundi kilitegemea hela ndogo ndogo walizopata kwa kuomba omba, na kwa kuuza plastiki na vitu kuukuu. Maisha yalikuwa magumu zaidi hasa kwa sababu ya vita dhidi ya vikundi pinzani vilivyotaka kudhibiti baadhi ya maeneo ya jiji.


有一日,瑪哥威正喺度抄緊垃圾桶,佢搵到本甩皮甩骨嘅故仔書,就吹走咗書上面嘅塵,放入佢嘅袋度。以後每日得閒嘅時候,佢都會攞本書出嚟睇圖畫,只可惜佢睇唔明上面嘅文字。

Siku moja Magozwe alipokuwa anachakura kwenye mapipa ya takataka, alikuta kitabu cha hadithi kilichokuwa kimechakaa. Aliondoa uchafu kwenye kitabu na kukiweka ndani ya mfuko wake. Kila siku baada ya hapo, alikitoa kitabu na kuangalia picha. Hakujua kusoma maandishi.


啲圖畫講嘅係一個男仔大個成為飛機師嘅故仔。瑪哥威有時會發白日夢想象自己都成為飛機師。有時,佢仲會想象自己就係故仔入面嘅男仔。

Picha zilikuwa zinaongelea hadithi ya mvulana ambaye alikuja kuwa rubani. Magozwe aliota kuwa rubani. Mara nyingine alifikiria kwamba yeye ni yule mvulana kwenye hadithi.


有一日,天氣好凍,瑪哥威企喺街頭乞食。一個男人走過嚟,同佢打招呼,就話:「你好,我叫湯瑪斯。我喺呢度左近打工,你得閒可以去嗰便攞啲嘢食。」佢指住間藍頂黃牆嘅大屋,「我希望你唔會嫌棄,去嗰便攞啲嘢食啦!」瑪哥威睇咗吓個男人,又睇咗吓間屋,就話:「或者啦!」然之後佢就走開咗嘞。

Kulikuwa na baridi na Magozwe alikuwa amesimama barabarani akiomba omba. Mtu alimkaribia. “Hujambo? Naitwa Thomas. Nafanya kazi karibu na hapa, mahali unapoweza kupata kitu cha kula,” mtu yule alisema. Alionyesha nyumba ya njano yenye paa la buluu. “Natumaini utaenda pale kupata chakula kidogo?” Thomas aliuliza. Magozwe alimwangalia yule mtu, kisha akaiangalia ile nyumba. “Labda,” akasema, halafu akaondoka.


跟住落嚟嘅幾個月,班流浪男仔慢慢識咗湯瑪斯。佢好鍾意同人傾偈,特別係啲無家可歸嘅人。湯瑪斯會聽人哋講自己嘅經歷。佢雖然睇落去好嚴肅,但係非常之有耐心、有禮貌,尊重他人。班男仔開始每逢中午就去藍頂黃牆屋度搵嘢食。

Miezi iliyofuata, wavulana wale wa mtaani walizoea kumwona Thomas hapa na pale. Alipenda kuzungumza na watu, hasa walioishi mitaani. Thomas alisikiliza simulizi za maisha ya watu. Alikuwa makini na mwenye subira, na hakuwa na kiburi wala dharau. Baadhi ya wavulana walianza kwenda kwenye ile nyumba ya njano na buluu ili kupata chakula cha mchana.


有日,瑪哥威正坐喺行人路上面睇故仔書,湯瑪斯就坐低喺隔籬。湯瑪斯問佢:「呢本書講咩嘢故仔呢?」瑪哥威答佢就話:「係一個男仔成為飛機師嘅故仔。」湯瑪斯又問佢:「男仔叫咩嘢名呢?」瑪哥威好細聲噉就話:「我唔知呀,我都唔識字。」

Magozwe alikuwa amekaa kando ya barabara akiangalia kitabu chake cha picha Thomas alipokaa pembeni mwake. “Hadithi hiyo inahusu nini?” Thomas akauliza. “Inahusu mvulana aliyekuja kuwa rubani,” Magozwe akajibu. “Jina lake ni nani?” Thomas akauliza. “Sijui, siwezi kusoma,” Magozwe akasema kwa sauti ya chini.


當佢哋再次見面嘅時候,瑪哥威開始同湯瑪斯講自己嘅經歷,佢叔叔係點樣對待佢,佢又係點樣逃離佢叔叔屋企。湯瑪斯乜都冇講,亦都冇講瑪哥威應該點做,但係佢成日都會好留心噉樣聽佢講嘢。有時佢哋會一路喺藍頂黃牆屋度食嘢,一路傾吓偈。

Walipokutana, Magozwe alianza kumsimulia Thomas maisha yake. Alimwelezea kuhusu mjomba wake na sababu zilizomfanya atoroke. Thomas hakuongea sana, wala hakumwambia Magozwe nini cha kufanya, bali alisikiliza kwa makini kila mara. Wakati mwingine waliongea wakiwa wanakula kwenye ile nyumba yenye paa la buluu.


