Download PDF
Back to stories list

Magozwe Magozwe

Written by Lesley Koyi

Illustrated by Wiehan de Jager

Translated by Bether Mwale Moyo

Read by Christine Mwanza

Language Nyanja

Level Level 5

Narrate full story The audio for this story is currently not available.


Mu tauni ya Nairobi, kutali nama banja, kunali kunkala anyamata analibe mabanja. Anangonkala mwa siku pa siku. Kuseni kwina, anyamata anali kulonga mpasa zao pambuyo pogona pampepo mumbali mwa museu. Kusewenzesa vinyalala, anayasa moto kuti asangenewe mpepo. Pagulu la anyamata ili panali Magozwe. Iye ndiye anali wamung’ono.

Kwenye jiji la Nairobi lenye pilikapilika nyingi, mbali na malezi ya nyumbani, paliishi kikundi cha wavulana wasiokuwa na makwao. Waliipokea kila siku ijayo kama ilivyo. Siku moja asubuhi, walikuwa wanakusanya virago vyao baada ya kulala kwenye baridi kando ya barabara. Ili kuondoa baridi, walikoka moto kwa kutumia takataka. Miongoni mwa kikundi hicho cha wavulana alikuwepo Magozwe. Alikuwa ni mdogo kuliko wote.


Pomwe makolo ake Magozwe anamwalila, iye anali na zaka cabe kumi. Ndipo anayenda kunkala na amalume ake. Amalume ake sanatayeko nzelu kwa mwana. Sanali kumupasa cakudwa cokwanila Magozwe. Ndipo anali kugwilisa ncito zambili.

Wakati wazazi wa Magozwe walipofariki, alikuwa na miaka mitano tu. Alienda kuishi na mjomba wake. Mjomba hakumjali Magozwe. Hakumpa chakula cha kutosha. Alimfanyisha kazi nyingi nzito.


Ngati Magozwe wafunsa mwina wadandaula, amalume ake anali kumumenya. Pomwe anafunsa kuti ayende kusukulu amalume ake anamumenya nanena nati “Ndiwe cisilu kwambili sungapunzile kalikonse.” Patapita zaka zitatu zosungiwa mozuzindwa, Magozwe anataba kucoka pa nyumba pa amalume ake. Ndipo anayamba kunkala pa museu.

Magozwe alipolalamika au kuuliza, mjomba wake alimpiga. Magozwe alipouliza kama ataweza kwenda shule, mjomba wake alimpiga na kumwambia, “Wewe ni mjinga, hutaweza kujifunza chochote.” Baada ya miaka mitatu ya kunyanyaswa, Magozwe alitoroka kwa mjomba wake. Akaanza kuishi mtaani.


Kunali kovuta kunkala kwa pa museu ndipo anyamata ambili anali kuvutika masiku onse kupeza cakudya. Masiku ena anamenyedwa, ntawi zina anagwilidwa na apolisi. Akadwala kunalibe muntu owatandiza. Ndalama zomwe anapeza mukupempa pempa, kugulisa ma pulasitiki na zina, ndiye ndalama zomwe zinali kuwatandizila. Umoyo unavutilako cifukwa magulu ena a anyamata anali kufuna kulanda malo osiyana siyana mu tauni.

Maisha ya mtaani yalikuwa magumu na wavulana wengi walipambana kila siku ili wapate chakula tu. Mara nyingine walikamatwa, mara nyingine walipigwa. Walipougua, kulikuwa hakuna mtu wa kuwasaidia. Kikundi kilitegemea hela ndogo ndogo walizopata kwa kuomba omba, na kwa kuuza plastiki na vitu kuukuu. Maisha yalikuwa magumu zaidi hasa kwa sababu ya vita dhidi ya vikundi pinzani vilivyotaka kudhibiti baadhi ya maeneo ya jiji.


Siku lina pamene Magozwe anali kusakila-sakila muvinyalala, anapeza buku lina losila long’ambika. Anacosako madoti ndipo analiika mu saka. Siku lililonse lokonkapo, anacosa buku ndipo anayamba kulangana vitunzi tunzi mu buku. Sanali kuziwa kuwelenga mau.

Siku moja Magozwe alipokuwa anachakura kwenye mapipa ya takataka, alikuta kitabu cha hadithi kilichokuwa kimechakaa. Aliondoa uchafu kwenye kitabu na kukiweka ndani ya mfuko wake. Kila siku baada ya hapo, alikitoa kitabu na kuangalia picha. Hakujua kusoma maandishi.


