Download PDF
Back to stories list

ما قالته أخت فوسي Alichokisema dada yake Vusi

Written by Nina Orange

Illustrated by Wiehan de Jager

Translated by Maaouia Haj Mabrouk

Read by Mashael Muhanna

Language Arabic

Level Level 4

Narrate full story

Reading speed

Autoplay story


في صباح باكر من أحد الأيام، نادت الجدة حفيدها فوسي قائلة: “فوسي، أرجو أن تأخذ هذه البيضة لوالديك. يريدان تحضير كعكة كبيرة بمناسبة حفل زفاف أختك”.

Siku moja asubuhi bibi yake Vusi alimwita na kumwambia, “Tafadhali peleka yai hili kwa wazazi wako. Wanataka kutengeneza keki kubwa kwa ajili ya harusi ya dada yako.”


وفي طريقه إلى منزل والديه، اعترض فوسي ولدين يقطفان الفواكه. خطف أحد الولدين البيضة من يد فوسي وألقى بها على شجرة فتهشمت البيضة.

Alipokuwa njiani kuelekea kwa wazazi wake, Vusi akakutana na vijana wawili wanaokota matunda. Kijana mmoja akanyakua yai kutoka kwa Vusi na akalirusha kwenye mti. Yai likavunjika.


صاح فوسي: “ماذا فعلت؟ البيضة كانت لصنع كعكة، والكعكة كانت لحفل زفاف أختي. ماذا ستقول أختي إذا لم يكن في العرس كعكة؟”.

“Umefanya nini?” Vusi akalia. “Yai lile lilikuwa kwa ajili ya keki. Keki ilikuwa kwa ajili ya harusi ya dada yangu. Dada yangu atasemaje kama hakutakuwa na keki ya harusi?”


أسف الولدان لإزعاجهما لفوسي وقال أحدهما: “لن نستطيع المساعدة في صنع الكعكة، لكن ها هي عصا للمشي، خذها لأختك”. أخذ فوسي العصا وواصل طريقه إلى المنزل.

Vijana wale waliomba msamaha kwa kumchokoza Vusi. “Hatuna la kufanya kuhusu keki, lakini hii hapa ni fimbo kwa ajili ya dada yako,” mmoja alisema. Vusi akaendelea na safari yake.


وفي الأثناء، التقى فوسي رجلين يبنيان منزلاً. سأله أحدهما: “هل يمكننا أن نستخدم تلك العصا الغليظة التي بيدك؟”. لكن العصا كسرت لدى استعمالها، لأنها لم تكن قوية بالقدر الكافي لتستخدم في البناء.

Njiani alikutana na wanaume wawili wakijenga nyumba. “Tunaweza kutumia hiyo fimbo imara?” mmoja akaomba. Lakini fimbo haikuwa imara kwa kujengea, na ikavunjika.


صاح فوسي: “ماذا فعلتما؟ تلك العصا كانت هدية لأختي. لقد أعطاني إياها جامعا الفواكه اللذان كسرا البيضة التي كنا سوف نستخدمها لعمل كعكة لأختي بمناسبة زواجها. أما الآن، فلا بيضة ولا كعكة ولا هدية. ماذا ستقول أختي؟”

“Mmefanya nini?” Vusi akalia. “Fimbo hii ilikuwa zawadi kwa ajili ya dada yangu. Waangua matunda walinipa fimbo hiyo kwa sababu walivunja yai la keki. Keki ilikuwa ni kwa ajili ya harusi ya dada yangu. Sasa hakuna yai, hakuna keki, na hakuna zawadi. Dada yangu atasemaje?”


أسف البناءان على كسر العصا. فقال أحدهما: “لن نستطيع فعل شيء بخصوص الكعكة، لكن هذا بعض القش، خذه لأختك”. أخذ فوسي القش وواصل طريقه.

Wajenzi waliomba msamaha kwa kuvunja fimbo. “Hatuna la kufanya kuhusu keki, lakini tutakupa makuti umpelekee dada yako,” mmoja alisema. Na Vusi akaendelea na safari yake.


وبينما هو في طريقه إلى البيت، اعترضه مزارع ومعه بقرة. قالت البقرة: “هذا القش لذيذ، هل لي بقضمه منه؟” لكن القش كان حلو المذاق لدرجة أن البقرة التهمته كله.

