Download PDF
Back to stories list

Magozwe Magozwe

Written by Lesley Koyi

Illustrated by Wiehan de Jager

Translated by Penelope Vos

Language Esperanto

Level Level 5

Narrate full story The audio for this story is currently not available.


En la okupata urbo Najrobo, malproksime de zorgema vivo hejme, loĝis grupo de senhejmaj knaboj. Ili bonvenigis ĉiun tagon kiel ajn ĝi venis. Unu mateno, la knaboj pakis siajn matojn post dormado sur malvarmaj trotuaroj. Por forpeli la malvarmon ili ekbruligis fajron per rubo. Inter la grupo de knaboj estis Magozwe. Li estis la plej juna.

Kwenye jiji la Nairobi lenye pilikapilika nyingi, mbali na malezi ya nyumbani, paliishi kikundi cha wavulana wasiokuwa na makwao. Waliipokea kila siku ijayo kama ilivyo. Siku moja asubuhi, walikuwa wanakusanya virago vyao baada ya kulala kwenye baridi kando ya barabara. Ili kuondoa baridi, walikoka moto kwa kutumia takataka. Miongoni mwa kikundi hicho cha wavulana alikuwepo Magozwe. Alikuwa ni mdogo kuliko wote.


Kiam la gepatroj de Magozwe mortis, li havis nur kvin jarojn. Li iris loĝi kun sia onklo. Ĉi tiu viro ne zorgis pri la infano. Li ne donis al Magozwe sufiĉe da manĝaĵo. Li igis la knabon multe labori.

Wakati wazazi wa Magozwe walipofariki, alikuwa na miaka mitano tu. Alienda kuishi na mjomba wake. Mjomba hakumjali Magozwe. Hakumpa chakula cha kutosha. Alimfanyisha kazi nyingi nzito.


Se Magozwe plendis aŭ demandis, lia onklo batis lin. Kiam Magozwe petis, ĉu li povas iri al lernejo, lia onklo batis lin kaj diris: “Vi estas tro stulta por lerni ion ajn.” Post tri jaroj de ĉi tiu traktado Magozwe forkuris de sia onklo. Li ekloĝis surstrate.

Magozwe alipolalamika au kuuliza, mjomba wake alimpiga. Magozwe alipouliza kama ataweza kwenda shule, mjomba wake alimpiga na kumwambia, “Wewe ni mjinga, hutaweza kujifunza chochote.” Baada ya miaka mitatu ya kunyanyaswa, Magozwe alitoroka kwa mjomba wake. Akaanza kuishi mtaani.


Strata vivo estis malfacila kaj la plej multo de la knaboj luktis ĉiutage nur por akiri manĝon. Foje ili estis arestitaj, foje batitaj. Kiam ili estis malsanaj, estis neniu por helpi. La grupo dependis de la malmulta mono, kiun ili akiris de almozpetado, kaj de vendado de plastoj kaj aliaj reciklado. La vivo estis eĉ pli malfacila pro bataloj kun rivalaj grupoj, kiuj volis regi partojn de la urbo.

Maisha ya mtaani yalikuwa magumu na wavulana wengi walipambana kila siku ili wapate chakula tu. Mara nyingine walikamatwa, mara nyingine walipigwa. Walipougua, kulikuwa hakuna mtu wa kuwasaidia. Kikundi kilitegemea hela ndogo ndogo walizopata kwa kuomba omba, na kwa kuuza plastiki na vitu kuukuu. Maisha yalikuwa magumu zaidi hasa kwa sababu ya vita dhidi ya vikundi pinzani vilivyotaka kudhibiti baadhi ya maeneo ya jiji.


Iun tagon, dum Magozwe trarigardis la rubujojn, li trovis malnovan ĉifonan rakontolibron. Li purigis la malpuraĵon de ĝi kaj metis ĝin en sian sakon. Ĉiutage poste li elprenis la libron kaj rigardis la bildojn. Li ne sciis kiel legi la vortojn.

Siku moja Magozwe alipokuwa anachakura kwenye mapipa ya takataka, alikuta kitabu cha hadithi kilichokuwa kimechakaa. Aliondoa uchafu kwenye kitabu na kukiweka ndani ya mfuko wake. Kila siku baada ya hapo, alikitoa kitabu na kuangalia picha. Hakujua kusoma maandishi.


