Download PDF
Back to stories list

साकीमा का गाना Wimbo wa Sakima

Written by Ursula Nafula

Illustrated by Peris Wachuka

Translated by Nandani

Language Hindi

Level Level 3

Narrate full story The audio for this story is currently not available.


साकीमा अपने माता-पिता और अपनी चार साल की बहन के साथ रहता था। वे एक अमीर आदमी की ज़मीन पर रहते थे। उनका घास फूस का घर पेड़ों की कतार के आखिर में था।

Sakima aliishi na wazazi wake na dada yake wa miaka minne. Waliishi katika shamba la mtu tajiri. Nyumba yao ya nyasi ilikuwa mwisho wa safu ya miti iliyopendeza.


जब साकीमा तीन साल का था तब वह बीमार पड़ा और उसने अपनी आँखों की रोशनी खो दी। साकीमा में बहुत गुण थे।

Sakima alipokuwa na umri wa miaka mitatu, aliugua na kupoteza uwezo wa kuona. Hata hivyo, Sakima alikuwa mvulana mwenye kipaji.


साकीमा ऐसे कई काम कर सकता था जो अन्य छः वर्षीय बालक नहीं कर सकते थे। उदाहरण के लिए, वह गाँव के बुजुर्गों के साथ बैठता और महत्त्वपूर्ण मुद्दों पर चर्चा करता।

Sakima alitenda mambo mengi ambayo wavulana wengine wa umri wake hawakufanya. Kwa mfano, aliketi na watu wazima na kujadili mambo muhimu.


साकीमा के माता-पिता अमीर आदमी के घर पर काम करते थे। वे घर से जल्दी चले जाते और देर से घर लौटते। वे साकीमा को उसकी छोटी बहन के साथ छोड़कर जाते थे।

Wazazi wa Sakima walifanya kazi katika nyumba ya yule tajiri. Walitoka nyumbani asubuhi na mapema na kurudi jioni. Sakima aliachwa na dada yake.


साकीमा को गाना गाना पसंद था। एक दिन उसकी माँ ने उससे पूछा “तुमने ये गाने कहाँ से सीखे, साकीमा?”

Sakima alipenda kuimba nyimbo. Siku moja mama yake alimuuliza, “Sakima, unajifunza nyimbo hizi kutoka wapi?”


साकीमा ने जवाब दिया “ये ऐसे ही आते हैं, माँ। मैं इनको अपने मन में सुनता हूँ और फिर इन्हें गाता हूँ”

Sakima alimjibu, “Nazisikia akilini mwangu kisha naziimba.”


साकीमा को अपनी छोटी बहन के लिए गाना पसंद था, विशेषकर तब जब उसे भूख लगती थी।

Sakima alipenda kumwimbia mdogo wake hasa akihisi njaa. Dada yake alimsikiliza na kucheza.


“क्या तुम इसे बार-बार गा सकते हो,” उसकी बहन उससे प्रार्थना करती। साकीमा मान जाता और बार-बार उसके लिए गाता।

“Naomba uimbe tena na tena, Sakima,” mdogo wake alimsihi. Sakima alikubali na kuimba mara nyingine.


एक शाम जब उसके माता पिता वापस घर आए, वे बहुत चुप थे। साकीमा जान गया कि कुछ ठीक नहीं है।

Jioni moja, wazazi wake waliporudi nyumbani, walikuwa kimya sana. Sakima alijua kwamba lazima kulikuwa na jambo baya.


“क्या हुआ, माँ, पिताजी?” साकीमा ने पूछा। साकीमा को पता चला कि अमीर आदमी का लड़का खो गया है। वह आदमी बहुत ही उदास और अकेला था।

“Kuna shida gani, mama, baba?” Sakima aliuliza. Sakima aligundua kwamba mwana wa tajiri wao alikuwa amepotea. Tajiri alihuzunika na kuwa na upweke mkubwa.


