Download PDF
Back to stories list

Khalai azungumza na mimea Khalai talks to plants Khalai azungumza na mimea

Written by Ursula Nafula

Illustrated by Jesse Pietersen

Translated by Ursula Nafula

Read by Lauwo George

Language Kiswahili

Level Level 2

Narrate full story

Reading speed

Autoplay story


Khalai ni msichana mwenye umri wa miaka saba. Jina lake lina maana ya ‘aliye mzuri’ katika lugha yake ya Lubukusu.

This is Khalai. She is seven years old. Her name means ‘the good one’ in her language, Lubukusu.

Khalai ni msichana mwenye umri wa miaka saba. Jina lake lina maana ya ‘aliye mzuri’ katika lugha yake ya Lubukusu.


Khalai anaamka na kuongea na mmea mchanga wa Mchungwa, “Tafadhali mti wa Mchungwa, kua mkubwa uzae machungwa mengi mabivu.”

Khalai wakes up and talks to the orange tree. “Please orange tree, grow big and give us lots of ripe oranges.”

Khalai anaamka na kuongea na mmea mchanga wa Mchungwa, “Tafadhali mti wa Mchungwa, kua mkubwa uzae machungwa mengi mabivu.”


Khalai anaenda shuleni na njiani anaongea na Nyasi, “Tafadhali Nyasi, kua kijani zaidi na zaidi na wala usikauke.”

Khalai walks to school. On the way she talks to the grass. “Please grass, grow greener and don’t dry up.”

Khalai anaenda shuleni na njiani anaongea na Nyasi, “Tafadhali Nyasi, kua kijani zaidi na zaidi na wala usikauke.”


Khalai anayapita Maua ya mwituni na kusema, “Tafadhali Maua, endelea kunawiri ili niweze kukuweka kwenye nywele zangu.”

Khalai passes wild flowers. “Please flowers, keep blooming so I can put you in my hair.”

Khalai anayapita Maua ya mwituni na kusema, “Tafadhali Maua, endelea kunawiri ili niweze kukuweka kwenye nywele zangu.”


Akiwa shuleni, Khalai anazunguumza na Mti ulioko katikati ya shule, “Tafadhali Mti, toa matawi makubwa ili tusome chini ya kivuli chako.”

At school, Khalai talks to the tree in the middle of the compound. “Please tree, put out big branches so we can read under your shade.”

Akiwa shuleni, Khalai anazunguumza na Mti ulioko katikati ya shule, “Tafadhali Mti, toa matawi makubwa ili tusome chini ya kivuli chako.”


Khalai anazunguumza na ua unaoizingira shule yake, “Tafadhali ua, kuwa mwenye nguvu ili uzuie shule yetu kutokana na watu wabaya.”

Khalai talks to the hedge around her school. “Please grow strong and stop bad people from coming in.”

Khalai anazunguumza na ua unaoizingira shule yake, “Tafadhali ua, kuwa mwenye nguvu ili uzuie shule yetu kutokana na watu wabaya.”


Anaporudi nyumbani alasiri, Khalai anautembelea mti wa Mchungwa kuangalia kama machungwa yameiva.

When Khalai returns home from school, she visits the orange tree. “Are your oranges ripe yet?” asks Khalai.

Anaporudi nyumbani alasiri, Khalai anautembelea mti wa Mchungwa kuangalia kama machungwa yameiva.


“Machungwa bado mabichi,” Khalai anashusha pumzi. “Nitakuona kesho, we mti wa machungwa. Labda utanipa chungwa bivu wakati huo.”

“The oranges are still green,” sighs Khalai. “I will see you tomorrow orange tree,” says Khalai. “Perhaps then you will have a ripe orange for me!”

“Machungwa bado mabichi,” Khalai anashusha pumzi. “Nitakuona kesho, we mti wa machungwa. Labda utanipa chungwa bivu wakati huo.”


Written by: Ursula Nafula
Illustrated by: Jesse Pietersen
Translated by: Ursula Nafula
Read by: Lauwo George
Language: Kiswahili
Level: Level 2
Source: Khalai talks to plants from African Storybook
Creative Commons License
This work is licensed under a Creative Commons Attribution 4.0 International License.
Options
Back to stories list Download PDF