Vitunzi tunzi vinalangiza munyamata omwe anakula kunkala oyendesa ndeke. Magozwe analota na muzuba momwe, kunkala oyendesa ndeke. Ntawi zina anaziona kuti ndiye wamene anali munyamata wamubuku.

Picha zilikuwa zinaongelea hadithi ya mvulana ambaye alikuja kuwa rubani. Magozwe aliota kuwa rubani. Mara nyingine alifikiria kwamba yeye ni yule mvulana kwenye hadithi.


Kunali kozizila ndipo Magozwe anaimilila pa museu kupempa-pempa. Muzibambo wina anabwela pafupi naye. “Bwanji, ndine Thomas. Nisewenza pafupa napano, pamalo pamene ungapeze cakudya,” anakamba. Anasonta nyumba yacikasu, ya malata yobilibila. “Niziwa uzayenda kuti utengeko cakudya?” anafunsa. Magozwe analangana muzibambo nalangana nyumba. “Kapena nizayenda,” anayanka, ndipo anacokapo.

Kulikuwa na baridi na Magozwe alikuwa amesimama barabarani akiomba omba. Mtu alimkaribia. “Hujambo? Naitwa Thomas. Nafanya kazi karibu na hapa, mahali unapoweza kupata kitu cha kula,” mtu yule alisema. Alionyesha nyumba ya njano yenye paa la buluu. “Natumaini utaenda pale kupata chakula kidogo?” Thomas aliuliza. Magozwe alimwangalia yule mtu, kisha akaiangalia ile nyumba. “Labda,” akasema, halafu akaondoka.


Panapita Mwezi, ndipo anyamata alibe mabanja anali kuonana na Thomas. Thomas anali kukonda kukamba na antu makamaka antu onkala pa museu. Thomas ananvesela nkani za antu awa. Anali wacidwi ndipo wonkazikika mutima, ndiponso sanataye ulemu. Anyamata ena anayamba kuyenda kunyumba yacikasu ya malata obilibila, kutenga cakudya muzuba.

Miezi iliyofuata, wavulana wale wa mtaani walizoea kumwona Thomas hapa na pale. Alipenda kuzungumza na watu, hasa walioishi mitaani. Thomas alisikiliza simulizi za maisha ya watu. Alikuwa makini na mwenye subira, na hakuwa na kiburi wala dharau. Baadhi ya wavulana walianza kwenda kwenye ile nyumba ya njano na buluu ili kupata chakula cha mchana.


Magozwe anali nkale mumbali mwa museu alangana vitunzi tunzi mu buku yake pamene Thomas anabwela nankala pafupi naye. “Ikamba cani nkani?” anafunsa Thomas. “Ikamba pali munyamata amena anankala oyendesa ndeke,” anayanka Magozwe. “Nindani zina munyamata?” anafunsa Thomas. “Kaya, siniziba kuwelenga,” anayanka Magozwe mwacisinsi.

Magozwe alikuwa amekaa kando ya barabara akiangalia kitabu chake cha picha Thomas alipokaa pembeni mwake. “Hadithi hiyo inahusu nini?” Thomas akauliza. “Inahusu mvulana aliyekuja kuwa rubani,” Magozwe akajibu. “Jina lake ni nani?” Thomas akauliza. “Sijui, siwezi kusoma,” Magozwe akasema kwa sauti ya chini.


Pomwe anakumana, Magozwe anayamba kuuza Thomas, nkani za umoyo wake. Anamuuza za mwamene anatawila kucoka kwa amalume ake. Thomas sanakambe kwambili, ndipo sanauze Magozwe vocita koma anamvesela mwacidwi. Ntawi zina Magozwe na Thomas anakambilana pamene anali kudya munyumba ya malata obilibila.

Walipokutana, Magozwe alianza kumsimulia Thomas maisha yake. Alimwelezea kuhusu mjomba wake na sababu zilizomfanya atoroke. Thomas hakuongea sana, wala hakumwambia Magozwe nini cha kufanya, bali alisikiliza kwa makini kila mara. Wakati mwingine waliongea wakiwa wanakula kwenye ile nyumba yenye paa la buluu.


Pomwe Magozwe anali pafupi nakukwanisa zaka kumi, Thomas anamupasa buku. Buku inali pali munyamata wa mumunzi wamene anakula kunkala womenya bola wozibika kwambili. Thomas anamuwelengela Magozwi kwambili, mpaka siku lina anakamba nati, “Niganiza kuti uyambe kuyenda ku sukulu, kuti ukapunzile kuwelenga. Uganizapo bwanji?” Thomas anakamba kuti anali kuziba malo kumene ana angayende kunkala ndiponso kupunzila kwameneko.

