Download PDF
Back to stories list

Tom muuza ndizi Tom the banana seller Tom le vendeur de bananes

Written by Humphreys Odunga

Illustrated by Zablon Alex Nguku

Translated by Matteo E. Mwita

Read by Lauwo George

Language Kiswahili

Level Level 2

Narrate full story

Reading speed

Autoplay story


Tom anabeba tenga la ndizi zilizoiva.

Tom carries a tray of ripe bananas.

Tom transporte un plateau de bananes mûres.


Tom anaenda sokoni kuuza ndizi.

Tom goes to the market to sell bananas.

Tom va au marché pour vendre des bananes.


Sokoni watu wananunua matunda.

People at the market are buying fruit.

Les gens au marché achètent des fruits.


Lakini hakuna anayenunua ndizi za Tom. Wanapenda kununua matunda kutoka kwa akina mama.

But no one is buying Tom’s bananas. They prefer to buy fruit from women.

Mais personne n’achète les bananes de Tom. Ils préfèrent acheter leurs fruits des femmes.


“Kwenye jamii yetu, ni wanawake pekee ndio wanaouza matunda,” watu wanasema. “Ni mwanamume wa aina gani huyu?” watu wanahoji.

“In our community, only women sell fruit,” people say. “What kind of a man is this?” people ask.

« Dans notre communauté, seulement les femmes vendent des fruits, » disent les gens. « Quelle sorte d’homme est celui-ci ? » demandent les gens.


Lakini Tom hakati tamaa. Anaita, “Nunua ndizi zangu! Nunueni ndizi zangu tamu zilizoiva!”

But Tom does not give up. He calls, “Buy my bananas! Buy my sweet ripe bananas!”

Mais Tom ne démissionne pas. Il crie, « Achetez mes bananes ! Achetez mes bananes mûres et sucrées ! »


Mwanamke mmoja anachukua kichane cha ndizi kutoka kwenye tenga. Anaziangalia ndizi kwa umakini.

One woman picks up a bunch of bananas from the tray. She looks at the bananas carefully.

Une femme choisit un régime de bananes du plateau. Elle inspecte les bananes soigneusement.


Mwanamke ananunua ndizi.

The woman buys the bananas.

La femme achète les bananes.


Watu wengine wanakuja kwenye kichanja. Wananunua ndizi za Tom na kuzila.

More people come to the stall. They buy Tom’s bananas and eat them.

D’autres personnes viennent au stand. Elles achètent les bananes de Tom et les mangent.


Mara, tenga linakuwa tupu. Tom anahesabu pesa alizopata.

Soon, the tray is empty. Tom counts the money he earned.

Bientôt, le plateau est vide. Tom compte l’argent qu’il a gagné.


Tom ananunua sabuni, sukari, na mkate. Anaweka vitu kwenye tenga lake.

Then Tom buys soap, sugar, and bread. He puts the things in his tray.

Ensuite, Tom achète du savon, du sucre et du pain. Il met les choses sur son plateau.


Tom anajitwisha tenga kichwani na kwenda nyumbani.

Tom balances the tray on his head and goes home.

Tom balance le plateau sur sa tête et rentre chez lui.


Written by: Humphreys Odunga
Illustrated by: Zablon Alex Nguku
Translated by: Matteo E. Mwita
Read by: Lauwo George
Language: Kiswahili
Level: Level 2
Source: Tom the banana seller from African Storybook
Creative Commons License
This work is licensed under a Creative Commons Attribution 4.0 International License.
Options
Back to stories list Download PDF