La bildoj rakontis la historion de knabo, kiu fariĝis piloto. Magozwe revus esti piloto. Foje, li imagis, ke li estas la knabo en la rakonto.

Picha zilikuwa zinaongelea hadithi ya mvulana ambaye alikuja kuwa rubani. Magozwe aliota kuwa rubani. Mara nyingine alifikiria kwamba yeye ni yule mvulana kwenye hadithi.


Malvarmis kaj Magozwe staris sur la vojo almozpetante. Viro iris al li. “Saluton, mi estas Tomaso. Mi laboras proksime ĉi tie, en loko, kie vi povas havi ion por manĝi,” diris la viro. Li indikis flavan domon kun blua tegmento. “Mi esperas, ke vi iros tien por iom manĝi?” li demandis. Magozwe rigardis la viron, kaj poste la domon. “Eble,” li diris, kaj foriris.

Kulikuwa na baridi na Magozwe alikuwa amesimama barabarani akiomba omba. Mtu alimkaribia. “Hujambo? Naitwa Thomas. Nafanya kazi karibu na hapa, mahali unapoweza kupata kitu cha kula,” mtu yule alisema. Alionyesha nyumba ya njano yenye paa la buluu. “Natumaini utaenda pale kupata chakula kidogo?” Thomas aliuliza. Magozwe alimwangalia yule mtu, kisha akaiangalia ile nyumba. “Labda,” akasema, halafu akaondoka.


Dum la sekvaj monatoj, la senhejmaj knaboj kutimis vidi Tomason. Li ŝatis paroli kun homoj, precipe homoj surstrate. Tomaso aŭskultis la rakontojn pri la vivoj de homoj. Li estis serioza kaj pacienca, neniam malĝentila aŭ senrespekta. Iuj el la knaboj komencis iri al la flava kaj blua domo por manĝi tagmeze.

Miezi iliyofuata, wavulana wale wa mtaani walizoea kumwona Thomas hapa na pale. Alipenda kuzungumza na watu, hasa walioishi mitaani. Thomas alisikiliza simulizi za maisha ya watu. Alikuwa makini na mwenye subira, na hakuwa na kiburi wala dharau. Baadhi ya wavulana walianza kwenda kwenye ile nyumba ya njano na buluu ili kupata chakula cha mchana.


Magozwe sidis sur la trotuaro rigardante sian bildlibron, kiam Tomaso sidiĝis apud li. “Pri kio temas la rakonto?” demandis Tomaso. “Temas pri knabo, kiu fariĝas piloto,” respondis Magozwe. “Kiel nomiĝas la knabo?” demandis Tomaso. “Mi ne scias, mi ne scias legi,” diris Magozwe mallaŭte.

Magozwe alikuwa amekaa kando ya barabara akiangalia kitabu chake cha picha Thomas alipokaa pembeni mwake. “Hadithi hiyo inahusu nini?” Thomas akauliza. “Inahusu mvulana aliyekuja kuwa rubani,” Magozwe akajibu. “Jina lake ni nani?” Thomas akauliza. “Sijui, siwezi kusoma,” Magozwe akasema kwa sauti ya chini.


Kiam ili renkontiĝis, Magozwe komencis rakonti sian propran historion al Tomaso. Ĝi estis la rakonto de lia onklo kaj kial li forkuris. Tomaso ne multe parolis, kaj li ne diris al Magozwe kion fari, sed li ĉiam aŭskultis atente. Foje ili parolis dum ili manĝis ĉe la domo kun la blua tegmento.

Walipokutana, Magozwe alianza kumsimulia Thomas maisha yake. Alimwelezea kuhusu mjomba wake na sababu zilizomfanya atoroke. Thomas hakuongea sana, wala hakumwambia Magozwe nini cha kufanya, bali alisikiliza kwa makini kila mara. Wakati mwingine waliongea wakiwa wanakula kwenye ile nyumba yenye paa la buluu.


Proksime al la deka naskiĝtago de Magozwe, Tomaso donis al li novan rakontolibron. Ĝi estis rakonto pri vilaĝa knabo, kiu kreskis esti fama futbalisto. Tomaso legis tiun rakonton al Magozwe multfoje, ĝis unu tago li diris, “Mi pensas, ke venis la tempo, por vi iri al lernejo kaj lerni kiel legi. Kion vi pensas?” Tomaso klarigis, ke li scias pri loko, kie infanoj povas loĝi kaj iri al lernejo.

