Download PDF
Back to stories list

Inkonde shaba maama Ndizi za bibi

Written by Ursula Nafula

Illustrated by Catherine Groenewald

Translated by Sandra Mulesu

Language IciBemba

Level Level 4

Narrate full story The audio for this story is currently not available.


Ibala lyaba maama lyali ilisuma sana, mwali amasaka, amale, na tute. Nomba ifisuma palifyonse ni nkonde. Nangula bamaama bakwete abeshikulu abengi, Nalishibe ukuti nine batemwishishe. Balenjita lyonse kung’anda kumwabo. Balenshimikilako notwankama tumotumo. Nomba kwali inkama imo iyo bashanjebeleko. Uku balefumbika inkonde.

Bibi alikuwa na bustani nzuri iliyojaa mtama, ulezi na mihogo. Lakini kati ya mazao yote, alipenda zaidi ndizi. Japo bibi alikuwa na wajukuu wengi, nilikuja kubaini kuwa alikuwa ananipenda mimi zaidi ya wote. Mara nyingi alikuwa akinialika nyumbani kwake. Pia alikuwa ananiambia siri ndogo ndogo. Lakini kulikuwa na siri moja ambayo hakunishirikisha: alipokuwa anavundika ndizi.


Bushiku bumo namwene bamaama nababika icimuseke pakasuba panse yang’anda. Ilyo nabepwishe batile “museke wankama”. Mupepi nomuseke pali amabula yankonde ayenji aya bamaama balepilibula inshita nenshita. Nalefyaisha ukwishiba, eyo nabepwishe, “mabula yafinshi aya maama?” Banjaswikefye abati “Mabula ya nkama yandi”

Siku moja niliona tenga kubwa limeanikwa juani nje ya nyumba ya bibi. Nilipouliza lilikuwa la nini, jibu pekee nililopata lilikuwa, “Hilo ni tenga langu la maajabu.” Pembeni mwa tenga lile kulikuwa na majani ya ndizi ambayo bibi alikuwa akiyageuza kila mara. Nilipatwa na shauku. “Bibi, hayo majani ni ya nini?” niliuliza. Jibu pekee nililopata lilikuwa, “Ni majani yangu ya maajabu.”


Calinshansamusha ukutaamba, bamaama, inkonde, amabula yankonse, nomuseke uukulu. Nomba bamaama epakuntuma ukuya bombako utumilimo tumbi. Elyo nabebe nati, “Maama napapata lekeni imboneko efyo mucita…” Bamaama epakuti, “uluufwa, cita ifyo nakweba endesha” Efyo naile ulubilo.

Nilikuwa na shauku kubwa kumwangalia bibi, ndizi, majani ya ndizi na tenga kubwa. Lakini bibi alinituma kwenda kwa mama. “Bibi, tafadhali naomba nitazame unavyoandaa…” “Usiwe msumbufu, fanya ulichoambiwa,” alisisitiza. Nikaondoka nikikimbia.


Nishi nabwelele, nasangile bamaama nabekala panse, nomba tapali inkonde angula umuseke. “Maama umuseke ukikwisa, nenkonde shilikwi?” Bamaama epakuti “Fili kuncende yandi iya nkama”. Naliufwa ububi sana.

Niliporudi, bibi alikuwa amekaa nje, ila hakukuwa na tenga wala ndizi. “Bibi, tenga liko wapi, zile ndizi ziko wapi, na…” Jibu pekee nililopata lilikuwa, “Zipo kwenye eneo la maajabu.” Ilikuwa inasikitisha.


Panuma yanshiku shibili, bamaama bantumine mukusenda inkoto yabo kumuputule. Cilya naisulafye icibi, akacena kankonde ishapya kampokelela. Kukati ekwali umuseke wankama. Ninshi nabafisa bwino bwino mubulangeti bwakale. Nafimbulapo nanunshako akacena akasuma.

Siku mbili baadaye, bibi alinituma kwenda chumbani kwake kumletea mkongojo. Mara tu baada ya kufungua mlango, nilikaribishwa na harufu kali ya ndizi mbivu. Pembeni mwa chumba kulikuwa na tenga kubwa la maajabu la bibi. Lilikuwa limefichwa na blanketi la zamani. Nikaliinua na kunusa ile harufi nzuri.