瑪哥威十歲生日嗰陣時,湯瑪斯送咗本新故仔書俾佢,書入面係講一個鄉下男仔成為足球員嘅故仔。湯瑪斯講過好多次呢個故仔俾瑪哥威聽。有一日,湯瑪斯就話:「我覺得你應該去返學,去識字。你覺得呢?」湯瑪斯就話佢知道一個地方,可以俾細蚊仔住喺嗰便返學。

Mnamo mwaka wa kumi wa kuzaliwa kwa Magozwe, Thomas alimzawadia kitabu kipya cha hadithi. Ilikuwa ni hadithi inayohusu mvulana wa kijijini aliyekuja kuwa mcheza mpira maarufu. Thomas alimsomea Magozwe hadithi hiyo mara nyingi, mpaka siku moja akasema, “Nafikiri wakati umewadia wa kwenda shule kujifunza kusoma. Unaonaje?” Thomas alieleza kwamba anajua sehemu ambayo watoto wanaweza kuishi na kwenda shule.


瑪哥威諗諗吓去新地方生活,返學。但係,如果佢阿叔講得啱呢,如果佢真係蠢到學乜都冇用嘅話點算呀?如果喺新地方,佢又要捱打嘅話點算呀?佢有少少驚,心諗:「可能我整定要瞓街㗎。」

Magozwe alifikiria kuhusu sehemu hii mpya, na kuhusu kwenda shule. Itakuwaje kama mjomba wake alikuwa sahihi kwamba alikuwa mjinga kiasi cha kutoweza kujifunza chochote? Itakuwaje kama watampiga sehemu hii mpya? Aliogopa. “Labda ni heri kuendelea kuishi mtaani,” aliwaza.


佢將自己嘅諗法話俾咗湯瑪斯聽。湯瑪斯對佢循循善誘,終於說服咗佢,喺新地方生活一定會更加好。

Alimshirikisha Thomas juu ya hofu aliyokuwa nayo. Baada ya muda Thomas alimhakikishia kwamba maisha yatakuwa bora huko sehemu mpya.


瑪哥威搬到咗新屋企,新屋企嘅屋頂係綠色嘅。佢同兩個男仔住埋同一間房。間屋入面一共仲有十個細蚊仔。同佢哋一齊住嘅係思思阿姨同佢老公,仲有三隻狗,一隻貓,一隻老山羊。

Kwa hiyo Magozwe alihamia kwenye chumba katika nyumba yenye paa la kijani. Alikaa chumba kimoja na wavulana wengine wawili. Kwa ujumla kulikuwa na watoto kumi walioishi kwenye nyumba ile. Waliishi pamoja na Shangazi Cissy na mume wake, mbwa watatu, paka mmoja, na mbuzi aliyezeeka.


瑪哥威開始讀書,佢遇到唔少困難,好難先趕上班同學,有時佢幾乎想要放棄。但係佢每次諗返故仔書入面嘅飛機師同足球員,佢都會堅持落嚟,就好似佢哋一樣。

Magozwe alianza shule na ilikuwa ngumu. Alikuwa na mengi ya kujifunza. Mara nyingine alitaka kukata tamaa. Lakini aliwaza kuhusu rubani na mcheza mpira kwenye vitabu vya hadithi. Kama wao, hakukata tamaa.


有一日,瑪哥威正喺間藍頂屋後院度睇緊書,湯瑪斯就嚟到坐喺隔籬。湯瑪斯問佢:「呢本書講咩嘢故仔呢?」瑪哥威答佢就話:「係一個男仔成為老師嘅故仔。」湯瑪斯又問佢:「個男仔叫咩嘢名呢?」瑪哥威笑笑口噉話:「佢叫瑪哥威。」

Magozwe alikuwa amekaa uani kwenye nyumba yenye paa la kijani, akisoma kitabu cha hadithi cha shule. Thomas alikuja na kukaa kando yake. “Hadithi inahusu nini?” Thomas akauliza. “Inahusu mvulana aliyekuja kuwa mwalimu,” Magozwe akajibu. “Jina lake ni nani?” akauliza Thomas. “Jina lake ni Magozwe,” Magozwe akasema kwa tabasamu.


Written by: Lesley Koyi
Illustrated by: Wiehan de Jager
Translated by: dohliam
Read by: Zoe Lam
Language: Cantonese
Level: Level 5
Source: Magozwe from African Storybook
Creative Commons License
This work is licensed under a Creative Commons Attribution 4.0 International License.
Read more level 5 stories:
Options
Back to stories list Download PDF