Mnamo mwaka wa kumi wa kuzaliwa kwa Magozwe, Thomas alimzawadia kitabu kipya cha hadithi. Ilikuwa ni hadithi inayohusu mvulana wa kijijini aliyekuja kuwa mcheza mpira maarufu. Thomas alimsomea Magozwe hadithi hiyo mara nyingi, mpaka siku moja akasema, “Nafikiri wakati umewadia wa kwenda shule kujifunza kusoma. Unaonaje?” Thomas alieleza kwamba anajua sehemu ambayo watoto wanaweza kuishi na kwenda shule.


Magozwe pensis pri ĉi tiu nova loko, kaj pri irado al lernejo. Kaj kio se lia onklo pravus kaj li estus tro stulta por lerni ion ajn? Kio se ili batus lin ĉe ĉi tiu nova loko? Li timis. “Eble estas pli bone resti loĝanta sur la strato,” li pensis.

Magozwe alifikiria kuhusu sehemu hii mpya, na kuhusu kwenda shule. Itakuwaje kama mjomba wake alikuwa sahihi kwamba alikuwa mjinga kiasi cha kutoweza kujifunza chochote? Itakuwaje kama watampiga sehemu hii mpya? Aliogopa. “Labda ni heri kuendelea kuishi mtaani,” aliwaza.


Li dividis siajn timojn kun Tomaso. Post iom da tempo la viro trankviligis la knabon, ke la vivo povus esti pli bona ĉe la nova loko.

Alimshirikisha Thomas juu ya hofu aliyokuwa nayo. Baada ya muda Thomas alimhakikishia kwamba maisha yatakuwa bora huko sehemu mpya.


Kaj tiel Magozwe translokiĝis en ĉambron en domo kun verda tegmento. Li dividis la ĉambron kun du aliaj knaboj. Entute estis dek infanoj loĝantaj en tiu domo. Kune kun onklino Cissy kaj ŝia edzo, tri hundoj, kato, kaj maljuna kapro.

Kwa hiyo Magozwe alihamia kwenye chumba katika nyumba yenye paa la kijani. Alikaa chumba kimoja na wavulana wengine wawili. Kwa ujumla kulikuwa na watoto kumi walioishi kwenye nyumba ile. Waliishi pamoja na Shangazi Cissy na mume wake, mbwa watatu, paka mmoja, na mbuzi aliyezeeka.


Magozwe komencis lernejon kaj ĝi estis malfacila. Li havis multon por lerni post malfrua komenco. Foje li volis rezigni. Sed li pensis pri la piloto kaj la futbalisto en la rakontolibroj. Kiel ili, li ne rezignis.

Magozwe alianza shule na ilikuwa ngumu. Alikuwa na mengi ya kujifunza. Mara nyingine alitaka kukata tamaa. Lakini aliwaza kuhusu rubani na mcheza mpira kwenye vitabu vya hadithi. Kama wao, hakukata tamaa.


Magozwe sidis en la korto ĉe la domo kun la verda tegmento, legante rakontolibron de la lernejo. Tomaso venis kaj sidis apud li. “Pri kio temas la rakonto?” demandis Tomaso. “Temas pri knabo, kiu fariĝas instruisto,” respondis Magozwe. “Kiel nomiĝas la knabo?” demandis Tomaso. “Li nomiĝas Magozwe,” diris Magozwe ridetante.

Magozwe alikuwa amekaa uani kwenye nyumba yenye paa la kijani, akisoma kitabu cha hadithi cha shule. Thomas alikuja na kukaa kando yake. “Hadithi inahusu nini?” Thomas akauliza. “Inahusu mvulana aliyekuja kuwa mwalimu,” Magozwe akajibu. “Jina lake ni nani?” akauliza Thomas. “Jina lake ni Magozwe,” Magozwe akasema kwa tabasamu.


Written by: Lesley Koyi
Illustrated by: Wiehan de Jager
Translated by: Penelope Vos
Language: Esperanto
Level: Level 5
Source: Magozwe from African Storybook
Creative Commons License
This work is licensed under a Creative Commons Attribution 4.0 International License.
Read more level 5 stories:
Options
Back to stories list Download PDF