Download PDF
Back to stories list

Magozwe Magozwe

Written by Lesley Koyi

Illustrated by Wiehan de Jager

Translated by Arlene Avila

Read by La Trinidad Mina

Language Tagalog

Level Level 5

Narrate full story

Reading speed

Autoplay story


Sa mataong lungsod ng Nairobi, malayo sa mga tahanang mapagmahal, may mga batang walang matuluyan. Sila ang mga batang kalye. Lahat sila ay lalaki at tanggap nila kung ano man ang hatid ng araw sa kanilang buhay. Pagkagising sa umaga, nililigpit nila ang banig pagkatapos matulog sa malamig na bangketa. Sinisindihan nila ang basura para mabawasan ang ginaw. Kasama nila sa Magozwe, ang pinakabata.

Kwenye jiji la Nairobi lenye pilikapilika nyingi, mbali na malezi ya nyumbani, paliishi kikundi cha wavulana wasiokuwa na makwao. Waliipokea kila siku ijayo kama ilivyo. Siku moja asubuhi, walikuwa wanakusanya virago vyao baada ya kulala kwenye baridi kando ya barabara. Ili kuondoa baridi, walikoka moto kwa kutumia takataka. Miongoni mwa kikundi hicho cha wavulana alikuwepo Magozwe. Alikuwa ni mdogo kuliko wote.


Limang taon pa lang si Magozwe nang mamatay ang kanyang mga magulang. Tumira siya sa kanyang tiyo na walang pakialam sa kanya. Hindi niya pinapakain ng mabuti si Magozwe at binibigyan niya ito ng mahihirap na trabaho.

Wakati wazazi wa Magozwe walipofariki, alikuwa na miaka mitano tu. Alienda kuishi na mjomba wake. Mjomba hakumjali Magozwe. Hakumpa chakula cha kutosha. Alimfanyisha kazi nyingi nzito.


Bugbog ang inaabot ni Magozwe kung siya ay nagtatanong o nagrereklamo. Bugbog uli ang inabot niya nung banggitin niya ang tungkol sa pag-aaral, “Hindi ka matututo kasi tanga ka.” Lumayas si Magozwe pagkatapos ng tatlong taong paghihirap at siya ay sumama sa mga batang kalye.

Magozwe alipolalamika au kuuliza, mjomba wake alimpiga. Magozwe alipouliza kama ataweza kwenda shule, mjomba wake alimpiga na kumwambia, “Wewe ni mjinga, hutaweza kujifunza chochote.” Baada ya miaka mitatu ya kunyanyaswa, Magozwe alitoroka kwa mjomba wake. Akaanza kuishi mtaani.


Mahirap ang buhay at lahat sila nagkukumahog makahanap lang ng makakain. Minsan hinuhuli sila ng pulis, minsan naman ay nabubugbog. Walang nag-aalaga sa kanila pag sila’y nagkakasakit. Umaasa lang sila sa maliit na kita sa pagpapalimos at pangangalakal. Lalo silang naghihirap pag nanghahamon ng away ang ibang grupo ng batang kalye, makuha lang ang gustong teritoryo.

Maisha ya mtaani yalikuwa magumu na wavulana wengi walipambana kila siku ili wapate chakula tu. Mara nyingine walikamatwa, mara nyingine walipigwa. Walipougua, kulikuwa hakuna mtu wa kuwasaidia. Kikundi kilitegemea hela ndogo ndogo walizopata kwa kuomba omba, na kwa kuuza plastiki na vitu kuukuu. Maisha yalikuwa magumu zaidi hasa kwa sababu ya vita dhidi ya vikundi pinzani vilivyotaka kudhibiti baadhi ya maeneo ya jiji.


Isang araw, nakakita si Magozwe ng gula-gulanit na libro sa basura. Nilinis niya ang libro at nilagay iyon sa kanyang sako. Araw-araw, tinitingnan lang niya ang mga larawan sa libro sapagka’t hindi siya marunong magbasa.

Siku moja Magozwe alipokuwa anachakura kwenye mapipa ya takataka, alikuta kitabu cha hadithi kilichokuwa kimechakaa. Aliondoa uchafu kwenye kitabu na kukiweka ndani ya mfuko wake. Kila siku baada ya hapo, alikitoa kitabu na kuangalia picha. Hakujua kusoma maandishi.


