Download PDF
Back to stories list

Gadoo Dammaqajelchitu Kisasi cha Kiongozi

Written by Zulu folktale

Illustrated by Wiehan de Jager

Translated by Demoze Degefa

Language Oromo

Level Level 4

Narrate full story The audio for this story is currently not available.


Seenaan kuni wa’ee Nagade, dammaqajelchituu; fi nama sassattu dardar tokko kan Ginigilee jedhamaniti. Gaftokko Yeroo Gingileen admsa dhaqe, waamicha Nagade dhagahe. Afaan Gingilee damma yaade jennaan bayee hawwee. Gingileen dhabbatee dhageefate lafaa simbirron suni jiritu barbaade. Simbirroon xiqqoon sunis, “chitiik-chitiik-chitiik” jechaa muka tokko irra gara biraati cetee. Chitiik, chitiik jechuu dhifte Gingileen duuka dhufu isaa mirkaneesuf.

Hii ni hadithi ya Ngede, ambaye ni ndege mpenda asali, na mvulana mmoja mlafi anayeitwa Gingile. Siku moja Gingile alipokuwa akiwinda alisikia mwito wa Ngede. Kinywa chake kilianza kutokwa mate kwa kufikiria asali. Alisimama, akasikiliza na kuangalia vizuri hadi alipomwona yule ndege akiwa ametua kwenye matawi yaliyokuwa juu ya kichwa chake. “Chitik-chitik-chitik,” yule ndege mdogo alitatarika aliporuka na kutua kwenye mti mmoja hadi mwingine, na mwingine tena. “Chitik-chitik-chitik,” aliita, huku akinyamaza na kuhakikisha kwamba Gingile alikuwa amemfuata.


Sa’ati walakka booda, hundii isaani mukka gudda tokko jala gahan. Nagade akka nama maratee dameewan gubbaa figee. Boodas damee tokko gubbaa ta’ee mataa isaa gara Gingilee qabee, “Asii kunooti, Kootu as, maltu sitursiise?” Gingileen garauu kannisa tokko ille hinagaree garu Nagade amane.

Baada ya nusu saa, walifika kwenye mti wa matini. Ngede aliruka kama mwenda wazimu kutoka tawi moja hadi jingine. Kisha alitulia kwenye tawi moja na kupindua kichwa chake akimwangalia Gingile kana kwamba anasema, “Ipo hapa! Njoo sasa! Kwa nini unachukua muda mrefu?” Gingile hakuweza kuona nyuki wowote kutoka chini ya mti, lakini alimwamini Ngede.


Kanaafu Gingileen eboo isaa mukaa jala ka’ee, mukaa goggogaa waltti qabee ibidda qabsiee. Yeroo ibiddichi sirriti boba’uu mukaa dheraa tokko ibiddicaha kessa ka’ee. Mukti kuni aara bayee umuudhan beekama. Amma mukaa sana koruu calqabee, mukaa gara qnaqee hinqbnee afaanti qabatee.

Kwa hivyo Gingile aliweka mkuki wake alioutumia kuwinda chini ya mti, akakusanya vijiti vilivyokauka na kuwasha moto mdogo. Moto ulipokuwa ukiwaka vizuri, alichomeka kijiti kirefu kwenye moto. Mti huu ulijulikana kwa kutoa moshi mwingi ulipokuwa unaungua. Alianza kukwea mti huku akishika kijiti kwa meno upande usiofuka moshi.


Yerooma sana sagaale kannisa dhagahee. Kannisonni sunis holqaa mukaa kessaa bahan. Gingileen yeroo holqaa kannisaa bira gahu aara sana gara afaan holqichaati qabee. Kannisnis aarani holqichaa kessaa badani deeman. Aaraa sana waan jibbaniif baqatani sokkan. Otto hinsokkin dura garuu Ginglee hiddani turan.

Muda mfupi baadaye, aliweza kusikia sauti ya nyuki wenye harakati nyingi ikivuma. Walikuwa wakiingia na kutoka kwenye upenyo wa mti, yaani mzinga wao. Gingile alipoufikia mzinga, alisukuma ile kuni ya moto ndani ya ule upenyo. Nyuki waliharakisha kutoka ndani wakiwa na hasira na uchungu. Waliruka na kwenda mbali kwa sababu hawakupenda moshi – lakini walifanya hivyo baada ya kumuuma Gingile kwa uchungu!


Yeroo kannisonni alaati bahan, Gingileen harka isaa gara holqati galche. Biddeen damma walalaa bayee qabu argate. Damma sana sutaa jedhee korojooti naqatee sutaa jedhe mukkarra bu’ee.

Nyuki walipokuwa nje, Gingile aliingiza mikono yake ndani ya kiota. Alitoa kipande kikubwa cha sega kilichokuwa kinadondoka urojo mzito wa asali, na kilichojaa wadudu weupe wanene. Aliiweka taratibu ndani ya mkoba aliokuwa nao na kuanza kushuka kutoka mtini.


Nagadeen waan Gingileen hojjacha turee ilaala ture. Innis damma gudda isaa akka kennati eggachaa ture. Nagadenis damee irraa dameet utaalun gara lafaati dhihate. Dhummarrati Gingileen lafa gahe. Nagadeenis dhakaa gubbaa ta’ee kennaa isaa eggatee.