“मैं उनके लिए गा सकता हूँ। वे फिर से खुश हो जायेंगे,” साकीमा ने अपने माता-पिता से कहा। पर उसके माता पिता ने मना कर दिया। “वे बहुत अमीर है। तुम केवल एक अंधे लड़के हो। क्या तुम सोचते हो कि तुम्हारा गाना उनकी मदद करेगा?”

“Labda atafurahi tena nikimwimbia,” Sakima aliwaambia wazazi wake. Wazazi wake walidharau wazo lake. “Yeye ni tajiri sana. Wewe ni mvulana asiyeona. Unadhani wimbo wako utamsaidia?”


जो भी हो, साकीमा ने हार नहीं मानी। उसकी छोटी बहन ने उसका साथ दिया। वह बोली, “जब मैं भूखी होती हूँ तो साकीमा के गाने सुनकर मैं बहुत संतुष्ट और खुश महसूस करती हूँ। वे अमीर आदमी को भी सुकून देंगे।”

Hata hivyo, Sakima hakukata tamaa. Mdogo wake alimpa moyo. Alisema, “Nyimbo za Sakima hunituliza mimi nikiwa na njaa. Zitamtuliza tajiri vile vile.”


अगले दिन, साकीमा ने अपनी छोटी बहन से कहा कि वह उसे अमीर आदमी के घर ले चले।

Siku iliyofuata, Sakima alimwomba mdogo wake amwongoze hadi kwenye nyumba ya tajiri.


वह एक बड़ी खिड़की के नीचे खड़ा हो गया और उसने अपना पसंदीदा गाना गाना शुरू कर दिया। थोड़ी ही देर में, वह बड़ा आदमी बड़ी खिड़की के बाहर झाँक कर देखने लगा।

Alisimama chini ya dirisha moja kubwa na kuanza kuimba wimbo wake alioupenda. Pole pole, kichwa cha tajiri kilionekana dirishani.


साकीमा का मधुर गायन सुनकर सभी कर्मचारियों ने अपना काम बीच में ही रोक दिया। लेकिन एक आदमी बोला, “अब तक कोई भी मालिक को दिलासा नहीं दे सका। क्या यह अंधा लड़का यह सोचता है कि वह उनको दिलासा दे पायेगा?”

Wafanyakazi waliacha kazi zao. Wakasikiliza wimbo mzuri wa Sakima. Hata hivyo, mwanamume mmoja alisema, “Hakuna aliyefaulu kumtuliza bwana. Je, huyu mvulana asiyeona anafikiri atamtuliza?”


साकीमा ने अपना गाना खत्म किया और जाने के लिए मुड़ा। लेकिन अमीर आदमी बाहर निकल और बोला, “कृपया दोबारा गाओ”।

Sakima alipomaliza kuimba wimbo wake alianza kuondoka. Tajiri alitoka nje kwa haraka na kusema, “Tafadhali, imba tena.”


उसी समय, दो आदमी एक पालकी ले कर आए। उन्हें अमीर आदमी का बेटा घायल सड़क के किनारे पड़ा मिला था।

Wakati huo huo, watu wawili walikuja wakiwa wamembeba mtu kwenye machela. Walimkuta mwana wa tajiri akiwa amechapwa na kuachwa kando ya barabara.


अमीर आदमी अपने लड़के को दोबारा देख कर बहुत खुश हो गया। उसने साकीमा को दिलासा देने के लिए पुरस्कार दिया। वह अपने बेटे और साकीमा को अस्पताल ले गया ताकि साकीमा फिर से देख सके।

Tajiri alifurahi sana kumwona mwana wake tena. Alimzawadia Sakima kwa kumliwaza. Aliwapeleka mwanawe na Sakima hosipitali ili Sakima aweze kusaidiwa kuona tena.


Written by: Ursula Nafula
Illustrated by: Peris Wachuka
Translated by: Nandani
Language: Hindi
Level: Level 3
Source: Sakima's song from African Storybook
Creative Commons License
This work is licensed under a Creative Commons Attribution 4.0 International License.
Options
Back to stories list Download PDF