Download PDF
Back to stories list

የማር ቆራጩ መሪ በቀል Kisasi cha Kiongozi

Written by Zulu folktale

Illustrated by Wiehan de Jager

Translated by Mezemir Girma

Read by Abenezer Chane

Language Amharic

Level Level 4

Narrate full story

Reading speed

Autoplay story


ይህ የማር ቆራጩ መሪ የንጌዴና ግንጊሌ የተባለ ገብጋባ ወጣት ታሪክ ነው። አንድ ቀን ግንጊሌ አደን ላይ ሳለ የንጌዴን ጥሪ ሰማ። ግንጊሌ ማርን አስቦ ጎመዠ። ከራሱ በላይ ባሉት የዛፍ ቅርንጫፎች ወፉን እስኪያየው ድረስ እየፈለገ ቆም ብሎ በጥንቃቄ አደመጠ። ‹‹ችክ፣ ችክ፣ ችክ›› በማለት ወደ ቀጣዮቹ ዛፎች እየበረረ ትንሹ ወፍ ጮኸ። ግንጊሌ መከተሉን እርግጠኛ ለመሆን ቆም እያለ እያየ ‹‹ችክ፣ ችክ፣ ችክ›› እያለ ተጣራ።

Hii ni hadithi ya Ngede, ambaye ni ndege mpenda asali, na mvulana mmoja mlafi anayeitwa Gingile. Siku moja Gingile alipokuwa akiwinda alisikia mwito wa Ngede. Kinywa chake kilianza kutokwa mate kwa kufikiria asali. Alisimama, akasikiliza na kuangalia vizuri hadi alipomwona yule ndege akiwa ametua kwenye matawi yaliyokuwa juu ya kichwa chake. “Chitik-chitik-chitik,” yule ndege mdogo alitatarika aliporuka na kutua kwenye mti mmoja hadi mwingine, na mwingine tena. “Chitik-chitik-chitik,” aliita, huku akinyamaza na kuhakikisha kwamba Gingile alikuwa amemfuata.


ከግማሽ ሰዓት በኋላ ከአንድ ትልቅ ሾላ ጋ ደረሱ። ንጌዴ በቅርንጫፎቹ መካከል የሚያደርገውን አጥቶ ቱር ቱር አለ። ካንዱም ቅርንጫፍ ላይ ተረጋግቶ ራሱን ወደ ግንጊሌ ዘንበል አድርጎ ‹‹ይሄውና! አሁን ና! ይህን ያህል ምን አቆየህ?›› የሚለው መሰለ። ግንጊሌ ከዛፉ ስር ምንም ንቦች አልታዩትም፤ ንጌዴን ግን አምኖታል።

Baada ya nusu saa, walifika kwenye mti wa matini. Ngede aliruka kama mwenda wazimu kutoka tawi moja hadi jingine. Kisha alitulia kwenye tawi moja na kupindua kichwa chake akimwangalia Gingile kana kwamba anasema, “Ipo hapa! Njoo sasa! Kwa nini unachukua muda mrefu?” Gingile hakuweza kuona nyuki wowote kutoka chini ya mti, lakini alimwamini Ngede.


ስለዚህ ግንጊሌ የማደኛ ጦሩን ከዛፍ ስር አስቀምጦ ደረቅ እንጨቶችን ለቀመና እሳት አቀጣጠለ። እሳቱ በደንብ ሲቀጣጠል አንድ ረጅም ደረቅ እንጨት በእሳቱ መካከል አደረገ። ይህም እንጨት ሲነድ ብዙ ጭስ የሚወጣው ዓይነት ነበር። በእሳት ያልተያያዘውን የእንጨቱን ጫፍ በጥርሱ ይዞ ዛፍ ይወጣ ጀመር።

Kwa hivyo Gingile aliweka mkuki wake alioutumia kuwinda chini ya mti, akakusanya vijiti vilivyokauka na kuwasha moto mdogo. Moto ulipokuwa ukiwaka vizuri, alichomeka kijiti kirefu kwenye moto. Mti huu ulijulikana kwa kutoa moshi mwingi ulipokuwa unaungua. Alianza kukwea mti huku akishika kijiti kwa meno upande usiofuka moshi.


ወዲያውኑም የንቦች ድምጽ ጎልቶ ተሰማው። በዛፉ ግንድ ላይ ካለ ቀዳዳ ነበር እየወጡ ያሉት - ከቀፏቸው። ግንጊሌም ከቀፎው ሲደርስ በመቀጣጠል ላይ ያለውን የእንጨቱን ጫፍ ወደ ቀዳዳው ጨመረው። ንቦቹም ተናደው መውጣት ጀመሩ። ጭሱንም ስላልወደዱት በረው ጠፉ፤ ግንጊሌንም ነደፉት!

