Download PDF
Back to stories list

マゴズヴェ Magozwe

Written by Lesley Koyi

Illustrated by Wiehan de Jager

Translated by Rie TAKANUMA

Read by Yumi Okano

Language Japanese

Level Level 5

Narrate full story

Reading speed

Autoplay story


ナイロビの都会の喧騒の中、家庭でのあたたかい暮らしにはほど遠く、ホームレスの少年たちが暮らしていました。彼らは毎日を来るがまま暮らしていました。とある朝、男の子たちは舗装された冷たい道の上で起きて、布団代わりのマットを片付けていました。寒さを追い払おうと、ごみくずで火を燃やしました。少年たちの中に、マゴズウェという最年少の男の子がいました。

Kwenye jiji la Nairobi lenye pilikapilika nyingi, mbali na malezi ya nyumbani, paliishi kikundi cha wavulana wasiokuwa na makwao. Waliipokea kila siku ijayo kama ilivyo. Siku moja asubuhi, walikuwa wanakusanya virago vyao baada ya kulala kwenye baridi kando ya barabara. Ili kuondoa baridi, walikoka moto kwa kutumia takataka. Miongoni mwa kikundi hicho cha wavulana alikuwepo Magozwe. Alikuwa ni mdogo kuliko wote.


マゴズウェの両親が亡くなった時、彼はたった5歳でした。彼はおじさんのところでお世話になることになりました。おじさんはマゴズウェの面倒を見ませんでした。おじさんはマゴズヴェに十分に食べ物を与えず、辛い仕事をたくさん与えました。

Wakati wazazi wa Magozwe walipofariki, alikuwa na miaka mitano tu. Alienda kuishi na mjomba wake. Mjomba hakumjali Magozwe. Hakumpa chakula cha kutosha. Alimfanyisha kazi nyingi nzito.


マゴズウェが不満や疑問を言うと、おじさんは彼を叩きました。ある時、マゴズウェが学校に行けるか尋ねると、おじさんは彼を殴り「お前は愚か者すぎて何も学べない」と言いました。それから3年後、マゴズヴェはおじさんの元から逃げ出しました。そして路上で生活を始めたのです。

Magozwe alipolalamika au kuuliza, mjomba wake alimpiga. Magozwe alipouliza kama ataweza kwenda shule, mjomba wake alimpiga na kumwambia, “Wewe ni mjinga, hutaweza kujifunza chochote.” Baada ya miaka mitatu ya kunyanyaswa, Magozwe alitoroka kwa mjomba wake. Akaanza kuishi mtaani.


路上生活は困難で、大多数の少年たちは毎日食べ物を得るだけでもとても苦労していました。彼らは時には逮捕され、時には殴られました。病気になった時、助けてくれる人は誰もいません。彼らは物乞いや、プラスティックや他のリサイクル可能なものを販売して得たわずかなお金に頼っていました。街の地区を支配したいライバルグループとの闘いがあったので、生活はより一層厳しいものでした。

Maisha ya mtaani yalikuwa magumu na wavulana wengi walipambana kila siku ili wapate chakula tu. Mara nyingine walikamatwa, mara nyingine walipigwa. Walipougua, kulikuwa hakuna mtu wa kuwasaidia. Kikundi kilitegemea hela ndogo ndogo walizopata kwa kuomba omba, na kwa kuuza plastiki na vitu kuukuu. Maisha yalikuwa magumu zaidi hasa kwa sababu ya vita dhidi ya vikundi pinzani vilivyotaka kudhibiti baadhi ya maeneo ya jiji.


ある日、マゴズヴェがごみ箱を漁っていると、古いボロボロの物語の本を見つけました。本の汚れを綺麗にし、袋の中に入れました。それから毎日、彼はその本を取り出し、絵を眺めました。彼は文字の読み方を知らなかったのです。

Siku moja Magozwe alipokuwa anachakura kwenye mapipa ya takataka, alikuta kitabu cha hadithi kilichokuwa kimechakaa. Aliondoa uchafu kwenye kitabu na kukiweka ndani ya mfuko wake. Kila siku baada ya hapo, alikitoa kitabu na kuangalia picha. Hakujua kusoma maandishi.