Ngede alishuhudia kila kitu Gingile alichofanya. Alikuwa anamsubiri abakishe kiasi kidogo cha asali kama shukurani kwa Kiongozi. Ngede aliruka kutoka tawi hadi tawi huku akikaribia chini. Mwishowe Gingile alifika chini ya mti. Ngede alitua kwenye mwamba karibu na mvulana huyo na kusubiri zawadi yake.


Hata’u maale Gingileen ibdda dhamsee, eboo isaa qabatee Sibirricha dhisee gara mana isaa deeme. Nagaden aaree, akan jedheen. “vik-tor. vik-torr!” Gingileen dhaabbate, ijaa ittibasee akkan jedheen, “damma xinnoo barbaadee, ati hiriyaa kiyya moo? Hojii maraa anumatu hojaatee. Damma kana maliifan siqooda?” Sana booda nideeme. Nagaden bayee aaree! Hali kun garu mit. Garuu gaddo itti bahuu danda’aa.

Lakini Gingile alizima moto, akachukua mkuki wake na kuanza safari kwenda nyumbani bila kumjali ndege yule. Ngede aliita kwa hasira, “USH-ndi! USH-ndi!” Gingile alisimama, akamkodolea macho yule ndege kisha akacheka kwa sauti. “Unataka asali kidogo, rafiki yangu? Ha! Lakini ni mimi niliyefanya kazi yote pamoja na kuumwa na nyuki. Kwa nini nikugawie hii asali tamu?” Baada ya kusema hivyo, aliondoka na kwenda zake. Ngede alikasirika sana! Hivi sivyo alivyostahili kutendewa! Ila atalipiza kisasi.


Turbaan bayee booda, gaftokko Gingileen sagaale damma himaa Nagadee dhagahe. Damma walalaa sana yadatee Nagade dukaa bu’ee. Eega Gingilee karaa ittiagarsisuu calqabee booda boqachudhaf mukaa tokko jala ta’ee. “Ahha, holqii kannisaa asi jiraachu qaba” jdhee yadee. Hatataman mukaa aara isaa qabsifatee mukkicha koruu calqabe. Nagaden ta’ee ilaala ture.

Siku moja baada ya majuma machache, Gingile tena alisikia mwito wa asali kutoka kwa Ngede. Aliikumbuka asali tamu, na kwa hamu alimfuata ndege yule kwa mara nyingine. Baada ya kumwongoza Gingile pembeni mwa msitu, Ngede alisimama na kupumzika chini ya mti wa mwavuli. “Ahh,” Gingile aliwaza. “Lazima mzinga umo ndani ya mti huu.” Kwa haraka aliwasha moto wake na kuanza kukwea mti huku akibeba kuni iliyotoa moshi katika meno yake. Ngede alikaa na kuangalia tu.


Gingileen mukkicha yeroo koruu garu sagaale kannisa dhagahu dhisuun isaa isa dinqisiisa ture.” Holqichii gaddii fagachuu qaba jedhe yadee.” Damee biraa irra koree. Garuu holqaa kannisaa otu hinta’in fula qeransaa arge. Qeransichis hiribaa isaa irra waan dammaqeef bayee aare. Ija fi afaan ishee banudhaan ilkaan ishee hamam akka cimaa ta’e agarsiste.

Gingile alipopanda, alishangaa kwa nini hakusikia sauti ya nyuki. “Pengine mzinga umo ndani zaidi katika mti,” alifikiria. Alipanda tena juu ya tawi jingine. Lakini badala ya mzinga, alijikuta uso kwa uso na chui! Chui alikuwa na hasira sana kwa sababu usingizi wake ulikuwa umekatizwa. Aliyafanya macho yake kuwa madogo, akaufungua mdomo wake na kuonyesha meno yake makubwa na makali.


Otoo qeransichi itti hin utaalin, Gingileen dafee mukarra bu’ee. Otoo muddamu damee tokko qolee lafati akka maleeti kufee caphee. Akka carraa ta’e qeransci hirribarra hinkanee wantureef. isa dukaa hinbunee. Nagaden, dammaqajelchitun, gaddod Gingileeti batee. Gingileenis barnoota bayee argate.

Kabla ya Chui kumvamia Gingile, alishuka chini haraka. Katika haraka hiyo, aliteleza na kuanguka kwa kishindo huku akiumia mguu wake. Alirukaruka akienda kwa haraka alivyoweza. Kwa bahati nzuri, Chui alikuwa bado amelala kwa hivyo hakumfukuza. Ngede, Kiongozi alikuwa amelipiza kisasi chake na Gingile alikuwa amejifunza funzo lake.


Ijoolen Gingilee yeroo seenaa Nagadee dhagahan bayee simbirroo kana kabajan. Yeroo damma muraan hundaa, damma bayee dammaqajelchitudhaf dhissan.

Kwa hivyo wakati watoto wa Gingile wanaposikia hadithi ya Ngede, wanamheshimu yule ndege. Kila wanapotoa asali, huhakikisha kwamba wanamwachia Kiongozi fungu kubwa!


Written by: Zulu folktale
Illustrated by: Wiehan de Jager
Translated by: Demoze Degefa
Language: Oromo
Level: Level 4
Source: The Honeyguide's revenge from African Storybook
Creative Commons License
This work is licensed under a Creative Commons Attribution 3.0 International License.
Options
Back to stories list Download PDF