Muda mfupi baadaye, aliweza kusikia sauti ya nyuki wenye harakati nyingi ikivuma. Walikuwa wakiingia na kutoka kwenye upenyo wa mti, yaani mzinga wao. Gingile alipoufikia mzinga, alisukuma ile kuni ya moto ndani ya ule upenyo. Nyuki waliharakisha kutoka ndani wakiwa na hasira na uchungu. Waliruka na kwenda mbali kwa sababu hawakupenda moshi – lakini walifanya hivyo baada ya kumuuma Gingile kwa uchungu!


ንቦቹም እንደወጡ ግንጊሌ እጆቹን ወደ ቀፏቸው አስገባቸው። በጥሩ ማር የተሞላ ብዙ ከባባድ እጭም አወጣ። በትከሻውም ላይ ካነገተው ኮረጆ አስቀመጠውና ከዛፉ መወረድ ጀመረ።

Nyuki walipokuwa nje, Gingile aliingiza mikono yake ndani ya kiota. Alitoa kipande kikubwa cha sega kilichokuwa kinadondoka urojo mzito wa asali, na kilichojaa wadudu weupe wanene. Aliiweka taratibu ndani ya mkoba aliokuwa nao na kuanza kushuka kutoka mtini.


ንጌዴ ግንጊሌ የሚሰራውን እያንዳንዱን ነገር በጉጉት እየተከታተለ ነበር። ለማር ቆረጣ ስለመራው በማመስገን ከያዘው ማር ትንሽ ቆረጥ አድርጎ እንዲሰጠው እየጠበቀ ነበር። ንጌዴ ከቅርንጫፍ ቅርንጫፍ ለመሬት ቀረብ ብሎ ይዘዋወር ጀመር። በመጨረሻም ግንጊሌ ከዛፉ ወረደ። ንጌዴም ከአጠገቡ ካለ ድንጋይ ላይ ተቀምጦ ሽልማቱን ይጠብቅ ጀመር።

Ngede alishuhudia kila kitu Gingile alichofanya. Alikuwa anamsubiri abakishe kiasi kidogo cha asali kama shukurani kwa Kiongozi. Ngede aliruka kutoka tawi hadi tawi huku akikaribia chini. Mwishowe Gingile alifika chini ya mti. Ngede alitua kwenye mwamba karibu na mvulana huyo na kusubiri zawadi yake.


ግንጊሌ ግን እሳቱን አጥፍቶ፣ ጦሩን አንስቶና ወፉን ረሰቶ ወደቤቱ መሄድ ጀመረ። ንጌዴም በንዴት ‹‹ቪክ ቶር! ቪክ ቶር›› ሲል ተጣራ። ግንጊሌም ቆም ብሎ ትንሹ ወፍ ላይ አፈጠጠበትና ጮክ ብሎ ሳቀ። ‹‹ትንሽ ማር ፈለገህ ነው፣ ነው አይደል፤ ወዳጄ? አሃ! ግን ስራውን ሁሉ እኮ እኔ ነኝ የሰራሁት፤ የተነደፍኩትም እኔው ነኝ። ታዲያ ከዚህ ማር ለምን እሰጥሃለሁ?›› አለው። ነገደም ተናደደ። እንደዚህ መደረግ አልነበረበትም! መበቀል ግን አለበት።

Lakini Gingile alizima moto, akachukua mkuki wake na kuanza safari kwenda nyumbani bila kumjali ndege yule. Ngede aliita kwa hasira, “USH-ndi! USH-ndi!” Gingile alisimama, akamkodolea macho yule ndege kisha akacheka kwa sauti. “Unataka asali kidogo, rafiki yangu? Ha! Lakini ni mimi niliyefanya kazi yote pamoja na kuumwa na nyuki. Kwa nini nikugawie hii asali tamu?” Baada ya kusema hivyo, aliondoka na kwenda zake. Ngede alikasirika sana! Hivi sivyo alivyostahili kutendewa! Ila atalipiza kisasi.