その本の絵には、大人になってパイロットになる少年の物語が描かれていました。マゴズヴェはパイロットになる空想にふけりました。時々、彼はその物語の少年自身だと想像したのでした。

Picha zilikuwa zinaongelea hadithi ya mvulana ambaye alikuja kuwa rubani. Magozwe aliota kuwa rubani. Mara nyingine alifikiria kwamba yeye ni yule mvulana kwenye hadithi.


寒さの中、マゴズヴェは道に立ち、物乞いをしていました。とある男性が彼のところに歩み寄ってきました。男は「はじめまして、私はトーマスと申します。私はこの近く、あなたが何か食べ物を貰えるところで働いています」と言いました。彼は青い屋根の黄色い家を指さしました。「良ければ、あちらに行って何か食べませんか?」と尋ねました。マゴズヴェは男を見、そして家を見ました。そして「たぶん」と言い、立ち去りました。

Kulikuwa na baridi na Magozwe alikuwa amesimama barabarani akiomba omba. Mtu alimkaribia. “Hujambo? Naitwa Thomas. Nafanya kazi karibu na hapa, mahali unapoweza kupata kitu cha kula,” mtu yule alisema. Alionyesha nyumba ya njano yenye paa la buluu. “Natumaini utaenda pale kupata chakula kidogo?” Thomas aliuliza. Magozwe alimwangalia yule mtu, kisha akaiangalia ile nyumba. “Labda,” akasema, halafu akaondoka.


数か月もすると、ホームレスの少年たちはトーマスのそばにいることに慣れてきました。トーマスは人々、とりわけ路上で生活する人々と話をするのが好きでした。トーマスは人々の人生を聴いていました。彼は真剣で、そして我慢強く、決して無礼な態度や人を尊重しないような態度を取りませんでした。少年のうち何人かは、青い屋根の黄色い家へ、お昼にご飯を貰いに行きだしました。

Miezi iliyofuata, wavulana wale wa mtaani walizoea kumwona Thomas hapa na pale. Alipenda kuzungumza na watu, hasa walioishi mitaani. Thomas alisikiliza simulizi za maisha ya watu. Alikuwa makini na mwenye subira, na hakuwa na kiburi wala dharau. Baadhi ya wavulana walianza kwenda kwenye ile nyumba ya njano na buluu ili kupata chakula cha mchana.


トーマスがマゴズヴェの隣に座ったとき、彼は舗道に座り、絵本を見ていました。トーマスは「何のお話ですか?」と聞きました。「パイロットになる男の子のお話だよ」とマゴズヴェは答えました。「少年の名前はなんと言うのですか?」トーマスは聞きました。「分からないよ。僕は読めないんだ」マゴズヴェは静かに言いました。

Magozwe alikuwa amekaa kando ya barabara akiangalia kitabu chake cha picha Thomas alipokaa pembeni mwake. “Hadithi hiyo inahusu nini?” Thomas akauliza. “Inahusu mvulana aliyekuja kuwa rubani,” Magozwe akajibu. “Jina lake ni nani?” Thomas akauliza. “Sijui, siwezi kusoma,” Magozwe akasema kwa sauti ya chini.


マゴズヴェとトーマスが会っているとき、マゴズヴェはトーマスに、彼の人生を語り始めました。彼のおじさんと、なぜ彼は逃げ出したのかというお話でした。トーマスは多くを語らず、マゴズヴェに何をすべきかも言わず、いつも注意深く話を聴いていました。時々、青い屋根の黄色い家で食事をしながら、彼らは話をしました。

Walipokutana, Magozwe alianza kumsimulia Thomas maisha yake. Alimwelezea kuhusu mjomba wake na sababu zilizomfanya atoroke. Thomas hakuongea sana, wala hakumwambia Magozwe nini cha kufanya, bali alisikiliza kwa makini kila mara. Wakati mwingine waliongea wakiwa wanakula kwenye ile nyumba yenye paa la buluu.