Kinuwento ng mga larawan ang buhay ng isang batang lalaki na naging piloto at pinangarap ni Magozwe maging piloto. Minsan, iniisip niya na siya ang bata sa libro.

Picha zilikuwa zinaongelea hadithi ya mvulana ambaye alikuja kuwa rubani. Magozwe aliota kuwa rubani. Mara nyingine alifikiria kwamba yeye ni yule mvulana kwenye hadithi.


Isang malamig na araw, nakatayo si Magozwe sa kalye namamalimos nang lumapit sa kanya ang isang mama. “Magandang umaga. Ako si Tomas. Malapit lang dito ang pinagtatrabahuhan ko at namimigay kami ng libreng pagkain.” Tinuro niya ang dilaw na bahay na may asul na bubong. “Sana makadaan ka doon.” Tiningnan lang ni Magozwe ang mama at ang bahay. “Titingnan ko,” sabi niya sabay talikod.

Kulikuwa na baridi na Magozwe alikuwa amesimama barabarani akiomba omba. Mtu alimkaribia. “Hujambo? Naitwa Thomas. Nafanya kazi karibu na hapa, mahali unapoweza kupata kitu cha kula,” mtu yule alisema. Alionyesha nyumba ya njano yenye paa la buluu. “Natumaini utaenda pale kupata chakula kidogo?” Thomas aliuliza. Magozwe alimwangalia yule mtu, kisha akaiangalia ile nyumba. “Labda,” akasema, halafu akaondoka.


Unti-unting nasanay ang mga batang kalye kay Tomas. Mahilig makipagkuwentuhan si Tomas sa kanila. Gusto niyang marinig ang istorya ng kanilang buhay. Pasensiyoso, seryoso at magalang–ganun si Tomas. Nagsimulang pumunta ang ibang bata sa dilaw at asul na bahay tuwing oras ng tanghalian.

Miezi iliyofuata, wavulana wale wa mtaani walizoea kumwona Thomas hapa na pale. Alipenda kuzungumza na watu, hasa walioishi mitaani. Thomas alisikiliza simulizi za maisha ya watu. Alikuwa makini na mwenye subira, na hakuwa na kiburi wala dharau. Baadhi ya wavulana walianza kwenda kwenye ile nyumba ya njano na buluu ili kupata chakula cha mchana.


Isang araw, nakaupo si Magozwe sa bangketa habang nakatingin sa kanyang libro. Tumabi si Tomas, “Ano ang kuwento ng libro?” tanong niya. “Tungkol sa isang bata na naging piloto,” sagot ni Magozwe. “Anong pangalan niya?” tanong ni Tomas. “Hindi ko alam, e. Hindi ako marunong magbasa,” sabi ni Magozwe.

Magozwe alikuwa amekaa kando ya barabara akiangalia kitabu chake cha picha Thomas alipokaa pembeni mwake. “Hadithi hiyo inahusu nini?” Thomas akauliza. “Inahusu mvulana aliyekuja kuwa rubani,” Magozwe akajibu. “Jina lake ni nani?” Thomas akauliza. “Sijui, siwezi kusoma,” Magozwe akasema kwa sauti ya chini.


Sinabi ni Magozwe ang kuwento ng kanyang buhay kay Tomas. Kinuwento niya ang tiyo at kung bakit siya naglayas. Tahimik lang na nakinig si Tomas sa lahat ng sinasabi ni Magozwe. Naging madalas ang kuwentuhan nila. Isang araw, nag-usap sila habang kumakain sa loob ng bahay na dilaw at asul.

Walipokutana, Magozwe alianza kumsimulia Thomas maisha yake. Alimwelezea kuhusu mjomba wake na sababu zilizomfanya atoroke. Thomas hakuongea sana, wala hakumwambia Magozwe nini cha kufanya, bali alisikiliza kwa makini kila mara. Wakati mwingine waliongea wakiwa wanakula kwenye ile nyumba yenye paa la buluu.


Sa ika-sampung kaarawan ni Magozwe, binigyan siya ni Tomas ng bagong libro. Ito rin ay puno ng larawan at ang kuwento ay tungkol sa isang batang taga-nayon na naging tanyag na manlalaro ng soccer. Madalas pinapabasa ni Magozwe kay Tomas ang libro kaya sabi ni Tomas, “Panahon na para matuto kang magbasa. Kailangan mo na pumasok sa eskuwela. Ano sa palagay mo?” Dinagdag ni Tomas na may mga bahay na tumatanggap at nagpapa-aral sa mga batang kalye.

