Téléchargement PDF
Retour à la liste des contes

Anansi na hekima Anansi et la sagesse

Écrit par Ghanaian folktale

Illustré par Wiehan de Jager

Traduit par Mutugi Kamundi

Lu par Lauwo George

Langue kiswahili

Niveau Niveau 3

Lire l’histoire en entier

Vitesse de lecture

Lecture automatique du conte


Hapo zamani za kale, watu hawakujua chochote. Hawakujua kupanda mimea, hawakujua kushona nguo, wala hawakujua kuunda zana za chuma. Nyame, mungu aliyekuwa mbinguni, ndiye aliyekuwa mwenye hekima zote za dunia. Alihifadhi hekima hiyo kwenye chungu cha udongo.

Il y a longtemps, les gens ne savaient rien. Ils ne savaient pas comment ensemmencer et cultiver leurs champs, ou comment tisser, ou comment fabriquer des outils de fer. Le dieu Nyame dans le ciel avait toute la sagesse du monde. Il la gardait en sécurité dans un pot en argile.


Siku moja, Nyame aliamua kumpa Anansi chungu hicho cha hekima. Kila Anansi alipotazama ndani ya chungu cha udongo, alijifunza jambo jipya. Alifurahi sana!

Un jour, Nyame décida qu’il donnerait le pot de la sagesse à Anansi. Chaque fois qu’Anansi regardait dans le pot en argile, il apprenait quelque chose de nouveau. C’était tellement excitant !


Anansi mlafi alinong’ona moyoni, “Nitakificha chungu hiki juu ya mti mrefu ili nikifaidi mwenyewe.” Akasokota uzi mrefu na kuuzungusha kwenye chungu. Kisha, akajifunga tumboni. Akaanza kupanda kwenye mti. Lakini ilikuwa vigumu kupanda kwenye mti huku chungu kikimgonga magotini kila mara.

Anansi, l’avide, pensa: « Je vais garder le pot en sécurité en haut d’un grand arbre. Comme ça je pourrai l’avoir à moi seul ! » Il fila un fil long, l’enroula autour du pot en argile et l’attacha à son estomac. Il commença à grimper à l’arbre. Mais c’était difficile de grimper à l’arbre avec le pot qui lui cognait les genoux tout le temps.


Wakati huo wote, mwanawe alikuwa amesimama chini ya ule mti akimtazama baba yake. Akamwambia, “Baba, si ingekuwa rahisi kupanda endapo ungekifungia chungu mgongoni?” Basi Anansi akajaribu kukifungia chungu kilichojaa hekima mgongoni mwake, na kweli ikawa rahisi zaidi.

Pendant tout ce temps, le jeune fils d’Anansi était debout en bas de l’arbre en train de regarder. « Au lieu de faire ceci, ne serait-il pas plus facile d’attacher le pot à ton dos ? » Anansi essaya d’attacher le pot rempli de sagesse à son dos et ce fut vraiment plus facile.


Punde tu alipofika juu ya mti, aliwaza, “Natakiwa kuwa ndiye mwenye hekima zote, lakini hapa mwanangu ndiye mwenye akili kuliko mimi.” Anansi alikasirishwa sana kiasi kwamba alikitupa kile chungu chini ya mti.

En peu de temps il atteignit le sommet de l’arbre. Mais il arrêta et pensa, « Je suis censé être celui qui a toute la sagesse et voici que mon fils est plus sage que moi ! » Anansi était tellement fâché à propos de ceci qu’il lança le pot en argile en bas de l’arbre.


Chungu kilivunjika vipandevipande pale chini. Hekima zikawa za bure kwa mtu yeyote kujichukulia. Na hivyo ndivyo watu walivyojifunza kulima, kushona nguo, kuunda zana za chuma, na mambo yote mengine ambayo watu wanajua kuyafanya.

Le pot se cassa en mille morceaux sur le sol. La sagesse fut accessible à tous. Et c’est ainsi que les gens apprirent à cultiver, tisser, fabriquer des outils de fer, et toutes les autres choses que les gens savent faire.


Écrit par: Ghanaian folktale
Illustré par: Wiehan de Jager
Traduit par: Mutugi Kamundi
Lu par: Lauwo George
Langue: kiswahili
Niveau: Niveau 3
Source: Anansi and Wisdom du Livre de contes africains
Licence de Creative Commons
Ce travail est autorisé sous une licence Creative Commons Attribution 3.0 non transposé.
Options
Retour à la liste des contes Téléchargement PDF