Download PDF
Back to stories list

ኖዚቤሌና ሦስቱ ጸጉሮች Nozibele na nywele tatu

Written by Tessa Welch

Illustrated by Wiehan de Jager

Translated by Mezemir Girma

Read by Abenezer Chane

Language Amharic

Level Level 3

Narrate full story

Reading speed

Autoplay story


በድሮ ጊዜ ሦስት ሴቶች እንጨት ለመሰብሰብ ከቤታቸው ወጥተው ነበር።

Hapo zamani za kale, wasichana watatu walienda kukusanya kuni.


ሞቃት ቀን ስለነበር ለመዋኘት ወደ ወንዝ ወረዱ። ተጫወቱ፤ ውኃ ተራጩ፤ ዋኙ።

Ilikuwa ni siku yenye jua kali na wakaamua kwenda mtoni kuogelea. Wakaogelea huku wakicheza na kurushiana maji.


ድንገት ምሽት መሆኑን ተገነዘቡ። ወደ መንደራቸውም ተጣደፉ።

Ghafla waligundua kuwa muda umekwenda. Wakaharakisha kurudi nyumbani.


እቤታቸው ሊደርሱ ሲሉ ኖዚቤሌ እጇን አንገቷ ላይ አደረገች። የአንገት ጌጧን ረስታዋለች! ‹‹እባካችሁ አብራችሁኝ ተመለሱ!›› ብላ ባልንጀሮቿን ለመነቻቸው። ጓደኞቿ ግን በጣም እንደዘግየች ነገሯት።

Walipokuwa wanakaribia kufika nyumbani, Nozibele akajishika shingoni. Alikuwa amesahau shanga zake! “Tafadhali turudini!” aliwasihi rafiki zake. Lakini rafiki zake wakasema tumechelewa.


ስለዚህ ኖዚቤሌ ወደ ወንዙ ብቻዋን ተመለሰች። የአንገት ጌጧንም አግኝታ ወደ ቤቷ ለመመለስ ተቻኮለች፤ ነገር ግን በጨለማ ውስጥ ጠፋች።

Kwa hiyo Nozibele akarudi mwenyewe mtoni. Akapata shanga zake na akakimbia kurudi nyumbani. Lakini akapotea gizani.


ከሩቅ ከአንዲት ጎጆ የሚወጣ ብርሃን አየች። ወደሱም ሄዳ በሩን አንኳኳች።

Kwa mbali akaona mwanga unatoka kwenye nyumba. Akakimbilia kwenye nyumba na kugonga mlango.


ባልተጠበቀ ሁኔታ ዉሻ በሩን ከፈተላት። ‹‹ምን ፈልገሽ ነው?›› አላት። ‹‹ጠፍቻለሁ፤ እና ማደሪያ ቦታ ፈልጌ ነበር›› ብላ ነገረችው። ‹‹ነይ ግቢ፤ አለዚያ እነክስሻለሁ!›› አላት ዉሻው። ስለዚህ ኖዚቤሌ ገባች።

Akastaajabu kumwona mbwa akifungua mlango na akasema, “Unataka nini?” “Nimepotea na ninatafuta sehemu ya kulala,” akasema Nozibele. “Ingia ndani, la sivyo nitakung’ata!” mbwa akamwambia. Nozibele akaingia ndani.


ከዚያም ዉሻው ‹‹ምግብ አብስዪልኝ!›› አላት። ‹‹እንዴ፣ እኔ እኮ ለዉሻ ምግብ ሰርቼ አላውቅም›› ብላ መለሰችለት። ‹‹ስሪልኝ፤ አለዚያ እነክስሻለሁ!›› አላት ዉሻው። ስለዚህ ኖዚቤሌ ለዉሻው ምግብ ሰራችለት።

Mbwa akamwambia, “Nipikie!” “Sijawahi kumpikia mbwa,” akajibu. “Pika, la sivyo nitakung’ata!” mbwa akasema. Nozibele akampikia mbwa chakula.