マゴズヴェの10歳の誕生日付近に、トーマスは彼に新しい物語の本をあげました。それはある村の少年が有名なサッカー選手になるお話でした。トーマスはマゴズヴェに、ある日こう伝えるまで、そのお話を何度も読んであげました。「そろそろ学校に行って、読み方を習った方がよいと思います。どう思いますか?」トーマスは、子供たちが泊まり、学校に行ける場所を知っていると説明しました。

Mnamo mwaka wa kumi wa kuzaliwa kwa Magozwe, Thomas alimzawadia kitabu kipya cha hadithi. Ilikuwa ni hadithi inayohusu mvulana wa kijijini aliyekuja kuwa mcheza mpira maarufu. Thomas alimsomea Magozwe hadithi hiyo mara nyingi, mpaka siku moja akasema, “Nafikiri wakati umewadia wa kwenda shule kujifunza kusoma. Unaonaje?” Thomas alieleza kwamba anajua sehemu ambayo watoto wanaweza kuishi na kwenda shule.


マゴズヴェはその新しい場所や学校に行くことについて考えました。もし彼のおじさんが正しくて、自分が愚か者すぎて何も学べなかったら?もし新しい場所にいる人たちが自分のことを叩いたら?彼は恐ろしかったのです。「きっと路上生活を続けた方がいいんだろうな」と彼は思いました。

Magozwe alifikiria kuhusu sehemu hii mpya, na kuhusu kwenda shule. Itakuwaje kama mjomba wake alikuwa sahihi kwamba alikuwa mjinga kiasi cha kutoweza kujifunza chochote? Itakuwaje kama watampiga sehemu hii mpya? Aliogopa. “Labda ni heri kuendelea kuishi mtaani,” aliwaza.


彼はトーマスに不安を打ち明けました。トーマスは時間をかけて、新しい場所での生活の方がよくなると、マゴズヴェを安心させました。

Alimshirikisha Thomas juu ya hofu aliyokuwa nayo. Baada ya muda Thomas alimhakikishia kwamba maisha yatakuwa bora huko sehemu mpya.


そしてマゴズヴェは緑の屋根の家の一部屋に移り住みました。他の2人の少年たちとルームシェアをしました。その家には全部で10人の子供たちが住んでいました。スィシーおばさんとその旦那さん、犬3匹、猫1匹、年老いた山羊1蹄も一緒でした。

Kwa hiyo Magozwe alihamia kwenye chumba katika nyumba yenye paa la kijani. Alikaa chumba kimoja na wavulana wengine wawili. Kwa ujumla kulikuwa na watoto kumi walioishi kwenye nyumba ile. Waliishi pamoja na Shangazi Cissy na mume wake, mbwa watatu, paka mmoja, na mbuzi aliyezeeka.


マゴズヴェは学校に行き始めましたが、難しいものでした。追いつくためにたくさんのことをしました。時折、彼は諦めたくなりましたが、物語の本のパイロットやサッカー選手を考えました。彼らのように、マゴズヴェは諦めませんでした。

Magozwe alianza shule na ilikuwa ngumu. Alikuwa na mengi ya kujifunza. Mara nyingine alitaka kukata tamaa. Lakini aliwaza kuhusu rubani na mcheza mpira kwenye vitabu vya hadithi. Kama wao, hakukata tamaa.


マゴズヴェは緑の屋根の家の庭に座り、学校から持ってきた物語の本を読んでいました。トーマスがやってきて、マゴズヴェの隣に座りました。「何のお話ですか?」トーマスは尋ねました。「先生になる少年のお話だよ」マゴズヴェは答えました。「その少年の名前は?」トーマスは聞きました。「彼の名前はマゴズヴェだよ」マゴズヴェは笑顔で言いました。

Magozwe alikuwa amekaa uani kwenye nyumba yenye paa la kijani, akisoma kitabu cha hadithi cha shule. Thomas alikuja na kukaa kando yake. “Hadithi inahusu nini?” Thomas akauliza. “Inahusu mvulana aliyekuja kuwa mwalimu,” Magozwe akajibu. “Jina lake ni nani?” akauliza Thomas. “Jina lake ni Magozwe,” Magozwe akasema kwa tabasamu.


Written by: Lesley Koyi
Illustrated by: Wiehan de Jager
Translated by: Rie TAKANUMA
Read by: Yumi Okano
Language: Japanese
Level: Level 5
Source: Magozwe from African Storybook
Creative Commons License
This work is licensed under a Creative Commons Attribution 4.0 International License.
Read more level 5 stories:
Options
Back to stories list Download PDF