Download PDF
Back to stories list

Anansi und die Weisheit Anansi na hekima

Written by Ghanaian folktale

Illustrated by Wiehan de Jager

Translated by Anna Westpfahl

Read by Jula Eberth

Language German

Level Level 3

Narrate full story

Reading speed

Autoplay story


Vor langer, langer Zeit wussten die Menschen gar nichts. Sie wussten nicht, wie man Pflanzen anbaut, wie man Tücher webt, oder wie man Eisenwerkzeuge herstellt. Der Gott Nyame oben im Himmel hatte die ganze Weisheit der Welt. Er bewahrte sie sicher in einem Tontopf auf.

Hapo zamani za kale, watu hawakujua chochote. Hawakujua kupanda mimea, hawakujua kushona nguo, wala hawakujua kuunda zana za chuma. Nyame, mungu aliyekuwa mbinguni, ndiye aliyekuwa mwenye hekima zote za dunia. Alihifadhi hekima hiyo kwenye chungu cha udongo.


Eines Tages beschloss Nyame, den Tontopf Anansi zu geben. Jedes Mal, wenn Anansi in den Topf schaute, lernte er etwas Neues. Es war so aufregend!

Siku moja, Nyame aliamua kumpa Anansi chungu hicho cha hekima. Kila Anansi alipotazama ndani ya chungu cha udongo, alijifunza jambo jipya. Alifurahi sana!


Gierig dachte Anansi: „Ich werde den Topf sicher im Gipfel eines Baumes aufbewahren. So habe ich ihn ganz für mich allein!“ Er spann einen langen Zwirn, wickelte ihn um den Tontopf und band ihn um seinen Bauch. Er begann, den Baum hinaufzuklettern. Aber es war schwer den Baum so hinaufzuklettern, da der Topf ständig gegen seine Knie stieß.

Anansi mlafi alinong’ona moyoni, “Nitakificha chungu hiki juu ya mti mrefu ili nikifaidi mwenyewe.” Akasokota uzi mrefu na kuuzungusha kwenye chungu. Kisha, akajifunga tumboni. Akaanza kupanda kwenye mti. Lakini ilikuwa vigumu kupanda kwenye mti huku chungu kikimgonga magotini kila mara.


Die ganze Zeit hatte Anansis junger Sohn unten am Baum gestanden und ihm zugeschaut: „Wäre es nicht leichter, wenn du dir den Topf stattdessen auf den Rücken bindest?“ Anansi versuchte es mit dem Topf auf dem Rücken und es ging in der Tat viel besser.

Wakati huo wote, mwanawe alikuwa amesimama chini ya ule mti akimtazama baba yake. Akamwambia, “Baba, si ingekuwa rahisi kupanda endapo ungekifungia chungu mgongoni?” Basi Anansi akajaribu kukifungia chungu kilichojaa hekima mgongoni mwake, na kweli ikawa rahisi zaidi.


Im Nu erklomm Anansi die Baumspitze. Aber dann hielt er inne und dachte: „Ich soll derjenige mit der ganzen Weisheit sein und eben war mein Sohn schlauer als ich!“ Dies verärgerte Anansi so sehr, dass er den Tontopf vom Baum hinunter warf.

Punde tu alipofika juu ya mti, aliwaza, “Natakiwa kuwa ndiye mwenye hekima zote, lakini hapa mwanangu ndiye mwenye akili kuliko mimi.” Anansi alikasirishwa sana kiasi kwamba alikitupa kile chungu chini ya mti.


Am Boden zerbrach er in viele Stücke. Die Weisheit gehörte nun allen. Und so lernten die Menschen, Landwirtschaft zu betreiben, Tücher zu weben, Eisenwerkzeuge herzustellen und alles andere, was wir heute wissen.

Chungu kilivunjika vipandevipande pale chini. Hekima zikawa za bure kwa mtu yeyote kujichukulia. Na hivyo ndivyo watu walivyojifunza kulima, kushona nguo, kuunda zana za chuma, na mambo yote mengine ambayo watu wanajua kuyafanya.


Written by: Ghanaian folktale
Illustrated by: Wiehan de Jager
Translated by: Anna Westpfahl
Read by: Jula Eberth
Language: German
Level: Level 3
Source: Anansi and Wisdom from African Storybook
Creative Commons License
This work is licensed under a Creative Commons Attribution 3.0 International License.
Options
Back to stories list Download PDF