Schaltfläche PDF
Zurück zur Geschichteliste

Anansi na hekima Anansi und die Weisheit

Geschrieben von Ghanaian folktale

Illustriert von Wiehan de Jager

Übersetzt von Mutugi Kamundi

Gelesen von Lauwo George

Sprache Kiswahili

Niveau Niveau 3

Vollständige Geschichte erzählen

Lesegeschwindigkeit

Autoplay Geschichte


Hapo zamani za kale, watu hawakujua chochote. Hawakujua kupanda mimea, hawakujua kushona nguo, wala hawakujua kuunda zana za chuma. Nyame, mungu aliyekuwa mbinguni, ndiye aliyekuwa mwenye hekima zote za dunia. Alihifadhi hekima hiyo kwenye chungu cha udongo.

Vor langer, langer Zeit wussten die Menschen gar nichts. Sie wussten nicht, wie man Pflanzen anbaut, wie man Tücher webt, oder wie man Eisenwerkzeuge herstellt. Der Gott Nyame oben im Himmel hatte die ganze Weisheit der Welt. Er bewahrte sie sicher in einem Tontopf auf.


Siku moja, Nyame aliamua kumpa Anansi chungu hicho cha hekima. Kila Anansi alipotazama ndani ya chungu cha udongo, alijifunza jambo jipya. Alifurahi sana!

Eines Tages beschloss Nyame, den Tontopf Anansi zu geben. Jedes Mal, wenn Anansi in den Topf schaute, lernte er etwas Neues. Es war so aufregend!


Anansi mlafi alinong’ona moyoni, “Nitakificha chungu hiki juu ya mti mrefu ili nikifaidi mwenyewe.” Akasokota uzi mrefu na kuuzungusha kwenye chungu. Kisha, akajifunga tumboni. Akaanza kupanda kwenye mti. Lakini ilikuwa vigumu kupanda kwenye mti huku chungu kikimgonga magotini kila mara.

Gierig dachte Anansi: „Ich werde den Topf sicher im Gipfel eines Baumes aufbewahren. So habe ich ihn ganz für mich allein!“ Er spann einen langen Zwirn, wickelte ihn um den Tontopf und band ihn um seinen Bauch. Er begann, den Baum hinaufzuklettern. Aber es war schwer den Baum so hinaufzuklettern, da der Topf ständig gegen seine Knie stieß.


Wakati huo wote, mwanawe alikuwa amesimama chini ya ule mti akimtazama baba yake. Akamwambia, “Baba, si ingekuwa rahisi kupanda endapo ungekifungia chungu mgongoni?” Basi Anansi akajaribu kukifungia chungu kilichojaa hekima mgongoni mwake, na kweli ikawa rahisi zaidi.

Die ganze Zeit hatte Anansis junger Sohn unten am Baum gestanden und ihm zugeschaut: „Wäre es nicht leichter, wenn du dir den Topf stattdessen auf den Rücken bindest?“ Anansi versuchte es mit dem Topf auf dem Rücken und es ging in der Tat viel besser.


Punde tu alipofika juu ya mti, aliwaza, “Natakiwa kuwa ndiye mwenye hekima zote, lakini hapa mwanangu ndiye mwenye akili kuliko mimi.” Anansi alikasirishwa sana kiasi kwamba alikitupa kile chungu chini ya mti.

Im Nu erklomm Anansi die Baumspitze. Aber dann hielt er inne und dachte: „Ich soll derjenige mit der ganzen Weisheit sein und eben war mein Sohn schlauer als ich!“ Dies verärgerte Anansi so sehr, dass er den Tontopf vom Baum hinunter warf.


Chungu kilivunjika vipandevipande pale chini. Hekima zikawa za bure kwa mtu yeyote kujichukulia. Na hivyo ndivyo watu walivyojifunza kulima, kushona nguo, kuunda zana za chuma, na mambo yote mengine ambayo watu wanajua kuyafanya.

Am Boden zerbrach er in viele Stücke. Die Weisheit gehörte nun allen. Und so lernten die Menschen, Landwirtschaft zu betreiben, Tücher zu weben, Eisenwerkzeuge herzustellen und alles andere, was wir heute wissen.


Geschrieben von: Ghanaian folktale
Illustriert von: Wiehan de Jager
Übersetzt von: Mutugi Kamundi
Gelesen von: Lauwo George
Sprache: Kiswahili
Niveau: Niveau 3
Quelle: Anansi and Wisdom aus African Storybook
Creative Commons Lizenz
Dieses Werk ist unter einer Creative Commons Namensnennung 3.0 Lizenz lizenziert.
Optionen
Zurück zur Geschichteliste Schaltfläche PDF