ከዚያም ዉሻው ‹‹አልጋዬን አንጥፊልኝ!›› አላት። ኖዚቤሌም ‹‹እኔ እኮ ለዉሻ አልጋ አንጥፌ አላውቅም›› ብላ መለሰችለት። ‹‹አንጥፊልኝ፤ ያለዚያ እነክስሻለሁ!›› አላት ዉሻው። ስለዚህ ኖዚቤሌ አነጠፈችለት።

Mbwa akamwambia, “Nitandikie kitanda!” Nozibele akajibu, “Sijawahi kumtandikia mbwa kitanda.” “Tandika kitanda, la sivyo nitakung’ata!” mbwa akasema. Nozibele akatandika kitanda.


በየቀኑ ለዉሻው ምግብ መስራት፣ ማጽዳትና ማጠብ ስራዋ ሆነ። ከዚያም አንድ ቀን ዉሻው ‹‹ኖዚቤሌ፣ ዛሬ ጓደኞቼን ልጠይቅ እሄዳለሁ። እኔ ከመምጣቴ በፊት ቤቱን አጽጂ፤ ምግብ ስሪ፤ የሚተጣጠቡትንም ነገሮች እጠቢ›› አላት።

Akawa kila siku anampikia, anamfulia na kumfagilia mbwa. Siku moja mbwa akasema, “Nozibele, leo naenda kuwatembelea rafiki zangu. Fagia nyumba, pika chakula na osha vitu vyangu kabla sijarudi.”


ዉሻው እንደሄደ ኖዚቤሌ ከራሷ ላይ ሦስት ጸጉሮችን ከጭንቅላቷ ላይ ነቀለች። አንዱን ጸጉር ከአልጋው ስር፣ አንዱን ከበሩ ኋላ፣ እና ሌላውን ደግሞ በከብቶቹ በረት አስቀመጠቻቸው።

Mara baada tu ya mbwa kuondoka, Nozibele akanyofoa nywele tatu kutoka kwenye kichwa chake. Akaweka unywele mmoja chini ya kitanda, mmoja nyuma ya mlango, na mwingine akauweka kwenye uzio wa nyumba. Halafu, akakimbia kuelekea nyumbani kwa nguvu zote.


ዉሻዉም እንደተመለሰ ኖዚቤሌን ፈለጋት። ‹‹ኖዚቤሌ፣ የት ነሽ?›› ብሎ ተጣራ። ‹‹አልጋው ስር ነኝ›› አለ የመጀመሪያው ጸጉር። ‹‹በሩ ጀርባ ነኝ›› አለ ሁለተኛው ጸጉር። ‹‹በረት ውስጥ ነኝ፣›› አለ ሌላኛው ጸጉር።

Mbwa aliporudi akaanza kumtafuta Nozibele. “Nozibele, uko wapi?” akapiga kelele. “Niko hapa, chini ya kitanda,” unywele wa kwanza ukajibu. “Nipo hapa nyuma ya mlango,” unywele wa pili ukajibu. “Niko hapa kwenye uzio,” unywele wa tatu ukajibu.


ከዚያም ዉሻው ኖዚቤሌ እንዳታለለችው ገባው። ስለዚህ ወደ መንደሩ እየተሯተሯጠ ፈለጋት። የኖዚቤሌ ወንድሞች ግን ትላልቅ ዱላዎች ይዘው እየጠበቁት ነበር። ውሻው ተመልሶ ሮጠ፤ ከዚያም በኋላ በመንደሩ በጭራሽ ታይቶ አያውቅም።

Mbwa akagundua kuwa Nozibele amemkimbia. Kwa hiyo akakimbia kuelekea kijijini. Kaka zake Nozibele walikuwa wakimsubiri na fimbo. Mbwa alipowaona akageuka na kukimbia, na hajawahi kuonekana tena.


Written by: Tessa Welch
Illustrated by: Wiehan de Jager
Translated by: Mezemir Girma
Read by: Abenezer Chane
Language: Amharic
Level: Level 3
Source: Nozibele and the three hairs from African Storybook
Creative Commons License
This work is licensed under a Creative Commons Attribution 3.0 International License.
Options
Back to stories list Download PDF