Ishiwi lyaba maama epakuntinya lintu banjutile. “Finshi ulecita? Endesha ndetela inkoto”. Efyo naendeshe ukutwala inkoto, bamaama epakunjipusha ati, “Finshi uleseka”. Cilya banjipusha elyo naibukisha ukuti ncili nesekelela pakusanga incende yankama yaba maama.

Sauti ya bibi ilinishtua alipoita, “Unafanya nini? Fanya haraka niletee mkongojo.” Nikaharakisha kwenda nje na mkongojo wake. “Unatabasamu nini?” bibi aliuliza. Swali lake likanifanya nigundue kuwa kumbe bado nilikuwa ninatabasamu baada ya kugundua eneo lake la maajabu.


Ubushiku bwakonkelepo, elyo bamaama baishile mukupempula bamayo, nabutukile kumwabo mukumona inkonde nakabili. Nasanga umusemo wankonde ishapya. Nasendako lumo nafisa mwilaya. Nasha nafimbapo bwino bwino nakabili. Nabutukila kulukungu lwang’anda nokulya ulukonde bwangu bwangu. Iyi nkonde yali iyalowesha ukucila palishonse inkonde nalyapo.

Siku iliyofuata bibi alipokuja kumtembelea mama yangu, nikakimbilia nyumbani kwake kuangalia ndizi tena. Kulikuwa na vichane vya ndizi zilizoiva. Nikachukua ndizi moja na kuificha kwenye nguo yangu. Baada ya kufunika tenga tena, nikaenda nyuma ya nyumba na harakaharaka nikaila. Ilikuwa ni ndizi tamu ambayo sijawahi kula kamwe.


Ubushiku bwakonkelepo, elyo bamaama baile mwibala mukuswa umusalu, Naliya lushenshe muku lengela pa nkonde. Ninshi shonse shili mukupya. Efyo nasendelemo shicne. Cilya ndebendelela kucibi, naunfwa bamaama balekola panse. Efyo nafishile inkonde mwilaya nokuya bapita epobali.

Siku iliyofuata, bibi alipokuwa bustanini akichuma mboga, nikanyemelea ndani kuchungulia ndizi. Karibu zote zilikuwa zimeiva. Nikashindwa kujizuia nikachukua kichane cha ndizi nne. Nilipokuwa nanyata kuelekea mlangoni, nikamsikia bibi akikohoa nje. Nilifanikiwa kuzificha ndizi ndani ya nguo yangu na tukapishana bila ya kugundua.


Ubushiku bwakonkelepo, bwali bushiku bwakushitisha ku maliketi. Bamaama babukile lucelocelo. Baletwala inkonde ishapya na tute lyonse mukushitisha kumaliket. Nshacelele mukubamona, nomba nalibafuluka.

Siku iliyofuata ilikuwa siku ya gulio. Bibi aliamka asubuhi sana. Huwa anapeleka ndizi mbivu na mihogo kuuza gulioni. Siku hiyo sikuwa na haraka kwenda kumsalimia. Ila sikuweza kumkwepa kwa muda mrefu.


Mucungulo, bamayo, batata na bamaama efyo banjitile. Naishiba nelyashi. Ubushiku bulya lintu naile mukusendama, nasambilile ukuti nshakabwekeshepo ukwibbila bamaama, abafyashi bandi nangu umuntu umbi nakabili.

Jioni ile niliitwa na mama, baba na bibi. Nilijua kwanini. Usiku ule nilipokwenda kulala, nilijua siwezi kuiba tena. Siwezi kumwibia bibi, wazazi wangu na mtu yeyote yule.


Written by: Ursula Nafula
Illustrated by: Catherine Groenewald
Translated by: Sandra Mulesu
Language: IciBemba
Level: Level 4
Source: Grandma's bananas from African Storybook
Creative Commons License
This work is licensed under a Creative Commons Attribution 3.0 International License.
Options
Back to stories list Download PDF