Mnamo mwaka wa kumi wa kuzaliwa kwa Magozwe, Thomas alimzawadia kitabu kipya cha hadithi. Ilikuwa ni hadithi inayohusu mvulana wa kijijini aliyekuja kuwa mcheza mpira maarufu. Thomas alimsomea Magozwe hadithi hiyo mara nyingi, mpaka siku moja akasema, “Nafikiri wakati umewadia wa kwenda shule kujifunza kusoma. Unaonaje?” Thomas alieleza kwamba anajua sehemu ambayo watoto wanaweza kuishi na kwenda shule.


Magozwe anaganizila za kumalo uko ndiponse zoyenda ku sukulu. Nanga kapena amalume ake anakamba zoona kuti anali cisilu kwambili ndipo sangapunzile kalikonse? Nanga ngati bamumenya uku kumalo kwinangu? Anayopa. “Kapena cilibwino kupitiliza kunkala pa museu,” anaganiza.

Magozwe alifikiria kuhusu sehemu hii mpya, na kuhusu kwenda shule. Itakuwaje kama mjomba wake alikuwa sahihi kwamba alikuwa mjinga kiasi cha kutoweza kujifunza chochote? Itakuwaje kama watampiga sehemu hii mpya? Aliogopa. “Labda ni heri kuendelea kuishi mtaani,” aliwaza.


Anamuuza Thomas kuti anali na manta. Thomas anamusimikizila kuti, azankala na umoyo wabwina uku kumalo.

Alimshirikisha Thomas juu ya hofu aliyokuwa nayo. Baada ya muda Thomas alimhakikishia kwamba maisha yatakuwa bora huko sehemu mpya.


Ndipo Magozwe anapita kunkala mu cipinda mu nyumba ya malata amusipu. Anankala na anyamata ena awili mu cipinda. Pamozi anali anyamata kumi amene anali kunkala pamozi mu nyumba. Pamozi na a Anti Cissy na amuna ao, magalu atatu, ka kiti na mbuzi yokalamba.

Kwa hiyo Magozwe alihamia kwenye chumba katika nyumba yenye paa la kijani. Alikaa chumba kimoja na wavulana wengine wawili. Kwa ujumla kulikuwa na watoto kumi walioishi kwenye nyumba ile. Waliishi pamoja na Shangazi Cissy na mume wake, mbwa watatu, paka mmoja, na mbuzi aliyezeeka.


Magozwe anayamba sukulu ndipo inali yovuta. Nivambili vamene anali kufunikila kuziwa kuti alingane na anzake. Ntawi zina anali kufuna kuleka. Koma anaganizila oyendesa ndeke na omenya bola a muma buku ake. Monga aja anyamata amumabuku, sanaleke.

Magozwe alianza shule na ilikuwa ngumu. Alikuwa na mengi ya kujifunza. Mara nyingine alitaka kukata tamaa. Lakini aliwaza kuhusu rubani na mcheza mpira kwenye vitabu vya hadithi. Kama wao, hakukata tamaa.


Magozwe anali nkale panja panyumba ya malata a musipu, awelenga buku lake lakusukulu, pamene Thomas anabwela nonkala pafupi pake. “Ikamba cani nkani?” anafunsa Thomas. “Ikamba pali munyamata amene anankala mupunzisi,” anayanka Magozwe. “Nindani zina munyamata?” anafunsa Thomas. “Zina lake ni Magozwe,” anayanka Magozwe mosekelela.

Magozwe alikuwa amekaa uani kwenye nyumba yenye paa la kijani, akisoma kitabu cha hadithi cha shule. Thomas alikuja na kukaa kando yake. “Hadithi inahusu nini?” Thomas akauliza. “Inahusu mvulana aliyekuja kuwa mwalimu,” Magozwe akajibu. “Jina lake ni nani?” akauliza Thomas. “Jina lake ni Magozwe,” Magozwe akasema kwa tabasamu.


Written by: Lesley Koyi
Illustrated by: Wiehan de Jager
Translated by: Bether Mwale Moyo
Read by: Christine Mwanza
Language: Nyanja
Level: Level 5
Source: Magozwe from African Storybook
Creative Commons License
This work is licensed under a Creative Commons Attribution 4.0 International License.
Read more level 5 stories:
Options
Back to stories list Download PDF