አንድ ቀን በድጋሚ፣ ከብዙ ሳምንታት በኋላ ግንጊሌ ንጌዴ ማር ሊጠቁመው ሲጠራው ሰማ። ያንን ጣፋጭ ማር አስታውሶ ወፉን በጉጉት ይከተለው ጀመር። ገግንጊሌን በጫካው ጠርዝ ከመራው በኋላ ንጌዴ በአንድ እሾሃማ ዛፍ ስር ለማረፍ ቆመ። ‹‹አሃ፣›› ‹‹ቀፎው በዚህ ዛፍ ላይ መሆን አለበት›› ሲል ግንጊሌ አሰበ። እሳቱን በፍጥነት አያይዞና የሚያያዘውን እንጨት በአፉ ይዞ ዛፉን ይወጣ ጀመር። ንጌዴም ተቀምጦ ይከታተል ጀመር።

Siku moja baada ya majuma machache, Gingile tena alisikia mwito wa asali kutoka kwa Ngede. Aliikumbuka asali tamu, na kwa hamu alimfuata ndege yule kwa mara nyingine. Baada ya kumwongoza Gingile pembeni mwa msitu, Ngede alisimama na kupumzika chini ya mti wa mwavuli. “Ahh,” Gingile aliwaza. “Lazima mzinga umo ndani ya mti huu.” Kwa haraka aliwasha moto wake na kuanza kukwea mti huku akibeba kuni iliyotoa moshi katika meno yake. Ngede alikaa na kuangalia tu.


ግንጊሌ የተለመደውን የንቦች ድምጽ ለምን እንዳልሰማ እያሰበ ዛፉ ላይ ወጣ። ‹‹ምናልባት ቀፎው በጣም ጥልቅ ቦታ ላይ ይሆናል ያለው›› ሲል ለራሱ አሰበ። ወደሌላ ከፍ ወዳለ ቅርንጫፍ ላይ ወጣ። ያገኘው ነገር ግን ቀፎ ሳይሆን ፊት ለፊት የመጣችበትን ነብር ነበር! ነብሯ እንቅልፏን ሳታስበው ስላቋረጣት በጣም ተናደደች። ዓይኖቿን ጠበብ አድርጋ፣ አፏን ከፍታ፣ ትላልቅና ሹል ጥርሶቿን አገጠጠችበት።

Gingile alipopanda, alishangaa kwa nini hakusikia sauti ya nyuki. “Pengine mzinga umo ndani zaidi katika mti,” alifikiria. Alipanda tena juu ya tawi jingine. Lakini badala ya mzinga, alijikuta uso kwa uso na chui! Chui alikuwa na hasira sana kwa sababu usingizi wake ulikuwa umekatizwa. Aliyafanya macho yake kuwa madogo, akaufungua mdomo wake na kuonyesha meno yake makubwa na makali.


ነብሯ ለቀም ሳታደርገው ግንጊሌ ከዛፉ በፍጥነት መውረድ ጀመረ። በፍጥነቱም የተነሳ አንዱን ቅርንጫፍ ስቶት መሬት ላይ ክፉኛ ወድቆ ቁርጭምጭሚቱ ዞረ። በተቻለው መጠን በፍጥነት እያነከሰ ሄደ። ዕድሉ ረድቶት ነብሯ እንቅልፍ ስለተጫናት አላሳደችውም። ንጌዴ፣ የማር ቆራጩ መሪ፣ በቀሉን ተበቅሏል። ግንጊሌ ም ትምህርት ቀስሟል።

Kabla ya Chui kumvamia Gingile, alishuka chini haraka. Katika haraka hiyo, aliteleza na kuanguka kwa kishindo huku akiumia mguu wake. Alirukaruka akienda kwa haraka alivyoweza. Kwa bahati nzuri, Chui alikuwa bado amelala kwa hivyo hakumfukuza. Ngede, Kiongozi alikuwa amelipiza kisasi chake na Gingile alikuwa amejifunza funzo lake.


ስለዚህ የግንጊሌ ልጆች የንጌዴን ታሪክ ሲሰሙ ለዚያ ትንሽ ወፍ አክብሮት አላቸው። ማር በቆረጡ ቁጥር ለማር ቆራጩ መሪ ከነእጩ ብዙ ቆረጥ አድርገው መስጠታቸውን ያረጋጣሉ።

Kwa hivyo wakati watoto wa Gingile wanaposikia hadithi ya Ngede, wanamheshimu yule ndege. Kila wanapotoa asali, huhakikisha kwamba wanamwachia Kiongozi fungu kubwa!


Written by: Zulu folktale
Illustrated by: Wiehan de Jager
Translated by: Mezemir Girma
Read by: Abenezer Chane
Language: Amharic
Level: Level 4
Source: The Honeyguide's revenge from African Storybook
Creative Commons License
This work is licensed under a Creative Commons Attribution 3.0 International License.
Options
Back to stories list Download PDF