Mnamo mwaka wa kumi wa kuzaliwa kwa Magozwe, Thomas alimzawadia kitabu kipya cha hadithi. Ilikuwa ni hadithi inayohusu mvulana wa kijijini aliyekuja kuwa mcheza mpira maarufu. Thomas alimsomea Magozwe hadithi hiyo mara nyingi, mpaka siku moja akasema, “Nafikiri wakati umewadia wa kwenda shule kujifunza kusoma. Unaonaje?” Thomas alieleza kwamba anajua sehemu ambayo watoto wanaweza kuishi na kwenda shule.


Nag-isip si Magozwe nang matagal. Paano kung tama ang sabi ni tiyo? Paano kung totoo ngang bobo siya? Paano kung mabugbog siya uli? Natakot si Magozwe. “Mas ok na siguro ako dito sa kalye,” sabi niya sa sarili.

Magozwe alifikiria kuhusu sehemu hii mpya, na kuhusu kwenda shule. Itakuwaje kama mjomba wake alikuwa sahihi kwamba alikuwa mjinga kiasi cha kutoweza kujifunza chochote? Itakuwaje kama watampiga sehemu hii mpya? Aliogopa. “Labda ni heri kuendelea kuishi mtaani,” aliwaza.


Nabanggit niya kay Tomas ang kanyang mga takot. Tinulungan siya ni Tomas na magtiwala uli at umasa na magiging maayos ang lahat.

Alimshirikisha Thomas juu ya hofu aliyokuwa nayo. Baada ya muda Thomas alimhakikishia kwamba maisha yatakuwa bora huko sehemu mpya.


Isang araw, lumipat na nga si Magozwe sabay ng dalawang batang lalaki sa isang bahay na berde ang bubong. Sampu lahat ang mga batang alaga ni Tita Cissy at asawa nito. Meron din silang tatlong aso, isang pusa at isang matandang kambing.

Kwa hiyo Magozwe alihamia kwenye chumba katika nyumba yenye paa la kijani. Alikaa chumba kimoja na wavulana wengine wawili. Kwa ujumla kulikuwa na watoto kumi walioishi kwenye nyumba ile. Waliishi pamoja na Shangazi Cissy na mume wake, mbwa watatu, paka mmoja, na mbuzi aliyezeeka.


Nagsimulang mag-aral si Magozwe at sa una medyo nahirapan siya. Naisipan niya minsan na sumuko. Pero naaalala niya ang piloto at ang soccer player sa libro at nabubuhayan siya uli ng loob.

Magozwe alianza shule na ilikuwa ngumu. Alikuwa na mengi ya kujifunza. Mara nyingine alitaka kukata tamaa. Lakini aliwaza kuhusu rubani na mcheza mpira kwenye vitabu vya hadithi. Kama wao, hakukata tamaa.


Isang araw, nakaupo si Magozwe sa harap ng bahay nagbabasa ng libro. Dumating si Tomas, “Ano ang kuwento ng libro?” “Tungkol sa isang bata na naging titser,” sagot ni Magozwe. “Ano’ng pangalan ng bata?” tanong ni Tomas. “Magozwe,” sagot ni Magozwe na may ngiti.

Magozwe alikuwa amekaa uani kwenye nyumba yenye paa la kijani, akisoma kitabu cha hadithi cha shule. Thomas alikuja na kukaa kando yake. “Hadithi inahusu nini?” Thomas akauliza. “Inahusu mvulana aliyekuja kuwa mwalimu,” Magozwe akajibu. “Jina lake ni nani?” akauliza Thomas. “Jina lake ni Magozwe,” Magozwe akasema kwa tabasamu.


Written by: Lesley Koyi
Illustrated by: Wiehan de Jager
Translated by: Arlene Avila
Read by: La Trinidad Mina
Language: Tagalog
Level: Level 5
Source: Magozwe from African Storybook
Creative Commons License
This work is licensed under a Creative Commons Attribution 4.0 International License.
Read more level 5 stories:
Options
Back to stories list Download PDF