Téléchargement PDF
Retour à la liste des contes

Mbegu Ndogo: Hadithi ya Wangari Maathai Une petite graine : l'histoire de Wangari Maathai

Écrit par Nicola Rijsdijk

Illustré par Maya Marshak

Traduit par Ursula Nafula

Lu par Lauwo George

Langue kiswahili

Niveau Niveau 3

Lire l’histoire en entier

Vitesse de lecture

Lecture automatique du conte


Katika kijiji kimoja kwenye mteremko wa Mlima wa Kenya, katika Afrika Mashariki, msichana mdogo alifanya kazi za shambani pamoja na mama yake. Msichana huyu aliitwa Wangari.

Dans un village situé sur les flancs du Mont Kenya en Afrique de l’Est, une petite fille travaillait dans les champs avec sa mère. Son nom était Wangari.


Wangari alipenda kufanya kazi za nje. Alitumia jembe kulima katika bustani ya familia yake. Kisha alipanda mbegu ndogo katika ardhi yenye rutuba.

Wangari aimait beaucoup être dehors. Dans le potager de sa famille, elle faisait des trous dans le sol avec sa machette. Elle enfouissait des petites graines dans la terre chaude.


Alipenda majira ya jioni, wakati jua linapozama. Giza lilipozidi mpaka aliposhindwa kuona mimea, Wangari alifahamu kuwa wakati wa kwenda nyumbani uliwadia. Alikuwa anafuata kinjia chembamba kilichopita uwanjani huku akivuka mito akielekea nyumbani.

Son moment préféré de la journée était juste après le coucher du soleil. Quand il faisait trop nuit pour voir les plantes, Wangari savait qu’il était l’heure de rentrer à la maison. Pour rentrer, elle devait suivre des sentiers étroits à travers champs et traverser des rivières.


Wangari alikuwa mtoto mwerevu na alikuwa na hamu ya kwenda shule. Lakini wazazi wake walitaka awasaidie nyumbani. Alipofika umri wa miaka saba, kaka yake aliwashawishi wazazi wake kumwacha aende shule.

Wangari était une enfant intelligente et avait hâte d’aller à l’école. Mais sa mère et son père voulaient qu’elle reste à la maison pour les aider. Quand elle eut sept ans, son grand frère persuada ses parents de la laisser aller à l’école.


Alipenda kusoma! Wangari alijifunza zaidi na zaidi kwa kila kitabu alichokisoma. Alifanya vyema sana shuleni hadi akaalikwa kwenda Marekani kuendeleza masomo yake huko. Wangari alitiwa hamasa sana na nafasi hii! Alipenda kujua ulimwengu zaidi.

Elle aimait apprendre ! Wangari apprenait de plus en plus avec chaque livre qu’elle lisait. Elle travaillait si bien à l’école qu’elle fut invitée à étudier aux Etats Unis d’Amérique. Wangari était enthousiaste ! Elle voulait en savoir plus sur le monde.


Alipokuwa chuoni huko Marekani, Wangari alijifunza mengi mapya. Alisomea mimea na jinsi inavyokua. Na alikumbuka maisha yake yalivyokuwa utotoni: kucheza michezo na msitu zake katika kivuli cha miti kwenye misitu maridadi ya Kenya.

A l’université américaine, Wangari apprit beaucoup de choses nouvelles. Elle étudia les plantes et la manière dont elles grandissent. Et elle se rappela comment elle avait grandi : en jouant avec ses frères à l’ombre des arbres dans les magnifiques forêts du Kenya.


Jinsi alivyojifunza ndivyo alivyofahamu kuwa aliwapenda watu wa Kenya. Alitaka wafurahi na wawe wenye uhuru. Jinsi alivyojifunza ndivyo alivyokumbuka nyumbani kwao Afrika.

Plus elle apprenait, plus elle réalisait qu’elle aimait les habitants du Kenya. Elle voulait qu’ils soient heureux et libres. Plus elle apprenait, plus elle se rappelait son foyer africain.


Alipokamilisha masomo yake, alirudi Kenya. Lakini nchi yake ilikuwa imebadilika. Kulikuwa na mashamba makubwa kila upande. Wanawake hawakupata kuni za kuwasha moto wa kupikia. Watu walikuwa maskini na watoto walikuwa na njaa.

Quand elle eut terminé ses études, elle retourna au Kenya. Mais son pays avait changé. De larges fermes s’étendaient à travers la campagne. Les femmes n’avaient plus de bois pour cuire les aliments. Les gens étaient pauvres et les enfants avaient toujours faim.


Wangari alijua la kufanya. Aliwafundisha wanawake jinsi ya kupanda miti kutokana na miche. Wanawake waliuza ile miti na pesa walizopata walizitumia kwa mahitaji ya familia zao. Wanawake walifurahi. Wangari alikuwa amewasaidia kuwa wenye nguvu na uwezo.

Wangari savait ce qu’il fallait faire. Elle apprit aux femmes comment planter des arbres en utilisant des graines. Les femmes vendirent les arbres et utilisèrent l’argent pour faire vivre leurs familles. Les femmes étaient très heureuses. Wangari les avait aidées à se sentir puissantes et fortes.


Muda ulipopita, miti mipya ilikuwa misitu, na mito ilianza tena kupitisha maji. Ujumbe wa Wangari ulienea Afrika nzima. Leo, mamilioni ya miti imemea kutokana na mbegu za Wangari.

Avec le temps, les nouveaux arbres se transformèrent en forêts, et les rivières recommencèrent à couler. Le message de Wangari traversa toute l’Afrique. Aujourd’hui des millions d’arbres ont grandi grâce aux graines de Wangari.


Wangari alikuwa amefanya bidii. Watu ulimwengu mzima walifahamu hili na wakampa tuzo. Tuzo hii inaitwa, ‘Tuzo ya Amani ya Nobel.’ Na alikuwa mwanamke wa Kiafrika wa kwanza kupokea tuzo hii.

Wangari avait travaillé dur. Partout dans le monde, les gens s’en aperçurent et lui donnèrent un prix renommé. Il s’appelle le Prix Nobel de la Paix et elle fut la première femme africaine à le recevoir.


Wangari alifariki mwaka 2011, lakini tunaweza kumkumbuka kila tunapoona mti maridadi.

Wangari mourut en 2011 mais nous pensons à elle à chaque fois que nous voyons un bel arbre.


Écrit par: Nicola Rijsdijk
Illustré par: Maya Marshak
Traduit par: Ursula Nafula
Lu par: Lauwo George
Langue: kiswahili
Niveau: Niveau 3
Source: A Tiny Seed: The Story of Wangari Maathai du Livre de contes africains
Licence de Creative Commons
Ce travail est autorisé sous une licence Creative Commons Attribution 4.0 non transposé.
Options
Retour à la liste des contes Téléchargement PDF