Njiani, Vusi akakutana na mkulima akiwa na ng’ombe. “Una makuti mazuri, naweza kupata kidogo?” Ng’ombe akaomba. Lakini makuti yalikuwa matamu ng’ombe akayala yote!


صاح فوسي: “ماذا فعلت أيتها البقرة؟ ذاك القش كان هدية لأختي. أعطاني إياه البناءان بعد أن كسرا العصا التي تسلمتها من جامعيْ الفواكه الذيْنِ هشَّما البيضة التي كنا سنصنع بها كعكة لعرس أختي. لم يعد لي الآن لا بيضة ولا كعكة ولا هدية… ترى ماذا ستقول أختي؟”.

“Umefanya nini?” Vusi akalia. “Makuti haya yalikuwa zawadi ya dada yangu. Wajenzi walinipa makuti kwa kuwa walivunja fimbo yangu niliyopewa na waangua matunda. Waangua matunda walinipa fimbo kwa kuwa walivunja yai kwa ajili ya keki ya dada yangu. Keki ilikuwa kwa ajili ya harusi ya dada yangu. Sasa hakuna yai, hakuna keki, na hakuna zawadi. Dada yangu atasemaje?”


اعتذرت البقرة لجشعها، أما المزارع فقد قرر أن يسلم البقرة لفوسي كهدية لأخته. أخذ فوسي البقرة وواصل طريقه.

Ng’ombe aliomba msamaha kwa kuwa mlafi. Mkulima alikubali kumpa Vusi ng’ombe aende naye kama zawadi kwa ajili ya dada yake. Vusi akaendelea na safari yake.


لكن، وبحلول وقت العشاء فرت البقرة هاربة ورجعت إلى المزارع الذي سلمها لفوسي. أضاع فوسي طريقه ووصل متأخراً جداً لحفل زفاف أخته، فقد وجد المدعوين بصدد تناول الطعام.

Lakini wakati wa chakula cha jioni ng’ombe alikimbia kurudi kwa mkulima. Na Vusi akapotea njiani. Akafika kwa kuchelewa sana kwenye harusi ya dada yake. Wageni walikuwa tayari wanakula.


صاح فوسي: “ماذا عساي أن أفعل الآن؟ … لقد هربت البقرة، هدية العرس التي منحني إياه المزارع مقابل القش الذي سلمني إياه البناءان عندما كسرا العصا التي أعطاني إياها جامعا الفواكه بعد أن هشما البيضة التي كنا سنصنع بها كعكة زفاف أختي. أما الآن فلا بيضة ولا كعكة ولا هدية”.

“Nifanye nini?” alilia Vusi. “Ng’ombe aliyekimbia alikuwa ni zawadi, ambayo nilipewa kama mbadala wa makuti niliyopewa na wajenzi. Wajenzi walinipa makuti kwa sababu walivunja fimbo niliyopewa na waangua matunda. Waangua matunda walinipa fimbo kwa sababu walivunja yai la keki. Keki ilikuwa kwa ajili ya harusi. Kwa hiyo hakuna yai, hakuna keki, na hakuna zawadi.”


فكرت أخت فوسي قليلاً ثم قالت: “أخي، لا تهمني الهدايا، ولا الكعكة. نحن هنا معا، وأنا سعيدة. اذهب الآن والبس ثيابك الجميلة وتعال، نحتفل بهذا اليوم السعيد معاً”. وكان ذاك ما فعله فوسي.

Dada yake Vusi alifikiria kwa muda, halafu akasema, “Kaka yangu Vusi, usijali zawadi, pia usijali keki! Tupo hapa pamoja, nina furaha. Nenda kavae nguo zako nadhifu na uje tusherehekee siku hii!”


Written by: Nina Orange
Illustrated by: Wiehan de Jager
Translated by: Maaouia Haj Mabrouk
Read by: Mashael Muhanna
Language: Arabic
Level: Level 4
Source: What Vusi's sister said from African Storybook
Creative Commons License
This work is licensed under a Creative Commons Attribution 3.0 International License.
Options
Back to stories list Download PDF